Wafanyabiashara wa vyakula wa mkoa wa mbeya faida wanazipataje?

Wafanyabiashara wa vyakula wa mkoa wa mbeya faida wanazipataje?

Mahindi yamepanda debe 14000, Michele nao unaanza kupaa wa 35000 ni Yale matakataka ulitaka super ni 40000, mafuta lita Tano 30000, sema juice biscuit na pipi zinazotoka Zambia Bei ipo chini huku, pia Kuna simu hadi za 10000 huku mpya
 
1.Dar wali 1500 unapata yule mama anauza
2.Maziwa sawa na Dar to lita 5 ni elfu kumi
3.Chips mbeya bei yake sawa na Dar tu 2500 ,nimetoka uko juzi
4.kuna mwingine anadai eti wali kuku ni shilingi elfu 3 muongo ,nimepuyanga maeneo yote kuanzia mafiati,kabwe,mwanjelwa,sai mama john ,uyole hakuna kitu kama hicho maisha kwa sasa hata mbeya yameanza kuwa juu kutokana na muingiliano wa wageni umekua mkubwa pia wageni wengi hasa wakenya wanaenda mashambani kununua mazao,kwa sasa parachichi limepaa sana bei yake sawa na Dar tu shilingi 500
 

Attachments

  • 17412835832052491849885340647078.jpg
    17412835832052491849885340647078.jpg
    319.3 KB · Views: 1
Ndoa maana wanaitwa green city.ni mkoa uliobarikiwa kuwa na mvua nyingi,mazao mengi ya kila namna.ukiishi Mbeya ukashindwa kujenga basi nenda kwa mganga.hata bidhaa za ujenzi bado ni chini.
Na tofari ni bure kabisa. Tope tu pale kwa mama John nyumba inaenda.
 
Tunamwambia mje Mbeya
Mnajidai kung'ang'ana Dsm
Mtakuja kufa njaa.
Usiwashtue wakatuletea mabalaa, wao wanaamini utafutaji hela Mbeya ni mgumu 😀, wakati huko huko Dsm kuna watu wanalipwa hela ya mahindi ya kuchoma Uyole
 
1.Dar wali 1500 unapata yule mama anauza
2.Maziwa sawa na Dar to lita 5 ni elfu kumi
3.Chips mbeya bei yake sawa na Dar tu 2500 ,nimetoka uko juzi
4.kuna mwingine anadai eti wali kuku ni shilingi elfu 3 muongo ,nimepuyanga maeneo yote kuanzia mafiati,kabwe,mwanjelwa,sai mama john ,uyole hakuna kitu kama hicho maisha kwa sasa hata mbeya yameanza kuwa juu kutokana na muingiliano wa wageni umekua mkubwa pia wageni wengi hasa wakenya wanaenda mashambani kununua mazao,kwa sasa parachichi limepaa sana bei yake sawa na Dar tu shilingi 500
Chips 2500? Hiyo si chips yai na mayai matatu! Kwanza ni sehemu gani huko uliuziwa kwa hiyo bei? Parachichi Mbeya bei inaanzia 300, maziwa ni 1000 kwa lita eneo analokaa hiyo 10k ni mtindi, maisha sio ghali mbeya ila ni kweli kwasasa Wakenya wapo wengi kwenye parachichi kama ambavyo wapemba wapo wengi kwenye ndizi na viazi.
 
Niko mkoa wa mbeya hasa shughuli zangu zilizonileta nazifanyia mbeya mjini na Tukuyu.

Hizi bei ndogo za vyakula wanazouza zimenifanya nijiulize hawa watu faida wnazipataje.
Mfano

Kande la mahindi mabichi na maharage wanauza sh 500,wakati dar mara ya mwisho kula kande niliuziwa 2,000/=

Wali nyama bei ni 1,500/= Dar ni 3,000/=

Wali maharage ni 1,000/= wakt dar ni 2,000/=

Chips kavu bei ni 1,000/= za kushiba wanakuambia 1,500/= hizo za kushiba mwanaume wa dar hawezi kuzimaliza coz ni sahani inajaa fully.

Kitimoto kilo ni elfu 9,wakt Dar nimeacha 12,000/=
Parachichi kubwa ni 500/=
Viazi mviringo debe ni elfu 9.
Michele debe ni elfu 35.
Mahindi debe ni elfu 12.

Nyama ya ng'ombe nimeona hapo uyole bucha flani wameandika kilo ni elfu 7 wakt dar bei nimeacha ni elfu 12
Supu ya ng'ombe na ndizi tatu ni 1,500/=

Kichane cha ndizi mbivu ni elfu 1.
Maziwa lita 5 ni elfu 10
Mafuta ya alizeti lita 5 ni elfu 25
Hawa watu faida wanazipataje?
mbona hapo bei zimepanda mkuu?
kitimoto inakuwaga 6000-7000 kwa kilo

chips za buku jero unawekewa sahani mbili na kachumbali ya kutosha
 
Wilaya ya Rungwe na Busokelo ndio tajiri wa misosi. Huko Busokelo ndio wanalima sana viazi, chipsi ni kuanzia 700 ikizidi sana buku.

Mambo ya misosi sio shida zao kabisa, shida ya maeneo hayo mzunguko wa pesa ni mdogo na watu huridhika mapema.
 
Dar ya wapi hiyo wali nyama 3,000 nipajue vizuri ili siku nikiwa na ziara nitoke home nikiwa nimeshiba?

Actually ni kweli Mbeya kuna gharama nafuu za vyakula ila kwa Dar maeneo mengi regular bei za msosi ni 1,500.

Hapo hapo Mbeya ukisema ushuke wilaya ya Chunya utashangaa bei ya chakula ilivyokuwa ghali.
Chunya kila kitu bei ghali, hadi wadada wanaojiuza kule kuna hela ukimpa anakuona takataka wakati hela hiyo hiyo ukimpa msichana hapa mjini anaona ameokota buzi
 
Mimi nimeishi Mbeya maisha yangu yote, Airport ndo mtaa niliozaliwa. Nimesoma Mbeya kuanzia elimu ya msingi hadi chuo kikuu, nimetoka Mbeya mara chache sana na kipindi nikichotoka muda mrefu zaidi ni mwezi mmoja (napo nilikuwa locked up Morogoro).

Miaka kama mitatu iliyopita nilihamia Uyole, maisha ya huku nilishangaa kama ambavyo mtu anaetoka Dar anavoshangaa Mbeya. Huku vitu ni zaidi ya bei rahisi, sio vyakula, sio sehemu za kuishi, sio pisi!
 
Back
Top Bottom