Wafanyabiashara Stendi ya Magufuli wataka mabasi yote yashushe na kupakia abiria hapo stendi ili wapate wateja

Wafanyabiashara Stendi ya Magufuli wataka mabasi yote yashushe na kupakia abiria hapo stendi ili wapate wateja

Na wewe huoni nafuu mbeba mzigo akipata pesa yako?
Kwani mimi ndio niliomleta hapa mjini hadi nimpe huo unafuu wa jasho langu??
Arudi kwao akalime au akafuge kuku.
 
Na wewe huoni nafuu mbeba mzigo akipata pesa yako?
Kwanini nione unafuu kwenye kuongeza gharama? Yaani unauliza kwanini nisione unafuu wa kulipia basi na mizigo 75elfu sababu ya kusafiri kulifata basi badala ya 45elfu kwa basi kuniletea huduma karibu?
 
Siku zote biashara haitakiwi kutegemea Stendi, bali stendi ndio inapaswa kutegemea biashara yako, shida ni hawa wafanyabiashara walidanganywa na ccm

Nimepita hapo stendi zaidi ya mara 50 lakini sikuwahi kununua chochote, hii ni kwa sababu si lazima abiria kununua kitu hapo stendi, sasa wanacholilia ni nini?
Tundu lisuu na mbowe washaaungana tena...na wamekubaliana wale walioko Bungeni 19 wataendelea kuwa wanachama wa Chadema na watagombea Ubunge,vipi wewe washakupatia Kazi ya kufanya au utaendelea kuwapigia wezio uchawa humu?
 
Kwani mimi ndio niliomleta hapa mjini hadi nimpe huo unafuu wa jasho langu??
Arudi kwao akalime au akafuge kuku.
Hahaaa!! Hilo ni lako ila serikali haiwez kuhudumia wananchi wake hivyo. Tunaamn riziki popote hivyo kama yupo mjini acha tumtafutie namna kuliko akawe panya road
 
Tundu lisuu na mbowe washaaungana tena...na wamekubaliana wale walioko Bungeni 19 wataendelea kuwa wanachama wa Chadema na watagombea Ubunge,vipi wewe washakupatia Kazi ya kufanya au utaendelea kuwapigia wezio uchawa humu?
Achilia mbali kwamba hoja yako ni ya kijinga bali pia iko nje ya mada
 
Hahaaa!! Hilo ni lako ila serikali haiwez kuhudumia wananchi wake hivyo. Tunaamn riziki popote hivyo kama yupo mjini acha tumtafutie namna kuliko akawe panya road
Mwambie Hassan Bomboko mmepima maji ni marefu mno, raia wa Dar wamekataa kuwa watumwa kwenye nchi yao.
 
Nimesima baadhi ya comments hapa halika Watanzania tunatakiwa kuwa na kiongozi mwenye maamuzi magumu hasa, yaani HASA.

Kwanza mtoa mada kagusia wafanyabiashara kama tu sehemu ya stendi ila wale si muhomu sana kwa sasa.

Ila muhimu ni matumizi ya stendi, hapo juzi tu 2000yr stendi zilikuwa tatu, ubungo, mnazi mmoja na kisutu ila Scandinavian Express alikuwa na ofisi yake pale kamata, ubungo ilikuwa stendi kuu na kuna mabasi ya mhindi yakiitwa Royal alikuwa anapakilia upanda, kisutu.

Kuna Taqwa na Tawaqal masafa marefu hawa walikuwa kule ilala, sharif shamba, mnazi mmoja na Magomeni mapipa.

Lakini mabasi yote hayo yalikuwa lazima yapitie kutoka au kuingia ubungo kwa sababi ndiyo ilikuwa Main Bus Terminal kwa jiji la Dar Es Salaam.

Baada ya kuonekana vurugu katikati ya mji ndipo serikali ikasitisha mabasi makubwa yote kuingia katikati ya mji ziishie ubungo na ilikuwa hivyo.

Na hata hii ya Magufuri Bus Terminal ni katika kupanua huduma na msongamano wa kila mtu kuwa na ofisi yake imetokana na kadhia ya vurugu mjini.

Binafsi naona ni jambo jema sana mabasi yote yaanzie pale JPM-BT Mbezi kwa sababu iliyolengwa.

Ukiwa nchini Kenya jijini Nairobi au hata mliofika Afrika ya kusini mnaweza kuelewa ukitaka kusafiri ndipo unaweza kuona umuhimu wa stendi moja ila kwa ambaye hajasafiri anaona ni ujuha.

Kuna watu hapa wanapiga kelele mkoa wa Arusha kukosa stendi, kwa nini kila bus lisipakie eneo lake, yaani watawanyike kila mtaa how come mnataka stendi ya kisasa?.

Sheria zichukue mkondo, mfano pale shekilango hadi manzese ni vurugu tu kwa mabasi makubwa, zile ni nyumba za kuishi watu ila leo mmegeuza ofisi na stendi za mabasi HOW?.
Tunajenga stand ili kurahisisha si kuongeza tatizo. Maamuzi magumu yanafanywa kabla hujaijenga sio baada ya kuijenga. Wanaotumia usafiri wa mabasi ndio wanaorahisishiwa na uwepo wa stand. Kufanya maamuzi magumu ili kuwaumiza wasafiri ni ukatili tu.
 
Hii hata mimi nimeipenda.
Fikiria mtu anayekaa kimbiji kama anasafiri kwenda Mwanza na bus linatakiwa kuondoka saa 11 alfajiri stendi ya mbezi.
Sasa fikiria huyu mtu ataamka saa ngapi na apate usafiri gani wa kumfikisha mbezi saa 11 alfajiri?Au tufanye mtu anakaa Chanika akikodi taxi itamgharimu elfu 50 kumfikisha hadi mbezi,sasa wenye mabasi wameamua kujitolea kumfuata abiria alipo na abiria ataokoa hiyo pesa ya taxi hapa sioni tatizo ila itakuwa ni faida kwa wengi.
Na kama kuna abiria anayeishi mbezi ataingojea bus hiyohiyo kwenye stendi ya magufuli itampitia sioni ubaya wowote hapa.
Kweli kabisa mkuu. Huyu utaratibu ni rafiki Kwa abiria , shida hao wauza soda na juisi wanalazimisha wote tuishie Mbezi ili tununue juisi zao.
 
Hii hata mimi nimeipenda.
Fikiria mtu anayekaa kimbiji kama anasafiri kwenda Mwanza na bus linatakiwa kuondoka saa 11 alfajiri stendi ya mbezi.
Sasa fikiria huyu mtu ataamka saa ngapi na apate usafiri gani wa kumfikisha mbezi saa 11 alfajiri?Au tufanye mtu anakaa Chanika akikodi taxi itamgharimu elfu 50 kumfikisha hadi mbezi,sasa wenye mabasi wameamua kujitolea kumfuata abiria alipo na abiria ataokoa hiyo pesa ya taxi hapa sioni tatizo ila itakuwa ni faida kwa wengi.
Na kama kuna abiria anayeishi mbezi ataingojea bus hiyohiyo kwenye stendi ya magufuli itampitia sioni ubaya wowote hapa.
Wenye mabasi lazima wawe na mbinu za kukabiliana na ushindani, (changamoto),mojawapo ni hiyo njia ya kuwafuata wateja waliko ama karibu nao, hizo fikra za kwamba wateja wote waende mbezi ni dumavu, (primitive thinking)
 
Siku zote biashara haitakiwi kutegemea Stendi, bali stendi ndio inapaswa kutegemea biashara yako, shida ni hawa wafanyabiashara walidanganywa na ccm

Nimepita hapo stendi zaidi ya mara 50 lakini sikuwahi kununua chochote, hii ni kwa sababu si lazima abiria kununua kitu hapo stendi, sasa wanacholilia ni nini?
Ni wajinga wa kutupwa. Kwa nini abiria walazimishwe kushukia na kupakia hapo? Ili tu wafaidishe watu wengine? Nchi yetu ni nchi ya hovyo kweli kweli.
 
Punguzeni roho mbaya, Yani abiria kusogezwa Mpaka kigamboni au Magomeni au Shekilango unaona ni kosa? Hii roho ya wapi hii?
Hahaha, wanataka pipi na mikate inunuliwe stand.
 
Kama ndo mpango kwamba mkoa usiwe na stand shida ipo wapi sasa kulazimishana kwenda stand? Si mpango unatimia?
Tulitoka Mnazi mmoja, wakasema tuhamie Ubungo, sasa Mbezi , sababu ni kukua kwa mji , sasa Mbezi haijakua? utashangaa tunafika mikumi
 
Back
Top Bottom