Wafanyabiashara Halali wa Mbagala wanawezaje kulipa kodi ikiwa Wamezibwa 100% na Wamachinga?

Wafanyabiashara Halali wa Mbagala wanawezaje kulipa kodi ikiwa Wamezibwa 100% na Wamachinga?

I have been there once, I spent 15 mins kichwa kiliuma aiseee vile vispika Sasa Kila mtu anacho kinapiga kelele, mama lishe wanamisufuria imejaa mapilau wanauza barabarani uani ni tafrani in short wapaite Mbagala Republic
 
Usichojua wale MACHINGA wengi wao pale wanachukua mzigo kutoka kwenye maduka makubwa hapohapo ndiyo wanaenda kuuza kwa makubaliano kifupi zile biashara ni zawenye maduka makubwa palepale wale MACHINGA ni wauzaji tu wakiuza pesa wanapeleka kwa wenye maduka wao wanapewa chochote kitu
 
Halafu wenye maduka ya Nafaka wana utaratibu wa kishebzi na wizi. Iko hivi Unapo nunua mchele mfano kilo moja ni sh 2000 na umenunua kilo 10, badala ya kulipa sh 20,000 tu utadaiwa sh 20200. Hiyo sh 200 inayozidi ni service charge ( gharama ya kuhudumiwa). Hiyo Ndiyo Mbagala Republic.
 
Nimepita Mbagala wiki hii nikielekea kwenye Shamba langu Mkuranga, Hakika Mbagala ni Nchi nyingine kabisa, Utaratibu wao wa kuishi ni tofauti kabisa na Utaratibu wa Tanzania.

Wamachinga wamepanga bidhaa kuanzia kwenye milango ya maduka ya watu hadi katikati ya Barabara bila wasiwasi wowote, Wala hawaogopi hata milango ya Benki! yaani ni kama Mbagala haina serikali yoyote ile na ni kama hakuna mgambo wala polisi, Kumbukeni hawa Wamachinga hawalipi kodi yoyote ile, Ugali wa Mama Lishe unasongewa barabarani na magari yanasubiri msongaji amalize ndio yapite, Hili kwangu ni jambo la Ajabu mno!

Marafiki zangu wa kihindi wanaofanya biashara eneo hilo nilipowahoji kuhusu hali hiyo wamenieleza kwamba wanatishwa kulogwa ikiwa watafanya kampeni yoyote ya kuwazuia walioziba Milango yao!

Taarifa za chini chini zinaeleza kwamba Meya wa Eneo hilo, ambaye anatajwa kutisha kwa Ushirikina ndiye mlinzi wa Kwanza wa mambo hayo, anaunga mkono kila uchafu wa Wamachinga bla kujali athari zake, Kimsingi Wafanyabiashara wa Mbagala wanachosubiri ni kudura za Mungu, Hali yao ni mbaya kuliko nilichoandika.
tatizo sio hao wamachinga tatizo ni serikali yetu haijui kutumia rasilimali watu. Baadae nitafafanua vizuri
 
Usichojua wale MACHINGA wengi wao pale wanachukua mzigo kutoka kwenye maduka makubwa hapohapo ndiyo wanaenda kuuza kwa makubaliano kifupi zile biashara ni zawenye maduka makubwa palepale wale MACHINGA ni wauzaji tu wakiuza pesa wanapeleka kwa wenye maduka wao wanapewa chochote kitu
umeandika baadhi ya yale niliyotaka kusema. Na hiyo ndio njia wanayotumia hao wenye maduka makubwa kukwepa kodi maana wanasingizia wamachinga wakati wamachinga ndo wateja na wauzaji wa biashara zao
 
Sijawah kusifia uongozi wa samia isipokuwa katika suala la wamachinga japo lilikuwa na mapungufu lakin afadhali alivowaondoa barabaran japo kuna baadhi ya maeneo kama kariakoo wameshindikana kuondoka
 
umeandika baadhi ya yale niliyotaka kusema. Na hiyo ndio njia wanayotumia hao wenye maduka makubwa kukwepa kodi maana wanasingizia wamachinga wakati wamachinga ndo wateja na wauzaji wa biashara zao
Hii hoja haina Mashiko, unawezaje kuwapa mali yako ya thamani watu usiowajua?
 
Kiukweli watanzania wengi tunalalamika viongozi hawafuati sheria ila sisi pia ni wavunjifu wakubwa. Hao machinga wakiondolewa kwa nguvu watalalamika kwa kutumia kisingizio cha unyonge na umaskini. Pia watapata watetezi wengi wakiwemo baadhi ya wapinzani. Serikali ifanye maamuzi magumu.
Sasa hivi serikali haiwezi kufanya lolote! Mwaka huu na mwaka kesho ni kura mkuu!
 
Nimepita Mbagala wiki hii nikielekea kwenye Shamba langu Mkuranga, Hakika Mbagala ni Nchi nyingine kabisa, Utaratibu wao wa kuishi ni tofauti kabisa na Utaratibu wa Tanzania.

Wamachinga wamepanga bidhaa kuanzia kwenye milango ya maduka ya watu hadi katikati ya Barabara bila wasiwasi wowote, Wala hawaogopi hata milango ya Benki! yaani ni kama Mbagala haina serikali yoyote ile na ni kama hakuna mgambo wala polisi, Kumbukeni hawa Wamachinga hawalipi kodi yoyote ile, Ugali wa Mama Lishe unasongewa barabarani na magari yanasubiri msongaji amalize ndio yapite, Hili kwangu ni jambo la Ajabu mno!

Marafiki zangu wa kihindi wanaofanya biashara eneo hilo nilipowahoji kuhusu hali hiyo wamenieleza kwamba wanatishwa kulogwa ikiwa watafanya kampeni yoyote ya kuwazuia walioziba Milango yao!

Taarifa za chini chini zinaeleza kwamba Meya wa Eneo hilo, ambaye anatajwa kutisha kwa Ushirikina ndiye mlinzi wa Kwanza wa mambo hayo, anaunga mkono kila uchafu wa Wamachinga bla kujali athari zake, Kimsingi Wafanyabiashara wa Mbagala wanachosubiri ni kudura za Mungu, Hali yao ni mbaya kuliko nilichoandika.
Mbagala ipi hiyo yenye maduka ya wahindi? Barabara ya kuelekea wapi hiyo inayozibwa na mama ntilienwasonga ugali?
Meya yupi huyo mwenye mamlaka ya kuzuia vyombo vya Dola kutekeleza Sheria za nchi?

Fika kariakoo uone machiga wa pale ndio urudintena
 
Mbagala ipi hiyo yenye maduka ya wahindi? Barabara ya kuelekea wapi hiyo inayozibwa na mama ntilienwasonga ugali?
Meya yupi huyo mwenye mamlaka ya kuzuia vyombo vya Dola kutekeleza Sheria za nchi?

Fika kariakoo uone machiga wa pale ndio urudintena
Mada ya leo ni Mbagala, kariakoo tutakuja.

Kingine ulichokisahau ni hiki, Vyombo vya Dola vya Tanzania havijawahi kufanya kazi bila kutumwa na ccm
 
Mkuu wa mkoa washirikiane na meya kuhakikisha watu wote tunalipa kodi,si TRA kutupigia simu sisi tu Tena kila baada ya miez3.
Bado leseni,ada ya taka,ulinzi.daah
Waeke mazingira mazuri ya kibiashara kwa wote
 
Back
Top Bottom