Wadau wa JF tujuane kwa kazi zetu, na dharau zitapungua

holoholo

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2023
Posts
1,859
Reaction score
2,986
Wakuu

Humu kumekuwepo na dharau za hapa na pale humu jukwaani.unakuta mtu anakushambulia,anakutukana kwamba mnalingana umri, cheo, au mali.

Unakuta mtu anadharaulika mtaani kwake lakini jukwaani anajiona mtemi,anafoka na kuwadharau wengine

Leo nataka tukate mzizi wa fitna, tujuane kwa umri na vyeo vyetu,heshima itarejea na ustaarabu utarejea jukwaani

Mimi ni mmachinga wa kuuza maji,karanga,soda na vitu vidogovidogo vya wasafiri katika stand X na mkoa X (utani)

Karibuni
 
Mimi ni mbeba mikoba ya uganga, katika kamati ya ufundi ya timu mmoja wapo iliyopo kariakoo!

Hatuna Raha, tumekula hela ya uganga, mechi imeharishwa! Wenyewe wanataka hela yao.

Tunafikiria kutoa tamko Leo!
 
Sina kazi Mimi ni maskini wa kutupwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…