Wadau, vazi la dera linafaa kwa mpenzi/mke wa mtu?

Wadau, vazi la dera linafaa kwa mpenzi/mke wa mtu?

NIMEONA

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2019
Posts
3,862
Reaction score
5,693
Mtu wangu anapenda sana vazi la dera; akitoka ni dera tu na mara chache ni sketi au gauni.....anasema kanga au kitenge haviwezi kuvaa kwa maana hajavizoea na huwa vinampa shida sana anapovaa safarini ikiwemo kutomshika vizuri hali inayopelekea kutaka kumvuka hivyo kumkosesha utulivu.

Katika hisia zangu, ndani kabisa huko kwenye akili, silipendi vazi hili kwani mi huwa naona ni kama vazi fulani la kihuni hivi........wanaosasambua huko uswahilini nawaona wakipendelea sana madera; mashangingi nawaona wakipendelea sana madera (kama sikosei); n.k.

Maoni yenu wadau, maana isije ikawa ni 'ushamba' unanisumbua na hatimaye ukaniharibia mahusiano siku moja
 
Vazi la dera ni zuri mwanamke akivaa na kitu kingine ndani,,,
Lakini akivaa dera bila kuvaa kitu lingine ndani ni mtihani mzito Mkuu,,
Tena ni shawishi mkuu,,
Zigo linacheza cheza kama paka yupo kwenye kiroba,,,anakwenda kutupwa..
 
ndo mchango wako huo?
Mkuu unataka tukupe mawazo kama tunamjua huyo mtu wako.wewe unaeishi nae ndio unajua tabia yake.
Kuhusu mavazi sioni shida tatizo ni tabia kama anatabia ya hovyo hata avae gunia atafanya ushenzi wake tu.
Hapa uwezi pata jibu amna anajua tabia ya huyo mtu wako zaiidi ya wewe mwenyewe.
Unachotaka wewe tu jugde kitabu kwa kukiona cover kiuhalisia hutapata majibu yatakayo suluhisha hilo tatizo lako.
Kama huyapendi kaanae chini ongea nae.
 
Mimi pia silipendi vazi hilo ninalitafsiri kama vazi lauswahilini sana, yote hiyo nikwasababu wanaolivaa hilo vazi kwasana niwanawake wauswahilini. Ila kama akiwa nayo mawili matatu sio mbaya ila sio ndio liwe vazi lake lamara kwamara
 
Mkuu unataka tukupe mawazo kama tunamjua huyo mtu wako.wewe unaeishi nae ndio unajua tabia yake.
Kuhusu mavazi sioni shida tatizo ni tabia kama anatabia ya hovyo hata avae gunia atafanya ushenzi wake tu.
Hapa uwezi pata jibu amna anajua tabia ya huyo mtu wako zaiidi ya wewe mwenyewe.
Unachotaka wewe tu jugde kitabu kwa kukiona cover kiuhalisia hutapata majibu yatakayo suluhisha hilo tatizo lako.
Kama huyapendi kaanae chini ongea nae.
sawa mkuu, nimekuelewa. ilikuwa nataka kupata angalau kapicha ka tafsiri katika mazingira hayo kutoka upande mwingine. leo hii ukimkuta kijana wa kiume amevaa heleni sote tuna tafsiri yetu, uhuni, usharobaro n.k.
 
Aye, una level ambayo ukiifikia unajua kua saa hii uko broke na unahitaji msaada wa kijeshi? Mi nina level 3. Ya kwanza hua naanza kua na matamanio ya kubet, kuokota hela au simu. Nikivuka level hii naingia level ya 2 hapa hua naanza kupunguza idadi ya mlo kwa siku ya 3 hua nanunua panadol kopo zima najifungia tu ndani kila nikihisi njaa nameza viwili.

Msaada wa kijeshi usiponifikia ndani ya wiki mbili nitaingia level ya tatu.
 
Mtu wangu anapenda sana vazi la dera; akitoka ni dera tu na mara chache ni sketi au gauni.....anasema kanga au kitenge haviwezi kuvaa kwa maana hajavizoea na huwa vinampa shida sana anapovaa safarini ikiwemo kutomshika vizuri hali inayopelekea kutaka kumvuka hivyo kumkosesha utulivu.

Katika hisia zangu, ndani kabisa huko kwenye akili, silipendi vazi hili kwani mi huwa naona ni kama vazi fulani la kihuni hivi........wanaosasambua huko uswahilini nawaona wakipendelea sana madera; mashangingi nawaona wakipendelea sana madera (kama sikosei); n.k.

Maoni yenu wadau, maana isije ikawa ni 'ushamba' unanisumbua na hatimaye ukaniharibia mahusiano siku moja
mimi kwangu naona dera ukishalivaa kuna kitu hakipo sawa akilini mwako, mimi sitaki mke au mdada wa karibu yangu alivae...lina uswahili flani hv..hata ukitoka nae heshima yake na yako haviwezi zingatiwa kihivyoo
 
Back
Top Bottom