Wafanyabiashara wa mikoani mnaochukua vitu Kariakoo, njooni tujuzane machimbo ya bidhaa

Hivi Karibuni kampuni yetu itaanzisha Huduma za kuwatafutia wafanyabiashara wa mikoani bidhaa wanazohitaji hapa DSM, au nje ya nchi. Tutachukua oda zenu, tutawapa bei, mtatuma pesa, tutanunua na kuwasafirishia mlipo. Tutawatoza ada kidogo tofauti na gharama ungezitumia kuna DSM na kurudi. Stay tuned!
 
Kwa nini msinunue mzigo wenyewe then mkiufikisha kwa muhusika ndio awape pesa ili kujenga uaminifu kwanza?.
 
Kwa ujumla wafanya biashara wa Dar ni waaminifu sana na niwakalimu kuliko sisi wa mikoani maana ukituma pesa ikatokea mzigo uloagiza pesa imebaki utashangaa unapigiwa sm nakuambiwa pesa imebaki kias flani uamuz unabaki kwako uludishiwe au uongeze mzigo, mm hii imetokea Mara kibao laki wauzaji wa jumla uku mikoan usishangae anakuibia ukiwa dukani kwake, ongela zenu wauzaji wa jumla wa Dar.
 
Hawasemagi jamani, na madera yalivyo mengi.
 
Huu Uzi ni wa ukweli sana ngoja niufatilie kwa mbaaliiiii.
 
Dada Charty ongela kwa roho yako nzr km umeolewa mmeo nampa zake pongez kwa kuchagua.


Huyo mdada Charty ni mtu poa sana, hanaga ubagamoyo. Ana moyo wa kiskauti.

Na ukifuatilia michango yake mingi humu jf, utagundua kuwa ni mdada ambaye anazijua hustles za kimaisha. Siyo mchoyo wa kushea michongo au sapoti.

Ni miongoni mwa wadada wachache wa JF that will always have my maximum respect.

-Kaveli-
 
Yaan wanawake tungekuwa na roho nzuri hivi presha na mambo ya ajabu yasingetupata.
 
Mwenye kujua machimbo ya kuuza shanga, vibao vya kutengenezea mikoba, wallet, kacha n.k. atuambie wanakwetu.
 
Interesting, kwenda nje wakati mwingine gharama kubwa ila vichache mtu unachukua Dar tu, naomba unirushie namba ya inbox nikifika unipe direction ya vitu ntakavyo kuomba unielekeze.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…