Wafanyabiashara Stendi ya Magufuli wataka mabasi yote yashushe na kupakia abiria hapo stendi ili wapate wateja

Mipango miji kapangeni kwanza Tandale, Buza, Vingunguti na Mbagala, acheni ujinga went wa kusumbua abiria. Huwezi kupeleka vituo vya mabasi porini eti useme ndio unapanga mji.
Stendi ya bus ilitakiwa iwepo hata hapo Kariakoo kabisa mtu akichukua mzigo wake anatupia kwenye gari na kusepa.
 
Kwani lazima upande Abood kwenda Moro au ni masharti ya mganga wako??
 
Usitumie matako kufikiria...hakuna aliyesema kuwa abiria wa njiani asishushwe kabla ya basi kufika Magufuli bus terminal....kinachogusiwa hapa ni magari kugoma kupakia abiria hapo Magufuli
Kama lineshajaa tayari linakotokea aje Magufuli kupakia majini au?

Tiketi Sasa hivi zinakatwa Kwa njia ya mtandao ulioidhinishwa na LATRA kama mtandao Rasmi..ambao wenye mabasi lazima wautumie na uanaonyesha MTU atapandia au kushukia wapi mfano unaonyesha wazi kuwa uchague basi utapandia au kushukia wapi Shekilango au Maguful NK
Sio wenye mabasi ndio waliojiamulia kuweka hip mfumo hivyo ni LATRA

Sasa vyombo viwill vya serikali vinagongana LATRA anasema ruksa kupakia na kushusha mfano Shekilango au Urafiki hao wahuni wengine WA serikalini wanasema stendi mmoja Tu ya Magufuli vyombo viwilo cya serikali moja wanefanya KAZI kama wajinga Fulani hivi.Latra wako sahihi zaidi kuliko hao wajinga wengine mwaliko serikalini na hao wafanyabiashara

Kwa hiyo wanataka mfumo wote WA LATRA ufumuliwe ambao ulikubalika na Pande zote wenye mabasi ,Abiria na LATRA?

Hii nchi kuna upumbavu mwingi Sana Unaipa mlaka LATRA ifanye KAZI inafanya KAZI Yake vizuri anatokea mhuni huko anakuja na kupings KAZI yote kubwa na nzuri iliyofanywa na LATRA nini hicho?

Wafanyabiashara WA mabasi gomeni kabisa .Mpaki mabasi Abiria tunawaunga mkono .Haiwezekani watu wachache watese Abiria ambao wenyewe sio Abiria wala wamiliki WA mabasi
 
Kabisa....
 
Inashangaza sana mkuu walalamikaji ndio wamejigeuza wao center na kipaumbele cha stendi wanajiita "wadau wa stendi"!🤣 Hawajui wadau wa stendi ni Abiria, wasafirishaji na serikali, wao wauza crisps, pipi na karanga ni watu wa ziada tu ambao hata wakiondolewa hakuna hasara yoyote.
 
Sasa kama bus haliwezi kumfuata mteja mbona kuna vituo binafsi? Au ww Umeelewa kuwa bus kumfuata abiria nyumbani kwake?
 
Maamuzi Yake yatakuwa kinyume cha makubakuano Kati ya LATRA na wenye mabasi na Abiria

Ingia mtandao WA LATRA WA kukata Tiketi unaonyesha wazi vituo vipi vya kupandia na kushukia vituo vya Shekilango na Urafiki vimo kwenye mtandao

Akae chonjo muda wowote aweza ishia mahakamani.akienda pupa
 
Kwa nini mikoa mengine kila wilaya ina stendi yake ila Dar unataka iwe na kituo kimoja tu?
Kwa nini Airport wauza karanga, crisps na maji hawaruhusiwi kuuzia wateja bidhaa zao ndani ya ndege au kwenye madirisha ya ndege?
 
Harafu hao wavivu ambacho hawajui ni kuwa msongamano umepungua kwa Kasi hapo magufuli ni kwasababu ya usafiri kuwa wa masala 24 na sio hayo mawazo yao mgando
 
Kwa nini mikoa mengine kila wilaya ina stendi yake ila Dar unataka iwe na kituo kimoja tu?
Tatizo la Dar es salaam kwenye uongozi ni mawili wengi wa viongozi WA Dar kuwepo huwekwa sababu wanapendelewa Wana connection lakini vichwani hamna kitu wenye akili hupelekwa mikoani ndio maana mikoani kunafanya vizuri

Pili viongozi wengine huhamishiwa Dar Kwa sababu za kiafya ili wakae karibu na hospital ya rufaa ya Mloganzila na Muhimbili wanakotakiwa kuwa wanahudhuria matibabu mara Kwa mara Kwa hiyo mkoa unakuta unaongozwa na wagonjwa wazima wako mikoani

Hii combination ya akili finyu na wagonjwa ndio inasababisha hizo chaos tunazoona

Jiji la Dar linahitaji watu wazima na wenye akili hasa
 
Mtu anaishi Ubungo,umekata ticket Kilimanjaro Express ofisi zake zilipo na safari inaanzia hapo.Kwamba abiria asiruhusiwe kupanda basi,liondoke tupu na abiria apande Bajaj au bodaboda wakakutane Magufuli?

Kwamba akitoka zake Marangu na ndizi na maparachichi yake ashushwe kwa lazima,basi liondoke tupu ili apande Tena Bajaj na bodaboda aende Ubungo? Kichaa kibichi hiki!
 
Hata LATRA msimamizi mkuu WA usafiri WA nchi kavu hawatambui

Wanatambuliwa na wahuni Tu WA mjini
 
Harafu hao wavivu ambacho hawajui ni kuwa msongamano umepungua kwa Kasi hapo magufuli ni kwasababu ya usafiri kuwa wa masala 24 na sio hayo mawazo yao mgando
Hao vichwa panzi wakijua na hili utaona wameitisha mkutano mwingine wakitaka gari zote zianze safari kwa pamoja saa kumi na mbili asubuhi, hoja watakazokuja nazo sasa itakuwa vituko vitupu, wanaweza kusema hiyo lodge hapo ghorofani stendi haipati mapato hivyo serikali nayo inapoteza mapato.
 
Tatizo ni ushamba na kufanya mambo kwa sifa bila uhalisia. Darhaihitaji stand moja kubwa, bali inahitaji stand nyingi ndogo ndogo.
Huo ujenzi ulikuwa ni ufisadi tu.
 
Hatufikirii kabisa kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…