Wafanyabiashara Stendi ya Magufuli wataka mabasi yote yashushe na kupakia abiria hapo stendi ili wapate wateja

Wafanyabiashara Stendi ya Magufuli wataka mabasi yote yashushe na kupakia abiria hapo stendi ili wapate wateja

Sidhani kama ni kufanya biashara wanahitaji hao wa Magufuli Terminal tu, hata waliopo shekilango nao wanafanya biashara. Hiyo hoja ni dhaifu sana
Mkuu shekilango sio stendi, zile ni ofisi za wenye mabasi.
 
Mimi na-support mabus kufuata abiria walipo na sio abiria kufuata mabus yalipo.

Mwisho tutasema na SGR iwafuate huko huko tuliko (joke).

Anyway, my point is serikali lazima iwe na vituo maalumu ambapo mabasi yanaanzia. Kwa jinsi Dar ilivyo na magari mengi kuruhusu kila basi lianzie linakotaka ni vurugu mechi. Yanaongeza msongamano. Mabasi yote yaanzie Magufuli kama kituo cha kwanza kikuu lakini yaruhusiwe kusimama njiani huko mbeleni yanakoelekea mbele ya safari kuchua abiria wao.
 
Kieneo cha dar ni kidogo sana. Ni ngumu mtu kutoka ulanga akapandie moro (ulanga to moro ni kama safari ya mkoa hd mkoa ndo maana tunahitaji stendi ulanga). Sasa dar eneo dogo kila sehemu panafikika within 1 hour then unahutaji stend ya nn?

Nahesabu kuanzia center ya wilaya ilipo. Umbali hatuchukulii huko nanjilinji, huwa unachukuliwa kutoka center ya eneo husiki. Ukisikia Dar to mwanza ni km 1200 hawachukui umbali wa bango la umeingia mwanza na bango la umeingia mkoa wa dar.

😀😀
Wewe umevurugwa kweli.
Kwa hiyo hao wa mwakatobe sio Abiria?
 
Miongoni mwa wamiliki wasiotaka kupakia abiria Magufuli Bus terminal ni ABOOD.
Mkuu abood hana stendi Ubungo, ile ni ofisi yake, abiria wa maeneo hayo hupita pale kuhitaji huduma, sasa ache kuwa chukua kisa wanatakiwa waanzie safari Mbezi??? Unaona iko sawa???
 
Pengine hamjui maana ya ofisi ndo maana mnageuza ofisi khiyo paleama sehemu ya stendi. Ofisini kwako ni
Pengine hamjui maana ya ofisi ndo maana mnageuza ofisi kama sehemu ya stendi. Ofisini kwako ni sehemu ya abiria kupata tiketi, kutuma au kupokea mzigo uliotumwa.
Niseme wazi Kuna wakati nikikutana na Afisa wa serikali mjinga kama wewe Huwa najiuliza kwanza alipataje ajira huyu mjinga? Kwa hiyo hatujui maana ya ofisi ? Hivi zile ofisi pale bandarini za meli za kwenda Zanzibar kazi yake kukata tiketi na kupokea mizigo tu? Na pale stendi ya Tazara na ofisi ya TRC pale ofisi zao kazi Yao kukata tiketi na kupokea mizigo na kutuma tu na ofisi za pale Airport kazi Yao kukata tiketi na kutuma na kupokea mizigo tu? Ee Mungu nisamehe nisije nikakuporomoshea matusi ya nguoni mjinga wewe
 
Mwisho tutasema na SGR iwafuate huko huko tuliko (joke).

Anyway, my point is serikali lazima iwe na vituo maalumu ambapo mabasi yanaanzia. Kwa jinsi Dar ilivyo na magari mengi kuruhusu kila basi lianzie linakotaka ni vurugu mechi. Yanaongeza msongamano. Mabasi yote yaanzie Magufuli kama kituo cha kwanza kikuu lakini yaruhusiwe kusimama njiani huko mbeleni yanakoelekea mbele ya safari kuchua abiria wao.
Yes!! Hii ndo watu hawataki kuelewa, mimi mwenyewe nasapoti kupakia yaendako na kushusha vtuo ambavyo viko mwanzo. Magufuli stendi iwe kituo cha mwsho kuwa na abiria ndani ya gari. Hii ya kushushia hadi ofsini hapana labda kuwabeba kipindi inaanza safari ndo iwachukue huko ianziako then iptie wa stendi itembee
 
Wakuu wa wilaya ni sababu ya kuhudumia idadi ya watu na si geographically. Kijiografia dar ni ndogo sana kuiwekea stend 3 ni matumiz mabaya ya pesa za umma.
Angalia tu usije kufikia kusema hata hospitali za wilaya/manisipaa Dar ni matumizi mabaya ya pesa za umma watu wote wanatakiwa walundikane hospitali moja tu. Tutamuambia moderator akupige ban na kukuondoa kabisa humu jukwaani.
 
Nimesima baadhi ya comments hapa halika Watanzania tunatakiwa kuwa na kiongozi mwenye maamuzi magumu hasa, yaani HASA.

Kwanza mtoa mada kagusia wafanyabiashara kama tu sehemu ya stendi ila wale si muhomu sana kwa sasa.

Ila muhimu ni matumizi ya stendi, hapo juzi tu 2000yr stendi zilikuwa tatu, ubungo, mnazi mmoja na kisutu ila Scandinavian Express alikuwa na ofisi yake pale kamata, ubungo ilikuwa stendi kuu na kuna mabasi ya mhindi yakiitwa Royal alikuwa anapakilia upanda, kisutu.

Kuna Taqwa na Tawaqal masafa marefu hawa walikuwa kule ilala, sharif shamba, mnazi mmoja na Magomeni mapipa.

Lakini mabasi yote hayo yalikuwa lazima yapitie kutoka au kuingia ubungo kwa sababi ndiyo ilikuwa Main Bus Terminal kwa jiji la Dar Es Salaam.

Baada ya kuonekana vurugu katikati ya mji ndipo serikali ikasitisha mabasi makubwa yote kuingia katikati ya mji ziishie ubungo na ilikuwa hivyo.

Na hata hii ya Magufuri Bus Terminal ni katika kupanua huduma na msongamano wa kila mtu kuwa na ofisi yake imetokana na kadhia ya vurugu mjini.

Binafsi naona ni jambo jema sana mabasi yote yaanzie pale JPM-BT Mbezi kwa sababu iliyolengwa.

Ukiwa nchini Kenya jijini Nairobi au hata mliofika Afrika ya kusini mnaweza kuelewa ukitaka kusafiri ndipo unaweza kuona umuhimu wa stendi moja ila kwa ambaye hajasafiri anaona ni ujuha.

Kuna watu hapa wanapiga kelele mkoa wa Arusha kukosa stendi, kwa nini kila bus lisipakie eneo lake, yaani watawanyike kila mtaa how come mnataka stendi ya kisasa?.

Sheria zichukue mkondo, mfano pale shekilango hadi manzese ni vurugu tu kwa mabasi makubwa, zile ni nyumba za kuishi watu ila leo mmegeuza ofisi na stendi za mabasi HOW?.
 
Wa bus walishajiongezea ndo maana wana hamu ya kukufikisha unapotaka. Wese hata likishuka bei hutowasikia wakiomba nauli kushushwa. Hapo wanawaondolea kulalamika kuwa nauli za bus ni kubwa kisa wanakufikisha kitaani kwako.
Wenye mabasi Wana roho nzuri viafisa vya serikali baadhi Yao ndivyo vina roho mbaya kama shetani
 
Angalia tu usije kufikia kusema hata hospitali za wilaya/manisipaa Dar ni matumizi mabaya ya pesa za umma watu wote wanatakiwa walundikane hospitali moja tu. Tutamuambia moderator akupige ban na kukuondoa kabisa humu jukwaani.
Naunga mkono hoja
 
Angalia tu usije kufikia kusema hata hospitali za wilaya/manisipaa Dar ni matumizi mabaya ya pesa za umma watu wote wanatakiwa walundikane hospitali moja tu. Tutamuambia moderator akupige ban na kukuondoa kabisa humu jukwaani.
Kwa kosa gani?? Hospitali ni watu wanahitaji huduma ya chapu syo mlundikano wa kusubiri matibabu. Stend ya magufuli imeshindwa kuhimili idadi ya watu mbachelewa kisa stendi ndogo au? Bus zipo ni muda kufika we unatembea tu. Sasa km hospitali ingekuwa na uwezo wa kuhudumia watu milioni 1 kwa pamoja bila kusubiria kuna haja gani kuweka hospitali ya pili wakati ya kwanza tu inawahudumia wote bila shida.
 
Wa mwakatobe wasafiri kufika mjini ndo wasafiri. Tubataka kuua ajira za watu kisa unafuu (boda wa mwakatobe ale wapi kama bus zinakusanya hadi huko).

Ninyi ndio mkiwa viongozi mnatesa wananchi.
Kiongozi bora ni yule anayetoa huduma akirahisisha maisha ya Watu.

Ishu hapo ni kodi na huduma rahisi kura raia full stop.
Kama kuna chochote kimeguswa hapo ndio ipo haja ya kutazama jambo hilo
 
Unahitaji Elimu jinsi mikopo ya nchi inavyolipwa.. pole sana
Tuambie inalipwaje kama siyo kutokana na makusanyo ya kodi kutoka ktk vyanzo mbali mbali ikiwemo ushuru wa stendi?
 
bora iwe kupandia stand aseeee,,ila hii ya kushuka wanatuonea,, imagine umetoka zako hukoooo,umefika mahali husika unaona kabisa kituo chako kinapitilizwa eti hadi stand,,na hapo ni usiku pia gharama za nauli tena.
 
Hiyo nusu saa umeihesabu kutokea wapi?

Mtu atoke Twangoma mpaka Mbezi atatumia hiyo nusu saa?

Mtu atoke Mabwepande mpaka Mbezi atatumia hiyo nusu saa. Vipi chanika?

Hoja zenu hazina mashiko kwa sababu hazingatii ukweli.

Utaratibu uendelee kama ulivyo.

Juzi nilikuwa natoka Bukoba, nimeingia saa 10 usiku. Yaani mizigo kibao alafu nishuke Mbezi wakati Basi Limerahisisha huduma.

Lengo la serikali ni kurahisisha huduma kwa wananchi na serikali kujipatia kipato.

Ungesema mfumo uliopo unaukosesha serikali mapato au kuwapa ugumu wananchi ungekuwa na hoja.
Lakini sivyo
Huyo ni mshamba ambaye hajawahi kufika Dar, hajui ndani ya Dar kuna sehemu na wakati watu wanatumia hadi masaa matatu kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
 
Tuambie inalipwaje kama siyo kutokana na makusanyo ya kodi kutoka ktk vyanzo mbali mbali ikiwemo ushuru wa stendi?
Wenye mabasi wanalipa in advance na abiria Kodi inakatwa Kodi kwenye tiketi mnataka Nini nyie ? Kama sio ugomvi wenye mabasi chenu wamewapa kama ushuru abiria chenu wamewapa kama Kodi inayokatwa kwenye tiketi
 
Hassan Bomboko, Dc wa wilaya ya Ubungo aache kuhangaika na machangudoa wa Riverside na Sinza badala yake ajikite hili suala linalotokea katika kata yake ya Mbezi na ubungo.

Aamke alfajiri akafunge ofisi za haya Mabadi pale urafiki na shekilango ayaamuru yakapakie mbezi, magufuli bus terminal
Mkuu anafungaje ofisi za watu, kwa kosa gani?? una ushahidi kuwa hawapiti Magufuli???
 
Back
Top Bottom