Nawawekea hawa wazungu wachache walio pigania kupiga ban biashara ya utumwa [emoji117]
View attachment 990956View attachment 990959View attachment 990960 ...naomba jina la maarabu mmojà aliye pigania kupiga ban utumwa [emoji53]
Sent using
Jamii Forums mobile app
Wahispania waliona fursa ya kuwageuza imani wapagani ndani ya biashara hiyo, na (madhehebu ya Kikristo ya) “the Jesuits”, “Dominicans” na “Franciscans” walijihusisha mno na kilimo cha miwa, ambacho kilisababisha umilikaji wa watumwa muhimu. Hadithi imesimuliwa kuhusu mzee wa Kanisa huko Newport ambaye kila wakati, Jumapili iliyofuata baada ya kuwasili watumwa kutoka pwani, alikuwa anamshukuru Mungu kwamba mzigo mwingine wa viumbe washenzi uliletwa mahali ambapo wangeweza kupata manufaa ya neno la Injili.’
Lakini kwa ujumla wakulima wa Kiingereza walipinga Ukristo (kufundishwa) kwa watumwa wao. Ukristo uliwafanya watumwa kuwa wapotovu zaidi, kutokuwa watiifu na kwa hiyo wanakuwa hawana thamani. Pia ilikuwa na maana pia kutoa maelekezo kwa lugha ya Kiingereza, jambo ambalo liliruhusu makabila mbali mbali kukutana pamoja na kupanga njama za uasi… Gavana wa Barbados mnamo mwaka wa 1695 alilihusisha hilo na wakulima kukataa kuwapa watumwa mapumziko siku ya Jumapili na sikukuu, na mwishoni mwa 1832 maoni ya umma wa Uingereza (Britsh public opinion) yalishtushwa na wakulima walipokataa pendekezo la kuwapa Watu Weusi siku moja ya kupumzika ili kuruhusu kukomesha soko la Jumapili la Watu Weusi.
Kanisa lilitii. “Society for the Propagation of the Gospel” (chama cha kuitangaza Injili) kilikataza mafundisho ya Kikristo kwa watumwa wake huko Barbados, na kuwapiga chapa ya ‘Society’ (chama) watumwa wake wapya kuwatofautisha na wale waliomilikiwa na watu wa kawaida; watumwa wa mwanzo walikuwa urithi wa Christoper Codrington. Sherlock, baadaye akawa Bishop wa London, aliwahakikishia wakulima kwamba ‘Ukristo na kuikumbali Injili hakuleti hata cheme ya tofauti kuhusu mali za raia.’ Wala haukuwekwa vikwazo katika shughuli za kikanisa. Kwa kazi zake kuhusu Asiento ambazo zilisaidia kumfanya kama muwakilishi (Balozi) mwenye mamlaka kamili wa Uingereza huko Utrecht, Bishop Robinson wa Bristol alipandishwa cheo na kuwa Askofu wa dayosisi ya London.
Kengele za makanisa ya Bristol zililia kushangilia kuhusu taarifa ya kukataliwa na Bunge muswada wa Wilberforce uliotaka kukomeshwa kwa biashara ya watumwa. Mfanyabiashara wa biashara ya watumwa, John Newton, aliyashukuru makanisa ya Liverpool kwa ushindi wa jaribio hili la mwisho kabla hajabadilika na akaomba baraka za Mungu zimjie yeye. Alianzisha ibada ya hadhara mara mbili kwa siku kwa uchu wake, akihubiri yeye mwenyewe, na alitenga siku moja ya kufunga saumu na kusali, si kwa ajili ya watumwa bali kwa ajili ya wafanyakazi wa meli. ‘Sikujua,’ aliungama, ‘utamu au saa zaidi za sakramenti takatifu ziwe mara nyingi zaidi kuliko kwenye safari mbili za baharini za kwenda Guinea.’
Kadinali Manning maarufu wa karne ya kumi na tisa alikuwa mtoto wa mfanya biashara tajiri wa visiwa vya West Indies aliye kuwa anashughulika na bidhaa zilizo limwa na watumwa.Wamisionari wengi waliona ni faida kubwa kumfukuza Beelzebub kwa Beelzebub (yaani, kumfukuza shetani kwa kumtumia shetani). Kwa mujibu wa mwandishi wa siku hizi za karibuni sana wa Uingereza kuhusu biashara ya watumwa, walifikiri kwamba njia nzuri zaidi ya kurekebisha matumizi mabaya ya watumwa Weusi ilikuwa kumfanya mwenye shamba kuwa mfano mzuri kwa kuwatunza watumwa na mashamba wao weneywe, ili kutimiza katika utekelezaji wa aina hii ukombozi wa wamiliki wa mashamba na kuendeleza misingi yao.’
Wamisionari wa Kanisa la Moravian kisiwani hapo walimiliki watumwa bila kusita; Wamissionari wa Kanisa la, mwandishi mmoja wa historia anaandika kwa mtiririko wa mvuto kwamba Baptists (yaani, Wakristo wa madhehebu ya Baptst) hawakuruhusu wami- sionari wao wa mwanzo kupinga kumiliki watumwa. Hadi mwisho kabisa, Askofu wa Exeter aliendelea kuwa na watumwa wake 655, na mnamo mwaka wa 1833 alilipwa pauni za Kiingereza 12,700 kama fidia ya watumwa hao.
Wataalam wa historia wa Kanisa waliomba msamaha wa kufedhehesha, kwamba dhamiri ilizinduka polepole sana kutathmini uovu ulioletwa na utumwa na kwamba utetezi wa utumwa uliofanywa na watu wa kanisa ‘ulitokana na utashi wa uzuri wa utambuzi wa maadili.’ Hakuna haja ya kuomba msamaha wa aina hii. Msimamo wa watu wa kanisa ulikuwa ndio msimamo wa mtu wa kawaida. Karne ya kumi na nane kama nyingine yoyote, haingeweza kuvuka mipaka ya uchumi wake. Kama alivyo hoji Whitefield alipokuwa anatetea kusomwa tena kila kipengele cha mkataba wa Georgia uliositisha utumwa, ‘Ni rahisi kuonyesha kwamba nchi za joto haziwezi kulimwa bila Watu Weusi.’
Quaker (kundi la Wakirsto ambalo halipendelei mikutano rasmi na halipendelei ghasia au vita) - wasiofuata kanuni, hawakukubali kuacha biashsra ya watumwa. Mwaka wa 1756 walikuwepo Quaker themanini na nne waliorodhesh- wa kama wanachama wa kampuni ifanyayo biashara kwenda Afrika, miongoni mwao ni “the Barclay”: na “Baring families.” Shughuli ya watumwa ilikuwa moja wapo ya uwekezaji wenye faida kubwa wa Quaker wa Uingereza halikadhalika na wale wa Marekani na jina la mfanya biashara ya watumwa, The Willing Quaker, aliarifu kutoka Boston – Siera Leone mwaka wa 1793, inaashiria uthibitisho ambao ulisababisha biashara ya watumwa kuheshimiwa katika jamii ya Quaker.
Jamii ya Quaker ilifanya upinzani dhidi ya biashara ya watumwa kwanza kutoka Marekani na kutoka kwenye vijiji vya jamii ndogo vya kaskazini, ambavyo havikujihusisha na nguvu kazi ya watumwa. ‘Ni vigumu’, anaandika Dk. Gray, ‘kukwepa dhana kwamba upinzani huo dhidi ya mpango wa watumwa kwanza uliwekewa mipaka kwa kundi ambalo halikupata manufaa ya moja kwa moja kutoka kwenye biashara hiyo, kwa hiyo walikuwa wapinzani.’
Utumwa ulikuwepo wakati wa Mwingereza wa karne ya kumi na nane. Na sarafu ya Kiingereza, guinea, ingawaje ilipatikana kwa nadra, chanzo chake ilikuwa biashara ya Africa. Mhunzi wa dhahabu wa Westminster alitengeneza kufuli kwa ajili ya Watu Weusi na mbwa. Sanamu za watu weusi na tembo, ishara ya biashara ya watumwa zilipamba ukumbi wa Liverpool Town Hall. Alama za cheo na vifaa vya wafanya biashara ya watumwa vilionyeshwa wazi ili vinunuliwe kwenye maduka na kutangazwa kwenye magazeti.