Wadogo zangu, kabla TV hazijaja enzi hizo mgeni alikuwa anapewa album atazame picha za zamani. Yaani umpe Mtanzania album asichomoe picha hata moja?

Wadogo zangu, kabla TV hazijaja enzi hizo mgeni alikuwa anapewa album atazame picha za zamani. Yaani umpe Mtanzania album asichomoe picha hata moja?

Ila hata siku hizi zipo albums but zipo vizuri zaidi,ni picha zinapigwa halafu inakuwa kama kitabu iliyochapishwa
Yes upo sahihi mkuu, lakini wengi wanahifadhi kwenye hizo virtual drives kama Google, Facebook na Instagram.
 
My only regret sijawahi kupiga picha kwa star wa moro,mudi mpiga picha,picha zangu za utoto baba zangu wadogo wameiba zote
 
Ila hata siku hizi zipo albums but zipo vizuri zaidi,ni picha zinapigwa halafu inakuwa kama kitabu iliyochapishwa ,ikishachapishwa huwezi kuweka picha zingine hadi kitabu kingine
Albums za zamani zilikuwa ni rahisi sana kwa mgeni kuchomoa picha na kuondoka nayo
 
Watoto wa siku hizi hawajui that struggle ya kumpata mpiga picha

Aisee hadi leo nna album yangu ya picha za utotoni nimeihifadhi kwa kumbukumbu
Josee sikujua kabisa kuwa na wewe ni muhenga!

Mkuu Infantry Soldier ametukumbusha mbali sana lakini kuna kitu cha kujifunza katika huu uzi. Tusiweke kumbukumbu zetu kwenye soft copy tu,tukumbuke na kuweka kwa hard copy muhimu sana.
 
Josee sikujua kabisa kuwa na wewe ni muhenga!

Mkuu Infantry Soldier ametukumbusha mbali sana lakini kuna kitu cha kujifunza katika huu uzi. Tusiweke kumbukumbu zetu kwenye soft copy tu,tukumbuke na kuweka kwa hard copy muhimu sana.
Aaah jamaa uzi wake kanikumbusha mbali mno
 
Nimemiss nega za picha
Nimemiss kombolela na kidali poo.
Kujipikilisha michanga
Kuiba mchele kwa mpemba
Kujipikilisha kwenye vikopo vile vya bati (vya tomato sauce)

Ukipiga picha leo waipata baada ya siku 5 hadi week😂😂😂

Maisha ya zamani yalikuwa ya Raha sana
Daaah wee acha tu rafiki yangu. Unapiga picha huku umeweka dole na nguo nzuri za sikukuu
 
Woow..hii safi sana,niyakumbukayo;
1. Ndala za "Skyway"
2.Raba za "DH"
3.Suruali za "Tokyo & Beauct"
4.Mafuta ya kujipaka "Rays"
5.Tanbond sio blue band
6.Soda ya double cola na fahari.
7.Negro arushaa aliitwa " Masawee"
8.Peugeot 403 & 404[emoji3]
Zamani sana hii mkuu
 
"Picha zenu zote zimeungua", alisikika mpiga picha mmoja akituletea habari mbaya...

Hahaha, kumbuka hapo ulistruggle kishenz kufanya maandalizi ya picha, ikiwemo kununua viwalo vipya
 
Na hata baada ya kumpata, kulikuwa na strughle nyingine ya kusubiri picha zisafishwe, maana ni lazima mkanda wa 'negativu' ujae...
Walitusumbua sana enzi hizo, nilikuwa nikichukua Negative ile na kuiangalia kwenye jua nacheka sana
 
Bibi yangu amehifadhi picha zake zote na za watoto plus wajukuuu...
Since anasoma machame Girls ,,Then ashira ... Kupokea kipaimara...
Picha za wanae wote miaka ya 60 ...70 wakiwa wanapokea kipaimara na Vikaptula vyeupe 😅😅😅😂😂😂,
Picha za babu ... Akiwa school,Akiwa anatoa darasa kuhusu kilimo Cha kahawa sehemu mbali mbali Kilimanjaro,Bukoba...

Kiukweli ilikuwa kipindi fulani hv Cha kuvutia.
She's 89 now...
 
Ukiachana na haya ya album, hivi hawa watoto waliozaliwa juzi juzi wanajua kwamba hawa tunaowaita Wapiga debe jina lilitokana na kitu flani cha pembe nne kinachioitwa debe? Waliwahi kuliona debe? Siku hizi yapo wapi madebe wahenga?

Zamani mafuta ya kupikia walikuwa wanaweka kwenye madebe ila sasa kwenye madumu ya plastic.

Debe tupu lilikuwa linauzwa Tsh 100 ila sasa Dumu linauzwa 1500 hadi 2000.
 
Back
Top Bottom