DOKEZO Wafanyabiashara Kariakoo kugoma Mei 15, 2023

DOKEZO Wafanyabiashara Kariakoo kugoma Mei 15, 2023

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Wapi hapo tuwafate hao wasaliti?
Mtaa wapouza pikipiki kuna Mhindi kafungua duka lake, yuko karibu na Cate hotel

Mtaa huo huo maduka mengi ya dawa za kisuna yamefunguliwa.


Mtaa wa Lindi kuna duka limefunguliwa

Maeneo ya jangwani pamefunguliwa
 
Mpaka Abdul mtoto wa rais nae hajafungua duka
Umoja ni kitu kizuri sana, bora watu wakubali hasara hata ya siku 3 ila ujumbe uwe umewafikia.

Kodi hazieleweki

Matajiri ndo wanapaswa kukomaa na hili maana wao ndo huumizwa na kodi
 
Kuna tetesi ya mgomo wa wafanyabiashara eneo la Kariakoo.

View attachment 2622388

Sababu za kuitisha mgomo;
1. Urasimu bandarini
2. Usajili wa stoo
3. Kamata kamata hovyo ya wateja kwa ukuguzi wa risiti

Wao wapo tayari kufanya biashara kwa uhuru na kulipa kodi bila mambo ya rushwa rushwa na maonezi.

View attachment 2622389
Rai kwa mamlaka zinazohusika kuchukua hatua za haraka hili jambo lisitokee. Pale ni kitovu cha biashara ukanda huu. Makosa kidogo tunaweza hamisha hii biashara kwa jirani zetu.

kama vile namwona Omolo Odinga katia mguu bongo
 
Ieleweke, huu ni mgomo na wala sio maandamano, yani tumekuja Kariakoo lakini maduka yetu hatufungui kwahyo leo TRA hesabu zao za siku zitakuwa chini ya kiwango
 
sasa bro, wewe na we si mtanzania? hebu tuonyeshe shamba la ngano au la mahindi unalolima? sisi wananchi tunatakiwa kuchukua hatua kufanya kilimo biashara, sidhani kama serikali haijaweka mazingira rafiki ya kilimo. ukisafiri kwa basi unakutana na mapori kila sehemu yapo tu, hakuna watu wa kulima ila tunalaumu serikali kwamba inafanya watu waagize chakula nje? hizo akili au matope? wewe umefanya nini walau ili kutuhakikishia kuwa ukishika nchi utakuwa na pa kuanzia.
Acha kujitoa akili Ndg.....inamana huoni huu ukiritimba unaoendelea kila sekta....?!

Hayo unayoyasema.....unaweza kuyafanya kwa urahisi huooo...?!
 
Ukichunguza pande zote mbili, TRA na wafanyabiashara, wana hoja kwenye madai yao.

Itumike busara na hekima badala ya nguvu na makali ya Sheria (ambazo nyingine si za haki).

Swali: Kwa nini watu/wafanyabiashara wanakwepa au hawapendi kulipa kodi?

Jibu: Kodi ni nyingi na viwango ni vikubwa.

Solutions:

1. Serikali na TRA (kwa upande mmoja) watunge na kuweka viwango rafiki vya kodi.

•Je Kwanini VAT iwe 18% na sio 10 au 12%?
•Kwa nini corporate tax zisiwe 15%?
•Kwa nini withholding tax zisiwe 2-5%?

Kwa ufupi tu, mwishoni mwa miaka ya sitini(late 1960s) nchi za Africa, baada ya 'uhuru' zilijikuta kwenye matatizo - namna gani kukuza uchumi wao na kuongeza mapato. Nchi nyingi zikachagua njia "rahisi" na "fupi" toka kwa Wajamaa - Kodi nyingi na kubwa.

Botswana wao wakachagua njia iliyoonekana "ngumu" na "ndefu" - viwango vidogo/chini vya kodi pamoja na mazingira rafiki ya kufanya biashara.

Kufikia miaka ya themanini wale waliochagua njia 'fupi na rahisi' walikuwa HOI.
Botswana wao walikuwa wanaelekea kwa kasi uchumi wa kati kwa ile njia 'ngumu na ndefu'.

Na bado tumekuwa wazito sana wa kujifunza na kusahihisha makosa yetu; na mahali pengine hatukubali kubadilika kutokana na mahitaji na mazingira ya nyakati zetu.

2. Lazima tuifundishe jamii yetu umuhimu wa kulipa kodi na kupenda kulipa kodi. Utamaduni huo hufundishwa shuleni na majumbani tangu - toka watoto wakiwa wadogo upward.

3. Uwajibikaji na matumizi bora ya hela na mali za umma.

Hata kama tukukisanya trilioni 100 kwa mwaka, kama tabia na "Utamaduni " wa ubadhirifu, wizi, ufisadi, rushwa na matumizi mabovu na ya anasa utaeendelea kama ilivyo sasa - itakuwa ni sawa na kujaza maji kwenye gunia la sukari tu.

Tujenge mutual win-win environments.

Mkitaka, Inawezekana.
 
Ukichunguza pande zote mbili, TRA na wafanyabiashara, wana hoja kwenye madai yao.

Itumike busara na hekima badala ya nguvu na makali ya Sheria (ambazo nyingine si za haki).

Swali: Kwa nini watu/wafanyabiashara wanakwepa au hawapendi kulipa kodi?

Jibu: Kodi ni nyingi na viwango ni vikubwa.

Solutions:

1. Serikali na TRA (kwa upande mmoja) watunge na kuweka viwango rafiki vya kodi.

•Je Kwanini VAT iwe 18% na sio 10 au 12%?
•Kwa nini corporate tax zisiwe 15%?
•Kwa nini withholding tax zisiwe 2-5%?

Kwa ufupi tu, mwishoni mwa miaka ya sitini(late 1960s) nchi za Africa, baada ya 'uhuru' zilijikuta kwenye matatizo - namna gani kukuza uchumi wao na kuongeza mapato. Nchi nyingi zikachagua njia "rahisi" na "fupi" toka kwa Wajamaa - Kodi nyingi na kubwa.

Botswana wao wakachagua njia iliyoonekana "ngumu" na "ndefu" - viwango vidogo/chini vya kodi pamoja na mazingira rafiki ya kufanya biashara.

Kufikia miaka ya themanini wale waliochagua njia 'fupi na rahisi' walikuwa HOI.
Botswana wao walikuwa wanaelekea kwa kasi uchumi wa kati kwa ile njia 'ngumu na ndefu'.

Na bado tumekuwa wazito sana wa kujifunza na kusahihisha makosa yetu; na mahali pengine hatukubali kubadilika kutokana na mahitaji na mazingira ya nyakati zetu.

2. Lazima tuifundishe jamii yetu umuhimu wa kulipa kodi na kupenda kulipa kodi. Utamaduni huo hufundishwa shuleni na majumbani tangu - toka watoto wakiwa wadogo upward.

3. Uwajibikaji na matumizi bora ya hela na mali za umma.

Hata kama tukukisanya trilioni 100 kwa mwaka, kama tabia na "Utamaduni " wa ubadhirifu, wizi, ufisadi, rushwa na matumizi mabovu na ya anasa utaeendelea kama ilivyo sasa - itakuwa ni sawa na kujaza maji kwenye gunia la sukari tu.

Tujenge mutual win-win environments.

Mkitaka, Inawezekana.

Mkuu umeeleza vema sana. Wapunguze viwango vya kodi na idadi zake. Lakini zaidi kuelimisha umuhimu wa kulipa kodi. Serikali pia ijitathimini katika matumizi sahihi, sio kama haya tunayo yaona na kusoma katika ripoti ya CAG.
 
Back
Top Bottom