Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 11,550
- 40,697
Kuna kundi la vijana mchanganyiko wa Arusha ambao hawana kazi rasmi, wengi miongoni mwao wakijihusisha na ulevi uliopindukia, uvutaji wa bangi, matumizi ya unga, uporaji, ukabaji, ubakaji na uharifu mwingine mdogo mdogo wa mtaani huku wajitengenezea swaga, mikwara na miondoko fulani yakuweza kutrend mitandaoni, wakiitwa na kujiita wadudu. Ni rahisi kuwajua kutokana na mavazi ya ajabu ajabu, lugha ya ajabu ajabu na kutembea kiajabu ajabu.
Hili sio kundi jema kimaadili kwa jamii iliyostaarabika hususani katika jiji lenye mtazamo wa kimataifa na kitalii zaidi hapa Tanzania, yaani jiji la Arusha.
Ni kiwango cha juu sana cha ujinga na upumbavu kwa taifa kutafuta sifa za kujivunia kupitia wadudu wa Arusha. Watanzania hatuwezi kujivunia tabia za wadudu.
Ule ni uchafu wa kijamii na kimaadili. Arusha haihitaji 'wadudu' ili kuvuma. Arusha inahitaji sana usafi, usalama, ustaarabu, utaratibu, usomi, uungwana, uchapakazi na uwajibikaji.
Tukatae na kupinga kabisa harakati zozote za kuukuza na kuuvumisha huo mtindo wa harakati za wadudu katika jiji la Arusha.
Hivi tulishawaza haya;
1. Mtoto wako au ndugu yako awe ni sehemu ya hao wadudu.
2. Umuone dada yako au binti yako akiwa ana trend na wadudu wa Arusha.
3. Umeone shemeji yako naye ni miongoni mwa wadudu.
4. Hivi waandaji wa mikutano ya kimataifa au watalii wanaweza kutamani kuja Arusha ikiwa jiji litakuwa limetakapaa magenge ya wadudu.
Jamani, hivi tunawajua vizuri wale wadudu?
Yaani kama taifa tunaamua kuhalalisha magenge ya uhalifu, halafu tunategemea usalama utakuwepo?
#KATAAwadudu
#FUTAwadudu
#ARUSHAsafi
Hili sio kundi jema kimaadili kwa jamii iliyostaarabika hususani katika jiji lenye mtazamo wa kimataifa na kitalii zaidi hapa Tanzania, yaani jiji la Arusha.
Ni kiwango cha juu sana cha ujinga na upumbavu kwa taifa kutafuta sifa za kujivunia kupitia wadudu wa Arusha. Watanzania hatuwezi kujivunia tabia za wadudu.
Ule ni uchafu wa kijamii na kimaadili. Arusha haihitaji 'wadudu' ili kuvuma. Arusha inahitaji sana usafi, usalama, ustaarabu, utaratibu, usomi, uungwana, uchapakazi na uwajibikaji.
Tukatae na kupinga kabisa harakati zozote za kuukuza na kuuvumisha huo mtindo wa harakati za wadudu katika jiji la Arusha.
Hivi tulishawaza haya;
1. Mtoto wako au ndugu yako awe ni sehemu ya hao wadudu.
2. Umuone dada yako au binti yako akiwa ana trend na wadudu wa Arusha.
3. Umeone shemeji yako naye ni miongoni mwa wadudu.
4. Hivi waandaji wa mikutano ya kimataifa au watalii wanaweza kutamani kuja Arusha ikiwa jiji litakuwa limetakapaa magenge ya wadudu.
Jamani, hivi tunawajua vizuri wale wadudu?
Yaani kama taifa tunaamua kuhalalisha magenge ya uhalifu, halafu tunategemea usalama utakuwepo?
#KATAAwadudu
#FUTAwadudu
#ARUSHAsafi