Wadada, niulizeni kitu chochote kuhusiana na huduma za salon, hair & nails

Wadada, niulizeni kitu chochote kuhusiana na huduma za salon, hair & nails

Hapana hutaitaji kusubiri tena...natural hair ikishajitokeza basi unazitream kidogo tu kisha unaanza kuweka permanent curl yako
Samahani nakuuliza maswali mengi kwani nimechoka kuweka relaxer . Umegusia kuzitreat nywele kidogo je nazitreat na nini tafadhali nijibu kileiman nataka kuelewa ili nifanye mwenyewe. Nakumbuka ilikua june nilienda salun flani hapa napoishi nikataka curl lkn mtaalamu akaniambia haiwezekani kwani nywele hata kama zimeota haimaanishi kama hazina dawa nikachanganyikiwa manake nilikua nimekaa 6 months na nywele zilikua kipili pili kabisaa, majibu sikuridhika nayo ikabidi niwekeke tena relaxer kitu ambacho ssikukipenda kabisaa. Leo nimeshukuru kukuta hapa kuna mtaalamu so please nsaidie mwenzio kwani ujuzi unatofautianakwani huyo mdada sikuridhishwa hata na utendaji wake wa kazi. Swali jengine je apart from kuweka curl kuna option nyingine ya kufanya . Yaani nywele natural naweza weka dawa gani isiyo na madhara makubwa na ambayo naweza kuweka mwenyewe bila kwenda salun.
 
Ni mafuta gani yanafaa kufanyia massage hasa kwa nyumbani?
Mkuu sorry for my late reply bado niko kazini na busy kidogo...so tuvumiliane.

Okay, unapenda massage gani? thai,soft,au hard massage? Nijibu ili nijue ni mafuta gani yakupasa utumie.

Mwisho...unasumbuliwa na sehemu gani mwilini kiasi kwamba unahitaji massage? I mean viungo
 
Mimi nimeanza kufunga nywele last year mwez wa tano na hadi now nimeeka dawa mara mbili tu..bt nywele zinawahi sana kuotea yani na siwezi kuretouch mara kwa mara koz nimejiekea tabia ya kuretouch kila baada ya 3 months.natumia dark and lovely na nywele zangu ni kipilipili sasa sijui ndo sababu
 
Hakuna ubaya...lakini je hiyo Dr miracle mara ya mwisho umeweka lini? Hiyo Olive oil yakupasa uweke baada ya miezi miwili
au mitatu tokea uachane na hile ya kwanza.

Swali: nywele zako ni laini au ngumu?

Dr miracles ndo nimeweka November hii,nilitumia mega growth ikadunda,Miracles imenikubali kwa kweli maana nywele zangu ni ngumu kwa kweli.Nikiretouch feb mwakani no nataka niswitch to Olive oil
 
1.nywele zangu ni dreads ni nguuuuuumu hiiizo eheheh?,
nafanyaje ziwe soft na zikue fastaa?naweza kufanya steaming?
(kinaturale lakini madawa nehiiiiii)
2.vipi kuhusu ngozi,nina oliy face nafanyaje,situmii mafuta yoyote! jouneGwalu njoo ulipe bills huku!
 
Last edited by a moderator:
Na vipi kuhusu nywele zilizokatika kwa usoni?nisuke nywele gan ili zikue haraka yani nakua uncomfortable nikifumua nasuka apo apo siwezi kuziachia koz zinaleta show mbaya
 
mpenzi niko na dry scalp sijui yaan sijielewi au ni mba tuu bt nimetumia sulphur 8, sijui virgin na radiant sijapata mafanikio nitumie nn. nywele yangu ina dawa.
pole sana mpenzi wangu...wewe yakupasa uanze hair clinic ya Special treatment kwa miezi mitatu(3) I mean ndani ya kila mwezi mmoja utaifanya mara mbili. So jumla utaifanya mara 6 ndani ya miezi 3
 
Wapenzi,nawaombeni tuvumiliane kidogo kwani ndugu yenu bado nipo kazini na busy kidogo
Ila ninawahaidi nitajibu kila swali ambalo litakuwa ndani ya uwezo wangu...so endeleeni kuuliza lakini na pia muwe wapole
wa kusubiri majibu yenu.

Nakuhakikishieni kupitia thread hii mtapata mambo mazuri sana kwa faida ya mwili wako na urembo wako.
 

Attachments

  • image.jpg
    image.jpg
    471.2 KB · Views: 1,132
nywele zangu hazina dawa lakini zinakatika sana, naweza nikazitreat kwa kutumia nini ( bila kuweka dawa tafadhali)
 
ukija unambie dawa ya kuondoa madoa na makovu mwilini.
ile ambayo haina kemikali tafadhari..nina ngozi veery sensitive
 
Samahani nakuuliza maswali mengi kwani nimechoka kuweka relaxer . Umegusia kuzitreat nywele kidogo je nazitreat na nini tafadhali nijibu kileiman nataka kuelewa ili nifanye mwenyewe. Nakumbuka ilikua june nilienda salun flani hapa napoishi nikataka curl lkn mtaalamu akaniambia haiwezekani kwani nywele hata kama zimeota haimaanishi kama hazina dawa nikachanganyikiwa manake nilikua nimekaa 6 months na nywele zilikua kipili pili kabisaa, majibu sikuridhika nayo ikabidi niwekeke tena relaxer kitu ambacho ssikukipenda kabisaa. Leo nimeshukuru kukuta hapa kuna mtaalamu so please nsaidie mwenzio kwani ujuzi unatofautianakwani huyo mdada sikuridhishwa hata na utendaji wake wa kazi. Swali jengine je apart from kuweka curl kuna option nyingine ya kufanya . Yaani nywele natural naweza weka dawa gani isiyo na madhara makubwa na ambayo naweza kuweka mwenyewe bila kwenda salun.
Pole sana mpenzi…kwanza nimegundua unapenda kubaki natural hair.
So kama nywele zako ni ndefu kidogo basi ningekushauri uwe unafanyiwa hair brush (siyo hair boldry) na hiyo utaipata kwenye salon kubwa kubwa zenye wafanyakazi maprofesional na kama hair natural zako bado fupi basi nakushauri uweke permanent curl ya Wave Nouveau.
 
ukija unambie dawa ya kuondoa madoa na makovu mwilini.
ile ambayo haina kemikali tafadhari..nina ngozi veery sensitive
Oooh pole sana wangu!…je umewahi kwenda hospital na kuonana na doctor? hili liko nje ya uwezo wangu na ningependa
ukaonane na doctor
 
nywele zangu hazina dawa lakini zinakatika sana, naweza nikazitreat kwa kutumia nini ( bila kuweka dawa tafadhali)
Umewahi kuweka hair treatment yoyote before? kama bado unaweza kuanza na Dr miracle hair treatment kwa mwezi mara 2 au 3…lakini itakuwa vizuri kama utaanzia salon yoyote ilimradi iwe na huduma mzuri na siyo bora huduma
 
Umewahi kuweka hair treatment yoyote before? kama bado unaweza kuanza na Dr miracle hair treatment kwa mwezi mara 2 au 3…lakini itakuwa vizuri kama utaanzia salon yoyote ilimradi iwe na huduma mzuri na siyo bora huduma

Hapo saloon kwako mna huduma ya ZAZUU au KALIKITI?Maana dada yangu katoka kijijini juzi anahitaji huduma hiyo!
 
Na vipi kuhusu nywele zilizokatika kwa usoni?nisuke nywele gan ili zikue haraka yani nakua uncomfortable nikifumua nasuka apo apo siwezi kuziachia koz zinaleta show mbaya
Pole sana mpenzi wangu…mara nyingi unashonea weaving au kusuka kwa kutumia rasta au salsa na mitindo tofauti?
Ila kutokana na tatizo lako naweza guess kuwa unapenda sana kushonea weaving.

Sasa ushauri wangu kwako ni huu…jitahidi usishonee weaving wala kusuka marasta kwa kipindi cha miezi mitatu na wakati huo huo make sure nywele zako unazifanyia normal steaming tu hata kwenye salon za kawaida kwa kipindi hicho cha miezi 3. nakuhakikishia ukiziacha hizo nywele zako kwa kipindi hicho huku kizipata hiyo treatment basi nywele zako zitakuwa msitu na utaanza kushonea tena bila kukatika nywele zako
 
Hapo saloon kwako mna huduma ya ZAZUU au KALIKITI?Maana dada yangu katoka kijijini juzi anahitaji huduma hiyo!

Haha haaa…nani kakuambia mimi nipo salon?
Anyway hiyo Zazuu siijui na hiyo Kalikiti now days ni zilipendwa…labda mpeleke salon za uswahilini.
Kama unaswali jingine karibu sana mkuu
 
Pole sana mpenzi…kwanza nimegundua unapenda kubaki natural hair.
So kama nywele zako ni ndefu kidogo basi ningekushauri uwe unafanyiwa hair brush (siyo hair boldry) na hiyo utaipata kwenye salon kubwa kubwa zenye wafanyakazi maprofesional na kama hair natural zako bado fupi basi nakushauri uweke permanent curl ya Wave Nouveau .

Asante sana kwa kujitolea muda wako wa thamani kutushauri kwani muda ni mali. Nitajaribu kwenda saloon tena mpendwa.
 
Back
Top Bottom