Wafanyabiashara wa Tanzania hawataki kabisa kulipa kodi, wana tatizo gani vichwani? Too much kulia lia

Halafu kodi nyingi sana siyo za Wafanyabiashara.

Wao ni mawakala tu kwa niaba ya serikali lakini bado hawataki kulipa kodi mpaka kwa mbinde!

Mfano VAT, PAYE, n.k siyo hela zao lakini bado kulipa ni kwa shuruti [emoji848][emoji848][emoji848]

Bongo bahati nzuri.
 
Ila hizi fikra fupi kama mamba eti akihisi manyunyu anakimbilia mtoni asilowane ni shida tupu.
 
Ninakubali mkuu, changamoto zipo kwa pande zote. Hata wakusanya kodi baadhi siyo waaminifu. Ni kutafuta mbinu za kufichua maovu yao na kuyaweka hadharani.
 
Kodi ya elfu 20,000 ya kitambulisho? Sasa na ww unajiita mfanyabiashara?
Unameza ya maharage na karanga na unapeleka mbuzi mnadani. Mbona bado sana
JUzi nimepeleka mbuzi mnadani na nimelipa kodi. Sasa mtu anakuja na story kibao za kuhamia Kenya. So what? GO!
 
Upo sokoni Una meza YAKO unalipa Kodi ya maana kabisa.
UTOTO RAHA
Niko sokoni nina meza yangu tangu nimalize chuo kikuu. Hapa nalipa kodi ya maana kabisa! Bila hata kuzunguka kila kona nikilia lia bila sababu. Lipa kodi. Ukishindwa tafuta unakoona kodi haitakiwi.
 
Kwanza pole kwa misiba minne iliyokutokea pale white house. How are you feeling?
 
Usisugue makalio vitini na kusubiri mshahara.
Kafanye biashara na wewe ili ulipe kodi.
 
Tanzania wafanyabiashara wanalipa Kodi kubwa sana kuliko Nchi zote za sadc hapo SA ni 15% ya faida na ukiwa mfanyabiashara mdogo ufatiliwi kabisaa kama zambia hapo bongo box mbili mtu anaenda jela umasikini umewaingia kwenye damu sio bure...na Sheria za Kodi zipo wazi mapato yako kwa mwaka yakivuka kiasi fulani ulipe hivi...
 
Usisugue makalio vitini na kusubiri mshahara.
Kafanye biashara na wewe ili ulipe kodi.
Kama hiyo ndo Motto ya kufanya biashara, kwa nini wanalia-lia kila siku? Kodi kodi!
Soma message yangu #6. Usidhani kila anayefanyabiashara ni kutafuta kukwepa kodi. LIPA KODI kama mtu mwingine.
 

Mliosomea kukusanya kodi mmekuwa kama robots. Hamkuelewa somo. Mnadhani kuua biashara ndio kukusanya kodi.
Nani aliwadanganya kuua biashara ambayo hamna mchango wowote kuziazisha, ndio kukusanya kodi?
Msipoanza kuumiza vichwa vya kuongeza idadi ya walipa kodi, na kukazana kulazimisha watu wachache wawalipie watanzania wote kodi, mtafeli.
Tanzania walipa kodi ni wachache wakati wapo wengi wanazalisha vipato na hawalipi kodi. Kaongezeni wigo wa kkodi.Hizi kodi za kulazimisha hamtafika popote.
Hamuoni aibu kurudi nyuma na kuanza Kudai kodi kwenye mahesabu ambayo mlifunga wenyewe? Kama mmeshindwa kazi muache wachukue wengine
 

Kuna vilaza wamejaa kwenye ofisi za wakusanya kodi, wanadhani kutumia nguvu ndio dawa ya kusaidia mambo yaende.
 
Nimo ndani ya sekta hii ya biashara. Sehemu kubwa ni uzembe wa wafanyabiashara. Mtu anaingia kwenye biashara bila kujua mahitaji ya kisheria ya biashara yake. Angalia sheria za nchi zikoje, usiangalie waliomo wanafanyaje kukwepa hili na lile. Angalia kodi gani zinalipwa. angalia soko lako. Je, utapata faida? Then ingia. Usije faida kupitia uharifu. Siku ukisimamiwa vizuri utalia tu!

Wengi wanajiingiza kwenye biashara kwa mategemeo ya kukwepa kodi hii na ile. Nitahonga TRA, nitapunja mishahara, Sitalipa NSSF, nk. Huo ni upuuzi! HAyo yote yanapozuiliwa ndo mtu anakuja na hdithi za tupunguzie kodi, oooh mazingira siyo rafiki, oooh nchi jilani, oooh tunafunga. These are just rubbish!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…