Wadada mnajisikiaje mnapo tongozwa na mkaka ambaye humjui Wala yeye hakujui?

Wadada mnajisikiaje mnapo tongozwa na mkaka ambaye humjui Wala yeye hakujui?

Brigadier Isaac

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2021
Posts
495
Reaction score
1,436
Habari zenu members wote was jamiiforum pia poleni na mahangaiko

Mimi nina swali hasa kwa wadada kuhusu wanavyojisikia wanapo tongozwa na mkaka ambaye humjui Wala yeye hakujui Ila ndio hivyo mkaka ameamua kuja mpaka ulipo na kukuambia amevutiwa na wewe baada ya maongezi machache kutambulishana

Nimeuliza hivi kwa sababu Mimi ni introvert pia kwenye social circle yangu almost Hamna jinsia ya kike kiufupi sijawahi kua na rafiki wa kike kwenye maisha yangu ,rafiki wangu wote wengi ni wa kiume ndivyo nilivo naona uzito Sana kua na rafiki wa kike ni kitu ambacho sijazoea

Njia yangu kubwa ya kupata mademu natumia Sana cold approach
Kiukweli naona nafuu zaidi kutongoza mdada hapohapo kuliko kuanzia kwenye urafiki mpaka baadae kuja kufunguka mpaka Leo sijajielewa Nina shida gani Tena napenda kutongoza wanawake wa mbali kuliko karibu kiufupi wanawake wa maeneo ya karibu hata iweje si mtongozo ng'o

Shida inakuja nimekuja kugundua wanawake wengi wanashutka na kushangaa Sana pale mkaka hakujui Wala hakufahamu hata kidogo halafu umtongoze Tena kwa confidence wanakuwa na wasiwasi mpaka wengine wanakataa au anakupa namba halafu hajibu message
Ndio leo nimeona labda niwaulize nyie wenyewe wadada maana sitaki kuanza kuweka lawama kwa warembo kumbe Mimi mwenyewe njia ninayo tumia labda sio maana mdada anaonyesha ushilikiano wakati na mtongoza shida inakuja mda mwingine hawaoneshi ushilikiano baada ya kukupa namba Tena Cha kushangazwa hata mizinga sijawahi pigwa yangu nimeanza kutongoza😂 Sijui Kuna nini?

images (11).jpeg

images (13).jpeg
 
Uongo umeanzia hapa ;
Nimeuliza hivi kwa sababu Mimi ni introvert pia kwenye social circle yangu almost Hamna jinsia ya kike kiufupi sijawahi kua na rafiki wa kike kwenye maisha yangu ,rafiki wangu wote wengi ni wa kiume ndivyo nilivo naona uzito Sana kua na rafiki wa kike ni kitu ambacho sijazoea
Unaishia hapa;
Njia yangu kubwa ya kupata mademu natumia Sana cold approach
 
Back
Top Bottom