Wafadhili wa nini? - Hayati Rais John Pombe Magufuli

Wafadhili wa nini? - Hayati Rais John Pombe Magufuli

Wafadhili wa nini wakati tuna kila kitu Almasi,Dhahabu,ardhi yenye rutuba,sisi ndio wafadhili,naomba niwaambie ukweli,tulikuwa na shida kwa viongozi wetu.
View attachment 3165673
Ukiachilia mbali hayo yote, lakini bado wafadhili aliwatumia.... Shida ikaja akawa pesa imekopwa na bado anasema tunajenga kwa pesa zetu. Sijui kwanini alikuwa hataki kusema ukweli.
 
Mwamba huyu hapa, ni jembe sana,alijenga 1.hospitals za kutosha
2. Barabaran za kutosha na fry over
3.Nidhamu makazini.
4.Ndege
5.Makao makuu Dodoma
6.Kutoa wenye vyeti feki
7.kuthibiti mafisadi
8.Kukataa mikataba ya hovyo eg Bandari.
9.Elimu Bure.
10.Alikuza utalii na kiswahili na mengine ongezea
workdone = zero, yote yamerudi vile vile, mengine na kuzidi..makosa alifanya yeye mwenyewe! bora hata asingepata nafasi ya kuongoza..sababu tumerudi nyuma kuzidi pale alianzia!
 
Mwamba huyu hapa, ni jembe sana,alijenga 1.hospitals za kutosha
2. Barabaran za kutosha na fry over
3.Nidhamu makazini.
4.Ndege
5.Makao makuu Dodoma
6.Kutoa wenye vyeti feki
7.kuthibiti mafisadi
8.Kukataa mikataba ya hovyo eg Bandari.
9.Elimu Bure.
10.Alikuza utalii na kiswahili na mengine ongezea
"Fry over" nimeishia hapo
 
Jiwe, rais wa hovyo :-
1. Aliyeamini ktk maendeleo ya vitu na siyo watu.
2. Muasisi wa utekaji, uporaji na mauaji ya watu.
3. Aliamini kuwa mtu akiwa rais hapaswi kuiosolewa. Jinga kabisa.
4. Dikteta aliyekosa chembe ya huruma.
5. Aliminya haki za makundi yote kuanzia wakulima, wafanyakazi, wavuvi, n.k.

Kifo chake kilileta faraja na furaha kwa watu wengi.
Waambie ukweli Hawa mapimbi hawaelewi kitu chochote kabisa!
 
  • Thanks
Reactions: G4N
Kenge huyo amerasimisha utekaji, uuaji, kupita chaguzi bila kupingwa, Rais wa hovyo kuwai kutokea duniani.
Wewe huwezi kuwa Mr liverpool. Liverpool hatuna washabiki wenye mawazo ya ovyo ovyo namna hiyo. Badilisha hilo jina ujiite Mr ManU
 
Jiwe, rais wa hovyo :-
1. Aliyeamini ktk maendeleo ya vitu na siyo watu.
2. Muasisi wa utekaji, uporaji na mauaji ya watu.
3. Aliamini kuwa mtu akiwa rais hapaswi kuiosolewa. Jinga kabisa.
4. Dikteta aliyekosa chembe ya huruma.
5. Aliminya haki za makundi yote kuanzia wakulima, wafanyakazi, wavuvi, n.k.

Kifo chake kilileta faraja na furaha kwa watu wengi.
Nagongelea zaidi.
6. Alisababisha jobless wengi kwa wahitimu wa elimu za vyuo nchini
7. Alikopa sana afu anajifanya dona kanry.
8. Alileta ukabila na ukanda katika mambo ya msingi. Akapendelea chato kwao nk
9. Hakustahili kuwa raisi
 
  • Thanks
Reactions: G4N
Ukiachilia mbali hayo yote, lakini bado wafadhili aliwatumia.... Shida ikaja akawa pesa imekopwa na bado anasema tunajenga kwa pesa zetu. Sijui kwanini alikuwa hataki kusema ukweli.
tukirudi kwenye rekodi za Taifa letu kiuchumi hadi kufikia April 2021 deni la Taifa lilikuwa sh 60.9 trilioni,ikilinganishwa na sh 55.5 trilioni kipindi kama hicho mwaka 2020,kati ya kiasi hicho deni la nje lilikuwa ni sh 43.7 trilioni na deni la ndani lilikuwa sh 17.3 trilioni,kufikia June 2023 deni la taifa limefikia sh 82.25 trilioni sawa na ongezeko la asilimia 15 kutoka sh 71.31 trilioni kwa mwaka 2022,deni la ndani lilikuwa sh 28.92 trilioni na deni la nje lilikuwa sh 53.32 trilioni mwaka 2022,kwa miaka mitatu sh trilioni 21.35 zimekopwa toka 2021 hadi 2023,ikilinganishwa na sh 19 trilioni zilizokopwa toka 2016 hadi 2020 na Serikali ya awamu ya tano.
 
Nagongelea zaidi.
6. Alisababisha jobless wengi kwa wahitimu wa elimu za vyuo nchini
7. Alikopa sana afu anajifanya dona kanry.
8. Alileta ukabila na ukanda katika mambo ya msingi. Akapendelea chato kwao nk
9. Hakustahili kuwa raisi
Kwa mujibu wa hotuba ya bajeti ya mwaka 2016,deni la taifa lilikuwa ni shilingi trilioni 40.Kutoka mwaka 2016 hadi 2020 deni la taifa likafikia sh 59 trilioni sawa,kwa miaka mitano ongezeko lilikuwa ni sh 19 trilioni, Tarehe 1 July 2020 IMF ilisema Tanzania joins middle economy status na Magazeti ya kiingereza nchini yakaandika Magufuli sends Tanzania to middle economy status ahead of it's schedule,Hii ni record ambayo inamhitaji someone wiser to break it,kwa rekodi hii Hayati Rais John Pombe Magufuli ataendea kuwa measuring stick kwa vitu mbalimbali kiuchumi na kijamii hadi rekodi yake itakapovunjwa na mtu makini zaidi yake,kwa nini nasema hivyo,muda uliopangwa wa Tanzania kuingia uchumi wa kati ulikuwa ni mwaka 2025 lakini Hayati Rais John Pombe Magufuli aliweza kuipeleka Tanzania kwenye uchumi wa kati miaka mitano nyuma ya muda uliotarajiwa na benki ya dunia.
 
tukirudi kwenye rekodi za Taifa letu kiuchumi hadi kufikia April 2021 deni la Taifa lilikuwa sh 60.9 trilioni,ikilinganishwa na sh 55.5 trilioni kipindi kama hicho mwaka 2020,kati ya kiasi hicho deni la nje lilikuwa ni sh 43.7 trilioni na deni la ndani lilikuwa sh 17.3 trilioni,kufikia June 2023 deni la taifa limefikia sh 82.25 trilioni sawa na ongezeko la asilimia 15 kutoka sh 71.31 trilioni kwa mwaka 2022,deni la ndani lilikuwa sh 28.92 trilioni na deni la nje lilikuwa sh 53.32 trilioni mwaka 2022,kwa miaka mitatu sh trilioni 21.35 zimekopwa toka 2021 hadi 2023,ikilinganishwa na sh 19 trilioni zilizokopwa toka 2016 hadi 2020 na Serikali ya awamu ya tano.
La msingi tunakubaliana kuwa tulikopa. Hilo ndilo la msingi... usiishie hapo hebu tueleze na kiasi gani kilikopwa kuanzia 2005-2015 awamu ya nne ili point yako ieleweke vizuri.
 
Kifo chako kitaleta faraja na furaha kwa watu wengi.
Mpaka leo,kuna watu wanakasirika au wanashangaa anapozungumzwa Hayati Rais John Pombe Magufuli,? Watu awa wanashindwa kuelewa kwamba Hayati Rais John Pombe Magufuli bado hajaandikiwa biographies za maana za kuchambua maisha yake,If anything Tanzania hatujamuongelea vya kutosha Hayati Rais John Pombe Magufuli,hatujamuongelea kwa kina kuchambua mazuri na mabaya yake,kila mtu ana mapungufu,Rais wa awamu ya kwanza,Hayati Baba wa Taifa,Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alikuwa na mapungufu yake kama mwanadamu,vivyo hivyo kwa Rais wa awamu ya pili,awamu ya tatu na awamu ya nne,turekebishe penye mapungufu na mazuri yao tuyaenzi na kuyaendeleza,tuwape maua yao kwa kila zuri walilofanya kwa Watanzania,
 
Wanahadithia ya kwamba aliufikisha uchumi wa China hadi "kati-chini" hadi Bashing'waa/Chinese waligaragara mavumbini kuonesha kumpa ukuu uliotukuka na kusema masihi amekuja.😎
kama kweli haumpendi Hayati Rais John Magufuli,presumably na CCM,mimi ningetegemea ufurahie wana CCM kumuongelea Hayati John Magufuli ambaye amefariki (kwa sababu ndiye aliyeirudisha CCM kwenye ramani toka kuzomewa ukivaa sare za CCM hadi kusifiwa ukivaa sare za CCM sababu Hayati Rais Magufuli alitenda sawa sawa na Wananchi walivyotaka,lakini kingine kama watu walikuwa wanamuogopa basi hawezi kugombea kwenye uchaguzi) na wao waitumie fursa hiyo kumnadi mgombea wao,sasa, badala ya wao kumnadi mgombea wao,na wao wanajiunga kumuanzishia uzi Hayati Magufuli.Sasa unajiuliza mtu anaponda watu kumuongelea Hayati Rais John Magufuli,badala ya yeye atuambie habari za mgombea wake,anaishia kutukana na kuchukua uchafu wao kumrushia Hayati Rais Magufuli!!?
 
kama kweli haumpendi Hayati Rais John Magufuli,presumably na CCM,mimi ningetegemea ufurahie wana CCM kumuongelea Hayati John Magufuli ambaye amefariki (kwa sababu ndiye aliyeirudisha CCM kwenye ramani toka kuzomewa ukivaa sare za CCM hadi kusifiwa ukivaa sare za CCM sababu Hayati Rais Magufuli alitenda sawa sawa na Wananchi walivyotaka,lakini kingine kama watu walikuwa wanamuogopa basi hawezi kugombea kwenye uchaguzi) na wao waitumie fursa hiyo kumnadi mgombea wao,sasa, badala ya wao kumnadi mgombea wao,na wao wanajiunga kumuanzishia uzi Hayati Magufuli.Sasa unajiuliza mtu anaponda watu kumuongelea Hayati Rais John Magufuli,badala ya yeye atuambie habari za mgombea wake,anaishia kutukana na kuchukua uchafu wao kumrushia Hayati Rais Magufuli!!?
Umelalamika kwa sentensi moja ndefu sana bila kupumzika?Haujazimia?
 
Kuna watu wengi kama Mbowe,Zitto,Lissu,Mnyika,Kinana, Mama na machawa wake wanamsema sana Hayati Rais John Pombe Magufuli kwa kuharibu nchi,ebu tuone hayo wanayosema kayaharibu Hayati Rais John Pombe Magufuli,RIP.

Jpm kaharibu kujenga mradi wa umeme mkubwa,Bwawa la Rufiji (Bwawa la Mwalimu Nyerere) unaozidi uwezo wa umeme wote unaozalishwa tangu mkoloni,Nyerere,Mwinyi,Mkapa na Kikwete na Sasa hakuna tena mgao wa Umeme,tutapata Umeme na kusaza,tutasahau habari ya iptl,dowans,Richmond na Escrow!.

Jpm kaharibu kujenga Reli ya Umeme,Reli ya kisasa yenye uwezo mkubwa wa kwenda kwa haraka na kubeba mzigo mkubwa kuliko Reli zote nchini,Treni ambayo itatumia saa moja na nusu toka Dar hadi Morogoro,na Massa matano tu toka Dar hadi Mwanza,hii itafanya kuharakisha Maendeleo,badala ya kusafiri Masaa 17 toka Dar hadi Mwanza.

Jpm kaharibu kujenga maghala ya kutunzia vyakula kwa mikoa yote inayozalisha vyakula kwa hifadhi za taifa letu,Sasa Taifa litakuwa na hifadhi ya kutosha ya Mazao ya Chakula.!.

Jpm kaharibu kwa kufufua shirika la ndege la atcl na ununuzi wa ndege zake kumi na moja kwa ajili ya kukuza na kuboresha sekta ya Utalii,hivi sasa tunashuhudia Watalii zaidi ya 1,000 wakitua nchini.

Jpm kaharibu kwa kutoa ruzuku ya kielimu ( elimu bure) kwa shule za misingi na sekondari,hivi sasa hakuna mtoto asiyejua kusoma wala kuandika.!.

Jpm kaharibu kwa kujenga hospitali kwa wilaya zote ambazo hazikuwa na hospitali za wilaya na vituo vya Afya zaidi ya 300 nchini baada ya kuvikuta vituo 67 tu!

Jpm kaharibu kwa kumalizia miradi iliyoanzishwa na watangulizi wake ambayo ilikwama kuendelea baada ya pesa kupigwa ama ujenzi usioridhisha kama barabara,Madaraja,Viwanja vya ndege vya zamani na Vipya,Kujenga barabara za juu na zile za kukatisha bahari ya hindi na kule ziwa Victoria na vivuko mbalimbali.

Jpm kaharibu kwa kuendelea kujenga miundombinu ya bandari na ujenzi wa meli mpya kwa maziwa ya Nyasa,Victoria na Tanganyika!.

JPM kaharibu kwa kuijenga Ikulu ya Dodoma ambayo ilishindikana kujengwa kwa miaka 50.Jpm yeye kaijenga na kahamisha makao makuu ya nchi toka Dar es Salaam hadi Dodoma,kuna watu wameumia sana wanasema kaharibu,!!?

Haya ndio ambayo kaharibu JPM,sasa kwa akili ya kawaida watu wanaomsema wana akili timamu!?
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Kwa mujibu wa hotuba ya bajeti ya mwaka 2016,deni la taifa lilikuwa ni shilingi trilioni 40.Kutoka mwaka 2016 hadi 2020 deni la taifa likafikia sh 59 trilioni sawa,kwa miaka mitano ongezeko lilikuwa ni sh 19 trilioni, Tarehe 1 July 2020 IMF ilisema Tanzania joins middle economy status na Magazeti ya kiingereza nchini yakaandika Magufuli sends Tanzania to middle economy status ahead of it's schedule,Hii ni record ambayo inamhitaji someone wiser to break it,kwa rekodi hii Hayati Rais John Pombe Magufuli ataendea kuwa measuring stick kwa vitu mbalimbali kiuchumi na kijamii hadi rekodi yake itakapovunjwa na mtu makini zaidi yake,kwa nini nasema hivyo,muda uliopangwa wa Tanzania kuingia uchumi wa kati ulikuwa ni mwaka 2025 lakini Hayati Rais John Pombe Magufuli aliweza kuipeleka Tanzania kwenye uchumi wa kati miaka mitano nyuma ya muda uliotarajiwa na benki ya dunia.
Baada ya hapo ikawaje tena..? 😁😁😁😁 na wewe uliamini alitufikisha uchumu yeye ..? Uchumi wa kati ulifikishwa kwa mipango ya mkapa na JK kuifanyia kazi. Ila sifa anapewa mwamba 😁😁😁
 
Kwa hiyo unaunga mkono hoja yake. Adui mkubwa wa nchi hii ni CCM. Mambo yote yanayotendeka ni madhira ya CCM. Umasikini, kunyima democrasia, mauaji yanayoendelea,elimu duni na mengine mengi mabaya yanayofanyika hapa Tanzania hasa Tanganyika ni kwa sababu ya CCM.
Je Dkt Steven Ulimboka alitekwa awamu ya Magufuli?

Je unaweza kuwa na Maendeleo ya watu bila kuwa na Maendeleo ya
 
Inawezekana na pengine ndio maana hakuweza kuendelea ngwe ya pili..kosa lake ni kupandwa kichwani na wajinga wachache aliowakuta hapo ikulu wakafaulu kumjengea chuki na vyama vya upinzani, wahisani, baadhi ya watu nje ya ccm, viongozi wa nchi jirani, baadhi ya viongozi wa dini na wengine..alikosea sana kukubali uongo huo! yeye ndiye aliondoka wao bado wapo, na wanafanya yale yale..lakini dhamira yake ilikuwa njema kabisa kuwainua watanzania KUJITEGEMEA..!
Hapana. Hayo yote yalikuwa ni yake mwenyewe. Na aliamini ktk mawazo yake pekee. Yeye alijiona kuwa anajua na anweza kila kitu peke yake. Hakuwaamini hata Wataalam kwenye nyanja mbalimbali. Mfano akitoa tamko kuwa daraja lijengwe ndani ya siku 14 na lianze kutumika. Akitokea Mkandarasi akampa ukweli kuwa siku 14 ndiyo kwanza mchoro na vipimo utakuwa umekamilika. Utasikia wewe Mkandarasi ulisoma Chuo gani kwanzia leo sitaki nikuone hapa Tanroad. Mkuu wa Majeshi uko hapa? Kazi hii nakukabidhi wewe. Anapigiwa saluti anajiona mshindi. Alijiona yeye ni msomi kuliko hata Maprofesa waliomfundisha.

Kwa kifupi ni kwamba alikuwa siyo Kiongozi bali ni Mtawala tena katili. Yeyote aliyejaribu kuyarekebisha au kuyapinga matamko yake alimuona ni adui yake mkubwa na adhabu yake ni kutumbuliwa au kupotezwa kabisa.
 
Back
Top Bottom