Tetesi: Wachezaji watano wa Simba wasimamishwa kupisha uchunguzi kwa kichapo kikali cha goli 5 kutoka kwa Yanga

Sisi watz ni wanafki sana, badala ya Simba kukubali Ukweli kuwa Yanga ni ya moto na viongozi wa Simba wameshindwa kazi ya kusajili eti wanaenda kutoa kafara wachezaji na kocha!

Huu ni uonevu viongozi ndio watoke wapishe uchunguzi! Kufukuza kocha na kusimamisha wachezaji ni lengo la viongozi kuficha ubovu wao!

Wachezaji wa Simba wamechoka na hawana uwezo wa kiakili kushindana na vijana wa Yanga kina Ki Aziz na Max Nzegeli , timu ya Simba ni Ile Ile kwa msimu wa tano Sasa. Hebu angalia Yanga mchezaji Gani Bado yumo kikosini kwa misimu mitano?

viongozi wa Simba watoke wao kwa kushindwa kazi na sio kutafuta kichaka Cha kujificha kwa kubambikia kesi wengine!
 
Wamesajili wachezaji viwango vyao ni duni
 
SOURCE YA HII TAARIFA NI PRISCA KISHAMBA.

wanatafuta watu wa kuwaangushia jumba Bovu ila simba hakuna msafi hata mmoja.


Tatizo la simba ni kuanzia.
1. Muwekezaji.
2. Mwenyekiti mangungu.
3.Try again.
4. Body ya wakurugenzi
5. Management.
6.Benchi la ufundi lote.
7. Scout analyst,nk
8. wadau.
9. Washauri wa Bodi.
10 mashabiki mbumbumbu
Akitolewa chama wanalia na kuzomea pmf sana, wanamlilia miquisson kurejeshwa, Adebagor na manzoki.
 
Na kama sio kweli basi ni wakati sasa wa viongozi wa Simba kuwa "serious" kwa kumtafuta aliyezusha halafu wamchukulie hatua kali sana za kisheria. Hili jambo sio dogo kabisa wasiliache lipite hivi hivi na liwe onyo kwa wengine wote wanaochezea "brand" yao.
 
Reactions: Tsh
Mwandishi wa hii habari ni Prisca Kishamba, yule dada aliewahi kutukanagwa na Haji Manara mpaka media nyingi zikapigia kelele hilo jambo.

Since ni mtu anajulikana means rahisi tu kumuita na kumuuliza
 
Kweli
 
Mo siku zote anasema kuna watu wanamkwamisha ni wakati sasa awataje ili sisi wanachama tuanzie hapo. Asipowataja kipindi hiki lawama atabeba yeye kwa kuwafuga wahujumu wa timu yetu
 
Mwandishi wa hii habari ni Prisca Kishamba, yule dada aliewahi kutukanagwa na Haji Manara mpaka media nyingi zikapigia kelele hilo jambo.

Since ni mtu anajulikana means rahisi tu kumuita na kumuuliza
Hiyo haitoshi yanajirudia mara kwa mara. Simba ni "brand" kubwa sana Afrika na duniani kwa sasa na ina wadhamini wengi wemeweka pesa zao nyingi wakitegemea kupata faida kwenye biashara zao. Sasa watu wa namna hiyo wakiachwa waharibu "brand" ya watu halafu waachwe hivi hivi huku timu ikipata taharuki kwa wadhamini na kuharibu saikolojia ya wachezaji sio sahihi kabisa. Huyo ashtakiwe hata kama sio mahakamani basi hata kwenye baraza la habari ili iwe fundisho kwa waandishi wote wanaopenda kuzusha mambo hasa yanayozihusu timu hizi mbili kubwa Simba na Yanga bila kujua upuuzi wao ipo siku utaletya maafa.

Swali kubwa kabisa je baada ya kupata hiyo stori alienda kuuliza upande wa viongozi wa Simba? Au kwa kiherehere chake alikimbia mbio kuiposti mitandoni awe wa kwanza kuto "breaking news". Yote kwa yote alipaswa kujua taarifa yake iwe kweli au si kweli lazima ilete taharuki kwa sababu Simba ina wapenzi na wanachama kwa mamilioni Tanzania, Afrika na Duniani kwa ujumla kwa hiyo alipaswa kufuata miiko ya uandishi wa habari hasa ikizingatiwa ni mwandishi wa muda mrefu kwa hiyo anajua madhara ya kila ambacho atakipeleka kwenye jamii.
 
Safi kabisa.... haiwezekani wacheze kama Mashoga. Watu hawajitumi na hawana uchungu. Nashangaa kwanini wamemuacha BALEKE. na yeye angejumuishwa matako yule
 
W
Hebu tuache uswahili Tanzania!!
1. Chama anayetuhumiwa si ndo amepiga faulo ambayo ilizaa kona na baadae goli la simba?
2. Inonga amefanyaje?
3. Ukitazama magoli yote matano simba wanapokwa mipira/intercepted passes watu wanaenda kufunga
We pimbi kweli...unafkiri kwa aina hyo ya utazamaji utajua match fixing..??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…