Wachungaji mnaosema tukiwapa sadaka tutabarikiwa kuwa wateja wa kwenye ma Mall, mnajiona mko sawa?

stroke Chief hakuna anayekataa kuwa wachungaji wanapaswa kuhudumiwa na waumini sababu principally hawana kazi zaidi ya kuwahudumia waumini kiroho.

Kinachotia ukakasi ni uhalisia wa maisha na mahusiano ya mchungaji na waumini wake. Kwa sasa wachungaji wanajilimbikizia mali na sio kuhudumiwa ili kuhudumia waumini. So, kanisa kwa sasa ni mfumo wa kinyonyaji ambapo kuna kakikundi kadogo kanaishi, kuneemeka na kutajirika kwa jasho la watu wengi(waumini). Ni kama ile hadithi ya Animal Farm.
 
Kumbe wewe BMW huipendi!? Basi endelea kupanda daladala & bajaji sisi tunaotaka Benz ngoja tubarikiwe
Mkuu samahani ila kuna muda nakuona kama una matatizo makubwa hasa sehemu ya ubongo wako maana comments zako zinatia shaka.

Ni kama mtu aliyekata tamaa kutokana na kuumizwa mara kwa mara (multiple abuse).
 
Hao uliowataja wewe kwenye biblia sadaka zao walikuwa wanaenda kununulia Benz na Range rovers?na zingine walikuwa wanaenda kulipia lodge kulala na wake za watu?
 
Kuna siku tulikua kanisani, unajua mahibiri ya walokole ni mpaka mchungaji achoke kuongea. Imefika saa saba mahubiri yanaendelea na mke wa mchungaji anakunywa Coca-Cola kupoza koo.
[emoji23][emoji23][emoji23] duh! Mkuu nahisi ukamezea ka mate kidogo.
 
Sijatumia nguvu kuwatetea nilikua natoa maelezo kulingana na ufahamu wangu wa Biblia.

Mkuu, kama kutoa sadaka unaona unaibiwa Acha na kanisani usiende it's your choice.

Ila Mimi sitaacha kutimiza wajibu wangu so long as naamini ni miongozo sahihi ya Mungu kupitia kitabu chake kitakatifu (biblia).

Until then kila mtu abakie na msimamo wake, na apambane na hali yake.

Kama Mchungaji yeye anatumia abuse mahusiano yake na waumini wake it is entirely up to him with his God,

Ila kutimiza wajibu wangu kama mkristo sitaacha,

Nafahamu mambo mengi Sana yanayoendelea nyuma ya pazia kwenye taasisi za dini iwe ni wakristo au waislamu ila Mimi hayo hayanihusu ninachoangalia ni mahusiano yangu na Mungu pekee.

Adios.
 
Ndo mana nikasema dini ya mfumo wa madhehebu ni utapeli mtupu....
 
Ndo mana nikasema dini ya mfumo wa madhehebu ni utapeli mtupu....
It is absolutely impossible to separate religion from dhehebu, kama ambavyo huwezi separate an atom from matter. Dhehebu ni subset ya religion. Will you please consider adjusting your mental windshield, sawa!???
 
Mkuu samahani ila kuna muda nakuona kama una matatizo makubwa hasa sehemu ya ubongo wako maana comments zako zinatia shaka.

Ni kama mtu aliyekata tamaa kutokana na kuumizwa mara kwa mara (multiple abuse).
You are telling me kwamba comments zangu lazima ziafikiane na disposition yako, siyo!???
 

Kazana kutoa

Utabarikiwa!!!! LoL
 
Imani na ulimwengu wa roho Ni mpevu zaidi kuliko upeo wako wa kufikiri. Kanisani kwenyewe unatoa jero au Mia halafu unapiga kelele.Wewe hata hujiulizi ulipata wapi Akili ya kutafuta pesa Ila unajiuliza kwanini unatoa sadaka
Dah!! Nashukuru sana mkuu vipi kuhusu upeo wako na imani?? Aaaa naona wako ni mkubwa kuliko imani ndiyo maana hujui hata imani ni nini!!! NONSENSE [emoji57]
 
Upo sahihi, lazima sadaka ziwepo ili watumishi na wao waendeshe maisha yao.
 
Kuna siku tulikua kanisani, unajua mahibiri ya walokole ni mpaka mchungaji achoke kuongea. Imefika saa saba mahubiri yanaendelea na mke wa mchungaji anakunywa Coca-Cola kupoza koo.
Ifike mahali akili za watu zifunguke, Hivi mtu anashindishaje watu siku nzima kanisani bila kujali mahitaji yao ya msingi na watoto wadogo wanahitaji kula na wamama wanaonyesha hata wazee na wagonjwa, Alafu Mungu anatuhitaji tupumzike siku ya Saba yaani tuenjoy na kurelax, Sasa mtu siku ya kupumzika anambiwa akashinde kanisani mpaka anachoka, kwakweli wabadilike maana akili za watu zikiujua ukweli wa biblia watakosa waumini.
 
na ndio hii kitu ilinifanya niachane na makanisa eti mchungaji achangiwe hela ya gari wakati mm kula yangu ni mtafutano..
Nakubaliana na wewe hilo swala la michango siyo haki kabisa hata sadaka yakutoa kwenye kikapu Ili usionekane umebaki kwenye siti ni ubatili, waweke matoleo ya mwisho wa mwezi Kila muumini achangie Kama kwenye kikundi maana kanisa ni sehemu ya kufundishia Kama shule na siyo hekalu Kama yaliyokuwa yanajengwa zamani kwaajili ya uwepo wa Mungu na Sheria zake na wahudumu wa mahekalu wakiwa bikira na walipelekwa kulelewa mazingira ya ucha Mungu tangu kuzaliwa kwao hata mavazi yao yalikuwa spesho na hekaluni ndiko walikuwa wanaombea kwa kuwasiliana na Mungu na jibu lako unapata pale pale.
 
Dini iliyosafi nikuwajali mayatima na wajane so dini zilitakiwa ziwe vikundi vya kutoa misaada ya mayatima na wajane so sadaka zingetolewa kitu chochote alichonacho mtu kwaajili ya kuwezesha hao watu hawamunungunikii Mungu upweke wao, kwa kipindi cha Sasa hakuna Makuhani, ndo maana Kila mtu anajipa jina lake, kwenye utafiti wako muangalie Suleiman mwana wa Daudi utajua Mungu yupo Ila kwasasa hakuna mtu amejenga Hekalu sehemu za kwenda kwaajili ya kuvuta uwepo wa Mungu na kusema naye na watumishi wa mahekalu ni mabikira Ila hizi sehemu za mafundisho zilitakiwa zijitofautishe na kujiita dini, nazo zijipe majina yao.
 
Kwani Masheikh wanaishije? tusijustify wizi...sadaka atoe mtu kama anacho tu...siyo kulaghai waumini...na kuwatisha kwa vifungu vya bible,huu ni utapeli.
Ww kwani umelazimishwa kutoa? Kama unahisi unaibiwa piga chini, wacha kelele zko za kitoto.
 
Bora sadaka tuwape watoto yatima,tukiwapelekea sabuni,sukari,madaftari,kalamu n.k baraka unaziona waziwazi
Na dini ndo zimeteka hiyo nafasi na ndo maana hao watu hawapati huduma ya kuhudumiwa Kama Mungu anavyotaka na hapo ndipo sadaka ya mtu inapompa matokeo ya baraka za maisha ya kawaida, hata serikali inazisajili Kama taasisi za kufundisha na ndo zinatakiwa kujiita hivyo taasisi za kufundisha na walipwe mishahara ya kufundishia Kama walimu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…