Wachungaji kutaka fungu la kumi kwa lazima

Wachungaji kutaka fungu la kumi kwa lazima

Wakuu habarini

Mimi ni muumini wa kanisa la mahali pamoja ambalo ni T.A.G(X)

Jana nimepokea ujumbe wa kunikwaza kunifedhehesha na kunifanya nione kama natwaga maji kwenye kitu

Jana mchungaji kanitumia msg akiniuliza mbona sijahudhuria jana kanisani? Au na mpango wa kuhama kanisa !!

Nami 'nikamjibu kwa kumpigia simu nikamwambia mbona nilikuandikia msg kuwa nadharula sitahudhuria ibadani hukuupata ujumbe na nilimtumia pia na mzee nikakata simu nikascreen short msg nikamtumia whatsap

Akanijibu kuwa dharula zipo ila kama ni siku ya ibaada utume sadaka na michango , ni muhimu sana nikaa kimya

Leo Asubuhi nimeamka asubuhi nikiwa na ratiba ya kutoka kumpeleka mama yangu mzazi cliniki ya dialysis Bugado wakati natoa kausafiri kwenye chasis number alikuwa anapita tukasalimiana na kumwambia tunaelekea Hospital akasema sawa na hongera nyingi za kunua kausafiri kapya.

Imefika saa nne nipo hospitali naona Msg tena
akiniandikia ujumbe unasomeka hivi"

Leo ni mwisho wa mwezi na jana haukuwepo ibadani Tuma sasa hivi FUNGU LAKO LA KUMI UTUME NA HELA YA KUTOLEA KANISA LINA MADENI MENGI ""

Nikausoma nikatulia nakuvuta pumzi nikamtumia msg KUWA KWA SASA SINA PESA, FEDHA NINAYOBAKIA NAYO NI KWA AJILI YA MATUMIZI MUHIMU YA FAMILIA NAJUA PIA ZAKA UMUHIMU WAKE, nikikaa sawa nitatoa wala haina shida na hapo ndio nilikuwa najiandaa kulipia matibu ya mama kila mwezi natakiwa kulipia Milion 3 .8 kwa ajili ya dialsis ,mwez huu mambo yameyumba kabisa .

Akajibu tena wewe unabadili tu magari kwa habari ya zaka hutaki kutoa nikamwambia kwani zaka ni lazima lini sijatoa zaka zaidi ya mwezi huu nimepata msiba, na unanihusu kwa sehemu kubwa sina fedha na ninauguliwa wewe mwenyewe shahidi hali ya mzazi wangu Muda wote gari inapaswa kuwa na mafuta, muda wowote hali inabadilika tukawa tumeachana hivyo

Sasa hebu mnisaidie huu utaratibu unatoka wapi kwanini sadaka na zaka ni lazima au ni vile mtu anavyoguswa kulingana na Vile anavyopata! Maana Mungu anasema nijaribu sasa huku Naona mchungaji anatumia command utadhani kanipa yeye kisa anamadeni.

Hebu nipeni njia itakayoniondoa kanisa mikwaruzo na Mchungaji
Acha kulalamika hapa ndugu makanisa ya T A G ni mengi rafiki ama kabisa tafuta kanisa lingine la TAG.Sifa kubwa ya mchungaji ni kuwa na huruma.
 
Hapa kuna kitu hakiko sawa kwenye mambo ya imaini. Kwanza nakupa pole kwa huo usumbufu kutoka kwa mchungaji wako kiimani. Pili sisi wanadamu tunatakiwa kujitafakari na hizi imani zetu za kiroho sasa hivi wanadhihirisha ule msemo wa nipe Yesu nikupe ardhi yangu. Yaani huyo Yesu amekuwa ndiyo silaha kubwa inyotumika kuwapora watu kwa nguvu mali zao, unakutu eti pasta sijuhi mchungaji anakuombe kwa huyo Yesu kisha anadai pesa kwa kutamka vijineno eti nakuponya kwa jina la Yesu kisha ankinga mkono ulichonacho utoe. Mtu kila siku atoa hiyo sadaka mara fungu la kumi tena kwa nguvu lakini anadumu fukara na mchungaji anaedesha v8 .
 
Wanaume mnaojielezea Sana mnakera

Endelea kutoa zaka acha kujilalamisha
Umeamua mwenyewe.
Hakuna mtu anatoa zaka hapa kama mwanaume hata tukienda bar zaka tunatoa mara ninunulie moja tunanunua nayo ni zaka pia
 
Mwanaume mzima unaenda kwenye makanisa ya kitapeli....hayo wanaenda wanawake tu, ndio wenye akili za kutapeliwa
Acha uzwazwa, kuna nyumba ya ibada isiyokuwa na matoleo ? Mbona mnatoa kwa waganga wa kienyeji wakati mnapunga majini ? MPE Bwana Yesu maisha yako.
 
Acha uzwazwa, kuna nyumba ya ibada isiyokuwa na matoleo ? Mbona mnatoa kwa waganga wa kienyeji wakati mnapunga majini ? MPE Bwana Yesu maisha yako.
Huyo Yesu uliwahi kumwona? Ama ni zile picha za Hollywood na sinema zao za kutumpubaza akili eti Yesu mweupe alitoa maisha yake kufa kwa wewe mweusi. Wewe unajuaje kuwa huyo Yesu unayemwabudu hakuwa mganga wa kiyenyeji.
 
Nielimisheni kifungu cha zaka la kanisa kinasemaje.
 
itapendeza kama makanisa yakawa yanalipa kodi maana skuhzi zaka zinafosiwa
mfano mm nina kadi ya jengo kwenye kanisa letu na kila nikienda kanisani nachuma mchicha napeleka kama sadaka ukipigwa mnada wanaandika pale ila muinjilisti akaniita skumoja akaniambia utoaji wangu ni hafifu nkamuuliza mungunkanibariki mchicha kwahiyo nisimshukuru kwa bidhaa alio nibariki nayo akaniambia sawa mchicha mungu kakubariki nao ila unatakiwa utoe hela nyingi zaidi ya hyo ya mchicha nkamwambia nakuheshimu kwakua upo kwenye vazi la kanisa ila usije ukaniongelesha haya mambo ukiwa upo nje ya kanisa nkasepa .
hvi wanataka tutoe roho zetu ama maana wanaona tunachotoa kidogo sana wakat hawana kodi wala malipo wnaayofanya kutokana na wanachoingiza
Mchicha haaahaaahaaa [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Nielimisheni kifungu cha zaka la kanisa kinasemaje.
Ni project tu za watu kuwajaza hofu watu wazembe na wajinga kujipatia kipato.

Mungu hajaumba pesa na wala hana shida ya pesa yako.
 
Fungu la kumi ni ya kwanza kabisa, kabla hujapanga bajeti yako

Unaweza kuona ni shida ya mchungaji anataka hela lakini zaka ni ya Mungu na agizo

Lakini utoe kwa hiyari na si kwa kulazimishwa

Na usipotoa ni kosa kubwa.

Unaweza endelea uguza mpaka senti yako ya mwisho

Zaka inaweza kukulinda na ugonjwa wa mama na matatizo mengine.

Lakini pia kama unajua vizuri kuhusu sadaka, unatoa tu hata kama huendi kanisani

Kwani sh ngapi jamani inakuuma? Unatoaga sadaka kubwa sana?


Si unatuma tu hata elfu 2, buku, tano, kumi.
Nyie watu mmevurugwa sana na hili fundisho la Zaka... Eti Zaka inaweza kumlinda mama na ugonjwa... Kwa hiyo ni unanunua uponyaji kutoka kwa Mungu?

Yaani ili Mungu amponye mama yake, inabidi yeye atoe Zaka... kwa hiyo ni nipe nikupe kati ya mwanadamu na Mungu???

Amkeni nyie watu, Hakuna mahali popote pale ambapo Mungu amekuagiza wewe mtu usiye chini ya Torati kutoa Fungu la Kumi.. HAKUNA.

Hiyo Malaki 3:10 ni mkazo wa fundisho la Torati, wewe upo chini ya Torati?
 
Toa fungu la kumi litakulinda na magonjwa hata bi mkubwa anaweza kupona huo ugonjwa unaokula Hela , maana tunajua MUNGU akuleta magonjwa duniani magonjwa ni ya shetani , msikilize Mchungaji wako utanishukuru.
Kwa hiyo Mungu anahitaji hela yako(Zaka) ili akuponye!!!!

Yani ili Mungu akulinde wewe, anahitaji umpe hela!!

Nyie watu mtaendelea kuliwa hela zenu mpaka lini?
 
Back
Top Bottom