Wadau waulizia alipo Mwana CCM Thadei Ole Mushi

Wadau waulizia alipo Mwana CCM Thadei Ole Mushi

Ex Mayor Jacob na MMM wameandika katika mtandao wa X (formerly Twitter).
huyu ni kada kindakinda wa CCM!
Wanawalaumu wana CCM kuhusika na hilo.

NI TETESI MAANA HAKUNA NEWS FROM CONFIRMED SOURCE

Kupitia ukurasa wa X, Boniface Jacob ameandika haya

-
CCM KWANINI MNATAKA KUMUUA THADEI OLE MUSHI......!

Screenshots_2023-10-14-20-06-11.png


Nimepokea kwa masikitiko na mshangao mkubwa sana taarifa ya shambulio la ghafla linaloaminiwa kuwa la "SUMU" dhidi ya mwana CCM machachari na mkosoaji wa Serikali ya CCM ndugu yetu Thadei Ole Mushi

Baada ya kupata taarifa za siri kuhusu kulishwa/kunyweshwa au kushambuliwa kwa sumu ndugu Thadei Ole Mushi

Mimi Boniface Jacob nimefanya jitihada za kumtafuta Thadei Ole Mushi na kuchunguza ukweli wa taarifa hizo

Nimejiridhisha kwamba Thadei Ole Mushi yuko katika hali mbaya inayoonekana siyo ya kawaida kwake

Yupo mkoani Dodoma (sehemu ni siri) akiwa na mke wake ambaye nimepatiwa namba yake na mtoa taarifa wangu.

Kinacho nisikitisha ni ndugu Thadei Ole Mushi kukosa msaada wa kuletwa hospitali kubwa kama Muhimbili jijini Dar es Salaam

Wakati nikiwa nimejiridhisha kuwa Thadei Ole Mushi hayupo katika hali ya kawaida, ndugu na watu wale wa karibu wa Thadei Ole Mushi wanaonekana kujitahidi kumficha na kuficha taarifa za ugonjwa wa Thadei Ole Mushi na wakati mwingine kuogopa kutoa taarifa za nini kimemkuta ndugu yetu.

Thadei Ole Mushi ni mwana CCM kindakindaki na mkosoaji mkubwa wa chama chake na serikali yake ya CCM, lakini haiondoi ukweli kuwa Thadei Ole Mushi ni mtu muhimu kwa CCM na siasa za Tanzania kama mchambuzi wa siasa nilifikiri CCM na Serikali yake ilitakiwa kutoa umuhimu mkubwa kwa Afya ya Thadei Ole Mushi hata kama hawakubaliani naye baadhi ya misimamo na mawazo yake.

Nikifikiri Jinsi Thadei Ole Mushi alivyokaribu na baadhi ya viongozi wa CCM na Serikali kama katibu Mkuu wa CCM Bw. Daniel Chongolo, wabunge kama akina Charles Kimei, wakuu wa Mikoa kama Anthony Mtaka, Mawaziri na manaibu kama Ridhiwani Kikwete bado nashangaa kwanini Thadei Ole Mushi atelekezwe wakati muhimu kama huu wa kupigania Afya yake.

Kwa namna ambavyo marafiki zake wa CCM na viongozi Serikali wanavyo muacha Thadei Ole Mushi kwa kumuacha apambane na hali yake ni dhahiri huenda wabaya wa Thadei Ole Mushi wapo CCM au kutoka ndani ya serikali ya CCM

Ni wakati sahihi sasa familia ya Thadei Ole Mushi itoke hadharani ituambie nini kimemkuta ndugu yetu katika siasa na mtanzania mwenzetu haraka na mapema tuweze kushiriki kunusuru uhai wake kabla hatujaijumuisha familia yake kama sehemu ya watu wabaya wa Thadei Ole Mushi.

Sisi Watanzania tupo tayari kumpambania na kumuokoa ndugu yetu Thadei Ole Mushi

Mtoeni mlipomficha, mpelekeni hospitali na kama gharama za matibabu ni kubwa tujulishwe tuweze kuchangia haraka sana.

Boniface Jacob
 
Nimeona X-Mayor wa Ubungo Bwana Jacob akiripoti kwamba OLe MUSHI anaumwa na inasadikiwa amepewa sumu. Inaelezwa kuugua kwake ni siri na yupo Sehemu ya siri; wanadai wanasiasa wenzake wamemtenga na hakuna juhudi za kumfikisha hospital.

Nitoe rai kwa wanaohusika au familia watoke adharani kusema na jamii kuondoa uzushi huu unaolenga kubomoa taswira njema ya serikali ya kuwalinda wakosoaji wake. Serikali imejipambanua wazi kwamba haitishwi na wakosoaji hivyo ni vigumu wakosoaji wakapata madhara kiafya kisa wamesema vibaya chama au serikali.

Lakini pia nitoe wito kwa wanachama wa CCM kujiamini na kutosubiri maelekezo yakumsaidia binadamu anapopatwa na matatizo. Wenzenu CHadema wamewezaje kuwa wasemaji wema kwa wana CCM wanapougua au kupata majanga? Kwanini CHadema wawe wakwanza kutoa taarifa za msaada kwa mwana CCM?

Nape alipopata msaada marafiki wote wakamkimbia wakabaki wana harakati na CHadema kumsemea, same applies to mzee Kinana na hata akina polepole. Ninyi wahanga wanufaika wa siasa mnakosaje kujifunza kwa wenzenu?

Siasa zinapofika mahali zikakunyima uhuru wa kwenda msibani ,hospital au kwa mwanadamu mwenzako anayepitia kadhia flan basi hizo fikra za siasa zimekutenga na roho wa Mungu.

Kama ni kweli Ole MUSHI unaumwa tukutakie afya njema . Usisite kujitokeza kuomba msaada maana watu wema bado wapo na wanasubiri wito wako.
 
Tanzania ni nchi ngumu sana duniani.
Kwa nje watu wanatabasamu lakini moyoni wamenuna..


Wameja uuaji
Wamejaa chuki
Wana gumu na visirani.

Muogope sana Mtanzania anayekuchekea ni hatari kuliko Simba na dubu
 
Huyu na Malisa j wanaweka roho zao rehani na wanaocheza nao wana roho mbaya.

Ila kama ni ukweli basi ni unyama sana hii dunia ni ya kupita tu..
 
Nimeona X-Mayor wa Ubungo Bwana Jacob akiripoti kwamba OLe MUSHI anaumwa na inasadikiwa amepewa sumu. Inaelezwa kuugua kwake ni siri na yupo Sehemu ya siri; wanadai wanasiasa wenzake wamemtenga na hakuna juhudi za kumfikisha hospital.

Nitoe rai kwa wanaohusika au familia watoke adharani kusema na jamii kuondoa uzushi huu unaolenga kubomoa taswira njema ya serikali ya kuwalinda wakosoaji wake. Serikali imejipambanua wazi kwamba haitishwi na wakosoaji hivyo ni vigumu wakosoaji wakapata madhara kiafya kisa wamesema vibaya chama au serikali.

Lakini pia nitoe wito kwa wanachama wa CCM kujiamini na kutosubiri maelekezo yakumsaidia binadamu anapopatwa na matatizo. Wenzenu CHadema wamewezaje kuwa wasemaji wema kwa wana CCM wanapougua au kupata majanga? Kwanini CHadema wawe wakwanza kutoa taarifa za msaada kwa mwana CCM?

Nape alipopata msaada marafiki wote wakamkimbia wakabaki wana harakati na CHadema kumsemea, same applies to mzee Kinana na hata akina polepole. Ninyi wahanga wanufaika wa siasa mnakosaje kujifunza kwa wenzenu?

Siasa zinapofika mahali zikakunyima uhuru wa kwenda msibani ,hospital au kwa mwanadamu mwenzako anayepitia kadhia flan basi hizo fikra za siasa zimekutenga na roho wa Mungu.

Kama ni kweli Ole MUSHI unaumwa tukutakie afya njema . Usisite kujitokeza kuomba msaada maana watu wema bado wapo na wanasubiri wito wako.
Wanaccm hawaachiani maji ya kunywa mezani - Kikwete
 
Back
Top Bottom