Wadudu wa Arusha ni uchafu wa kijamii, sio sifa njema kwa Arusha. Ududu upigwe vita!

Wadudu wa Arusha ni uchafu wa kijamii, sio sifa njema kwa Arusha. Ududu upigwe vita!

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Kuna kundi la vijana mchanganyiko wa Arusha ambao hawana kazi rasmi, wengi miongoni mwao wakijihusisha na ulevi uliopindukia, uvutaji wa bangi, matumizi ya unga, uporaji, ukabaji, ubakaji na uharifu mwingine mdogo mdogo wa mtaani huku wajitengenezea swaga, mikwara na miondoko fulani yakuweza kutrend mitandaoni, wakiitwa na kujiita wadudu. Ni rahisi kuwajua kutokana na mavazi ya ajabu ajabu, lugha ya ajabu ajabu na kutembea kiajabu ajabu.

Hili sio kundi jema kimaadili kwa jamii iliyostaarabika hususani katika jiji lenye mtazamo wa kimataifa na kitalii zaidi hapa Tanzania, yaani jiji la Arusha.

Ni kiwango cha juu sana cha ujinga na upumbavu kwa taifa kutafuta sifa za kujivunia kupitia wadudu wa Arusha. Watanzania hatuwezi kujivunia tabia za wadudu.

Ule ni uchafu wa kijamii na kimaadili. Arusha haihitaji 'wadudu' ili kuvuma. Arusha inahitaji sana usafi, usalama, ustaarabu, utaratibu, usomi, uungwana, uchapakazi na uwajibikaji.

Tukatae na kupinga kabisa harakati zozote za kuukuza na kuuvumisha huo mtindo wa harakati za wadudu katika jiji la Arusha.

Hivi tulishawaza haya;
1. Mtoto wako au ndugu yako awe ni sehemu ya hao wadudu.
2. Umuone dada yako au binti yako akiwa ana trend na wadudu wa Arusha.
3. Umeone shemeji yako naye ni miongoni mwa wadudu.
4. Hivi waandaji wa mikutano ya kimataifa au watalii wanaweza kutamani kuja Arusha ikiwa jiji litakuwa limetakapaa magenge ya wadudu.

Jamani, hivi tunawajua vizuri wale wadudu?
Yaani kama taifa tunaamua kuhalalisha magenge ya uhalifu, halafu tunategemea usalama utakuwepo?

#KATAAwadudu
#FUTAwadudu
#ARUSHAsafi
 
Ukitaka tuvae kanzu na makobazi ndio vipimo vya usataarabu kwenu?
Wapi nimesema hayo?
Tamaduni za kanzu, misuli na makobazi ziko maeneo ya Pwani na hazijawa tatizo kwa watu.
Sasa yale mauchafu ya wadudu yana maana gani?
Kwanini basi wasivae hata kimasai ili tuwaelewe kuliko kuvaa yale matakataka ya kijinga kabisa.

#KATAAwadudu
#FUTAwadudu
#ARUSHAsafi
 
Kuna kundi la vijana mchanganyiko wa Arusha ambao hawana kazi rasmi, wengi miongoni mwao wakijihusisha na ulevi uliopindukia, uvutaji wa bangi, matumizi ya unga, uporaji, ukabaji, ubakaji na uharifu mwingine mdogo mdogo wa mtaani huku wajitengenezea swaga, mikwara na miondoko fulani yakuweza kutrend mitandaoni, wakiitwa na kujiita wadudu. Ni rahisi kuwajua kutokana na mavazi ya ajabu ajabu, lugha ya ajabu ajabu na kutembea kiajabu ajabu.

Hili sio kundi jema kimaadili kwa jamii iliyostaarabika hususani katika jiji lenye mtazamo wa kimataifa na kitalii zaidi hapa Tanzania, yaani jiji la Arusha.

Ni kiwango cha juu sana cha ujinga na upumbavu kwa taifa kutafuta sifa za kujivunia kupitia wadudu wa Arusha. Watanzania hatuwezi kujivunia tabia za wadudu.

Ule ni uchafu wa kijamii na kimaadili. Arusha haihitaji 'wadudu' ili kuvuma. Arusha inahitaji sana usafi, usalama, ustaarabu, utaratibu, usomi, uungwana, uchapakazi na uwajibikaji.

Tukatae na kupinga kabisa harakati zozote za kuukuza na kuuvumisha huo mtindo wa harakati za wadudu katika jiji la Arusha.

Hivi tulishawaza haya;
1. Mtoto wako au ndugu yako awe ni sehemu ya hao wadudu.
2. Umuone dada yako au binti yako akiwa ana trend na wadudu wa Arusha.
3. Umeone shemeji yako naye ni miongoni mwa wadudu.
4. Hivi waandaji wa mikutano ya kimataifa au watalii wanaweza kutamani kuja Arusha ikiwa jiji litakuwa limetakapaa magenge ya wadudu.

Jamani, hivi tunawajua vizuri wale wadudu?
Yaani kama taifa tunaamua kuhalalisha magenge ya uhalifu, halafu tunategemea usalama utakuwepo?

#KATAAwadudu
#FUTAwadudu
#ARUSHAsafi
Makonda ndio kapandikiza wengi zaidi
 
• Mi naona tuaze kuwakata makalio mashoga Kwanza... 🤒🤒

• Hao wadudu hawana shida yeyote ile
Arusha haijawahi kujivunia mashoga bali kwa sasa inajivunia wadudu!
Ni upumbavu mkubwa watu wenye akili timamu na upeo kama Arusha kujivunia wale vijana wa ovyo ovyo wanaoitwa wadudu.

#KATAAwadudu
#FUTAwadudu
#ARUSHAsafi
 
Arusha haijawahi kujivunia mashoga bali kwa sasa inajivunia wadudu!
Ni upumbavu mkubwa watu wenye akili timamu na upeo kama Arusha kujivunia wale vijana wa ovyo ovyo wanaoitwa wadudu.

#KATAAwadudu
#FUTAwadudu
#ARUSHAsafi
Kitu nilicho ona Hapa Jmt, tumejikita zaidi kwenye unafiki kuliko uhalisia..

Ndo maana tumekuwa tukitilia mkazo kwenye vitu vya kipuuzi, alafu mambo ya maana tunayaacha yanaangamia.
 
Kipimo cha uwezo wa kiumbe-binadamu kufikiria kwa umakini na tija huakisi anachoshangilia.
NB;Kuunga mkono uoambaff nayo ni in-born character.
 
Wapi nimesema hayo?
Tamaduni za kanzu, misuli na makobazi ziko maeneo ya Pwani na hazijawa tatizo kwa watu.
Sasa yale mauchafu ya wadudu yana maana gani?
Kwanini basi wasivae hata kimasai ili tuwaelewe kuliko kuvaa yale matakataka ya kijinga kabisa.

#KATAAwadudu
#FUTAwadudu
#ARUSHAsafi
Kwani kuvaa raba na shati kubwa ni uchafu??
Hao hao pia wanaona kanzu ni uchafu
 
Hapo ishu ni moja tuu kama huwezi control wapendwa wako kwenye mitandao basi piga marufuku wasitumie kabisa coz you can't decide for people on what to post on those sosho medias.

Halafu yaani wewe Arusha umeona ujinga wa wadudu tuu? Mbona Kuna upuuzi mwingi sana Arusha
 
Kwani kuvaa raba na shati kubwa ni uchafu??
Hao hao pia wanaona kanzu ni uchafu
Kutetea vitu vya kijinga ni ujinga maradufu. Wewe unaona ule uvaaji wa wadudu unakufurahisha?
Ungetamani ndugu yako, rafiki yako, mtoto wako, shemeji yako avae vile halafu mtembee wote barabarani?
 
Hapo ishu ni moja tuu kama huwezi control wapendwa wako kwenye mitandao basi piga marufuku wasitumie kabisa coz you can't decide for people on what to post on those sosho medias.

Halafu yaani wewe Arusha umeona ujinga wa wadudu tuu? Mbona Kuna upuuzi mwingi sana Arusha
Hapa nimezungumzia wadudu tu kwa kuwa kwa sasa ndio wanaotrend mitandaoni, na watu wasioijua au kuwahi kufika Arusha wanadhani Arusha ni mji wa wadudu tu kwa kuwa baadhi ya wakazi wa Arusha wanajivunia hao wadudu.
Sasa embu jiulize, hivi kwa jiji la kisomi, kijanja, kimataifa na kitalii kama Arusha, kuna faida ya kujivunia ududu?
 
Arusha ndio kwenu acha kutumia neno zanzibar , hiko ndio kizazi cha kwenu.
 
Back
Top Bottom