Wadukuzi wadai fidia ya Tsh Bilioni 162 ili kufungulia mifumo waliyofungia

Wadukuzi wadai fidia ya Tsh Bilioni 162 ili kufungulia mifumo waliyofungia

Sam Gidori

Senior Member
Joined
Sep 7, 2020
Posts
165
Reaction score
417
Wadukuzi wanaodhaniwa kuhusika na shambulio la kimtandao wamedai malipo ya dola milioni 70 (sawa na Tsh. bilioni 162 na milioni 330) ili kufungulia mifumo waliyodukua.

Madai yao yaliwekwa wazi siku ya Jumapili katika mtandao wa kihalifu unaohusishwa na genge la wahalifu wa kimtandao la Urusi linalojulikana kama REvil. Wadukuzi hao walifanikiwa kuingilia mifumo ya mamia ya makampuni duniani.

Shirika la Habari la Reuters limeripoti kuwa wadukuzi hao wamepunguza dau kufikia dola milioni 50 (sawa na Tsh. bilioni 115 na milioni 950 ) baada ya kufanya mazungumzo na wataalamu wa masuala ya usalama wa mtandao.

Wataalamu hao wanasema wadukuzi hao wanaweza kuwa katika wakati mgumu kifedha kutokana na wahanga wao kutokuwa tayari kulipa fedha ili kukomboa taarifa zao, baada ya wadukuzi kuonekana kuwa tayari kuzungumza kupunguza dau. Wengine wanasema kuwa wadukuzi hao wamekusanya kiasi kikubwa cha taarifa kutoka kwa wahanga wao kiasi cha kushindwa kuhimili wingi huo wa taarifa.

Mifumo ya kielektroniki ya makampuni mbalimbali ya kibiashara, zikiwamo shule 11 nchini New Zealand na mamia ya maduka ya jumla nchini Uswidi yameathirika na shambulio hilo. Takriban nchi zingine 12 zimeathiriwa na shambulio hilo.

Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) limesema genge hilo lilihusika na shambulio lingine la kimtandao mwezi Mei lililofanikiwa kufunga mtandao wa kampuni kubwa zaidi ya uchakataji nyama duniani, JSB.

Rais wa Marekani, Joe Biden amesema Marekani itaiwajibisha Urusi ikiwa itathibitika kuwa imehusika na shambulio hilo.

Chanzo: VOA
 
Tatizo la wadukuzi wa mifumo linaendelea kukua kwa kasi duniani. Sasa hivi targets sio tu mabenki na taasisi za kifedha bali taasisi na mashirika yote yenye taarifa za wateja wao.

Mwaka 2016 shambulio la WannaCry lilipiga makampuni mengi makubwa duniani mpaka mengine kulazimika kulipa fedha nyingi kwa wahalifu (hackers) ili kukomboa taarifa zao na mifumo yao.

Teknolojia ya mawasiliano inakuwa kwa kasi ila changamoto kubwa kwa sasa ni usalama wa taarifa za kidigitali.

Ransomware ndio tishio kwa watumiaji wengi wa mitandao na TEHAMA kiujumla.

Serikali ya Tanzania ni muda sasa umefika ianze kuwekeza kwenye wataalamu wa usalama wa mifumo la sivyo tutalia kilio cha mbwa koko. Tutalipa mabilioni kila siku kwa wahalifu.
 
[emoji23][emoji23],kumbe hata waumini wake mnautolea mate mkwanja wa askofu wenu[emoji23][emoji23]
Huo mkwanja wa bishop ni michango yetu , shida bishop ni mbahili sana hapendi kusambaza kwa wahitaji kama wajane na wasiojiweza, sasa dawa yake ni kumdukua ili agawe pesa kinguvu nguvu [emoji38][emoji38]
 
Tatizo la wadukuzi wa mifumo linaendelea kukua kwa kasi duniani. Sasa hivi targets sio tu mabenki na taasisi za kifedha bali taasisi na mashirika yote yenye taarifa za wateja wao.

Mwaka 2016 shambulio la WannaCry lilipiga makampuni mengi makubwa duniani mpaka mengine kulazimika kulipa fedha nyingi kwa wahalifu (hackers) ili kukomboa taarifa zao na mifumo yao.

Teknolojia ya mawasiliano inakuwa kwa kasi ila changamoto kubwa kwa sasa ni usalama wa taarifa za kidigitali.

Ransomware ndio tishio kwa watumiaji wengi wa mitandao na TEHAMA kiujumla.

Serikali ya Tanzania ni muda sasa umefika ianze kuwekeza kwenye wataalamu wa usalama wa mifumo la sivyo tutalia kilio cha mbwa koko. Tutalipa mabilioni kila siku kwa wahalifu.
Lazima Gepg, Hazina zilale hata siku 2 kwenye zile Tarehe zinazoanzia na 2
 
Back
Top Bottom