Wachezaji wazamani wa Simba ambao walikuwa mashabiki wa Yanga na wachezaji wa zamani wa Yanga walio kuwa mashabiki wa Simba

kwenye Maisha yoote ya kucheza mpira, Bakari Malima 'jembe ulaya' hajawai chezea / hamia / sajiliwa na simba …………..
Acha ubishi.


Fungua hiyo link hapo usome.
 
Dua Said na Thomas Kipese (uncle Tom) waiitesa Yanga sana, walikuwa wanafunga karibia kila gemu.
Kipese alienda simba mwishoni sana..alieavuruga sana simba...Dua ndio alikuwa mwiba sana kwa Yanga.
 
Nteze John Lungu nilisoma naye darasa na kucheza naye mpira timu ya darasa pale Mzimuni Primary School, Magomeni, alikuwa shabiki mkubwa wa Yanga, nilishangaa alipoenda kujiunga na Simba na kucheza kwa mafanikio Simba.

Vv
 
Mshindo Msolwa ni Simba Lia Lia ,Gharib wa GSM ni Simba Lia Lia ,Manji ni Simba Lia Lia ,baada ya kukosa nafasi Simba wakaenda kuongoza Yanga ,kuna muda nacheka kimya kimya tukiwa pale VP tunaangalia mpira,mechi ya Simba na Yanga waangalie namna wanavyoshangilia magori
 
Na hizi timu zilivyokuwa nuksi hata uwe mwenyekiti yanga lkn mapenzi yako kama yapo kwa simba ikifungwa lazima uumie,, kama manara anvyoenda kuchekea chooni sasa ivi
 
Nilisikia kipindi cha Simba ile ya njaa Manara alimfata GSM kumshawishi asurpport
 
Naam..Adeyum Alipopata nafasi ya kucheza simba baba yake alishangilia sana kwamba afadhali mwanae nafsi itatulia kwa kupata timu ya ndoto yake... akamleta mwenyewe mpaka dar kumkabidhi kwa kina Kaburu.
 
Haji Manara lia lia wa simba lakini domo limeajiriwa utopolo na anaupiga mwingi!! Akizidiwa anaenda kujificha chooni na kuwacheka utopolo original!!
[emoji3][emoji3][emoji3]huwa anawacheka wakifungwa
 
Nteze John Lungu nilisoma naye darasa na kucheza naye mpira timu ya darasa pale Mzimuni Primary School, Magomeni, alikuwa shabiki mkubwa wa Yanga, nilishangaa alipoenda kujiunga na Simba na kucheza kwa mafanikio Simba.

Vv
Very interesting. Ila wachezaji wote wa kibongo ndoto zao huwaga Ni kuchezea Simba au Yanga Na wengine huwa wanajikuta wanapata mapenzi ya timu waliyo ichezea kutokana Na mafanikio watakayo yapata Na timu husika. Mfano Lunyamila inasemekana utotoni alikuwaga Simba Lia Lia but at the end of the day baada ya kuchezea Yanga akajikuta na yeye anahamia Yanga kimapenzi. Sasa hivi anajitanabaisha kama shabiki wa Yanga
 
Lazima wewe ni uto fc maana uandishi wako ni wa kujipa faraja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…