Wafanyakazi Mgodi wa CATA Mining Mara waandamana, wakidai Mishahara, NSSF, wamwangukia Rais Samia

Wafanyakazi Mgodi wa CATA Mining Mara waandamana, wakidai Mishahara, NSSF, wamwangukia Rais Samia

KwetuKwanza

Member
Joined
Mar 13, 2023
Posts
82
Reaction score
150

IMG-20240912-WA0016.jpg

Waliokuwa wafanyakazi wa mgodi wa dhahabu wa CATA MINE uliopo kijiji cha Kyabakari, Wilayani Butiama Mkoani Mara, jana wameandamana kwa mara nyingine kuelekea katika Ofisi za mgodi huo, kushinikiza mwekezaji kuwalipa malimbikizo ya mishahara yao pamoja na NSSF.

Wakiwa na mabango yenye jumbe Mbalimbali wafanyakazi hao zaidi ya 300 wamesema kuwa mpaka sasa hawajui hatma ya haki yao, kwani wamefanya jitihada zote za kufika hadi kwa Waziri wa Madini lakini hakuna kilichofanyiwa kazi.

Wamemuomba Rais Dkt. Samia kuingilia kati jambo hilo, kwani kwa muda mrefu wameachishwa kazi bila ya kulipwa mishahara yao, huku viongozi wa serikali akiwemo Waziri wakishindwa kutatua shida yao.

Mbele ya waandishi wa Habari, wafanyakazi hao wamesea kuwa wanadai zaidi ya miezi 20 mishahara yao huku wengine wakidai miezi nane, ambapo wamesema mwekezaji huyo hajawahi kuweka fedha zao NSSF tangu wameanza kazi.

“ Kila siku tukifuatilia tunawambiwa njoo kesho, njoo Kesho, maisha yetu kwa sasa magumu sana, tumeenda kwa viongozi wote wa serikali akiwemo Waziri wa Madini lakini imeshindakana, tunamuomba mama aingilie kati Jambo hili,” alisema Joshua Chamolo,

IMG-20240912-WA0020.jpg

IMG-20240912-WA0023.jpg
Walisema kuwa madai ya NSSF ambayo wanamdai mwekezaji huyo ni zaidi ya Bilioni 7, huku Mishahara ikiwa ni zaidi ya miezi 20, “ Tumeangaika sana, sasa tunamuomba Rais Samia atusaidia na sisi ni watanzania, tunaomba aingilie kati huyu mwekezaji hatujui yuko wapi mpaka sasa,” alisema Ally Abas.

Aidha, walisema kuwa mgodi huo ulisimama kufanya kazi tangu mwezi Desemba 2023, ambapo baada ya shughuli zote kusimama hakuna taarifa yoyote ambayo ilitolewa kwao wala barua ya kusimamishwa kazi.

Soma Pia: Wafanyakazi mgodi wa CATA Mining Mara, waanza mgomo kushinikiza kulipwa mishahara, michango NSSF

Wanabainisha viongozi wote wa mgodi huo akiwemo mwekezaji hawaonekani eneo la mgodi, na wamehaingaika sana kuwapata na imeshindikana.
 

Attachments

  • IMG-20240912-WA0018.jpg
    IMG-20240912-WA0018.jpg
    67.9 KB · Views: 6
Huyo ni financial crisis of the company ... Na ni kawaida.. Cha muhim ni kuwa na subra na kuvumilia mambo yakae sawa walipwe..

Hapo unakuta mwekezaj hajapata hata senti ya uwekezaji wake na hajavuna Mali inayoweza kumpa liquidity ya kutosha.. .

Ni bahati mbaya lakini nimemsikia akisema walipata hela watalipa...

Namna nzur angewapa hao wafanyakaz sehem ya share za mgodi wake kama stocks... Ili hata hela zikipatikana baadae kabisa huko angalao vizaz vyao vinufaike...

Poleni sana ndugu zangu
 
Huyo ni financial crisis of the company ... Na ni kawaida.. Cha muhim ni kuwa na subra na kuvumilia mambo yakae sawa walipwe..

Hapo unakuta mwekezaj hajapata hata senti ya uwekezaji wake na hajavuna Mali inayoweza kumpa liquidity ya kutosha.. .

Ni bahati mbaya lakini nimemsikia akisema walipata hela watalipa...

Namna nzur angewapa hao wafanyakaz sehem ya share za mgodi wake kama stocks... Ili hata hela zikipatikana baadae kabisa huko angalao vizaz vyao vinufaike...

Poleni sana ndugu zangu
Hakuna mining investor ambae anaweza kubali kutoa share kwa watumishi wake.
Maranyingi hua wanaamua kuuza Mine ikiwa wanaona wamezidiwa.
 
Hakuna mining investor ambae anaweza kubali kutoa share kwa watumishi wake.
Maranyingi hua wanaamua kuuza Mine ikiwa wanaona wamezidiwa.
Ikibidi walazimishwe Ili kulinda haki za hao wafanyakazi...
Ni bahati mbaya kwamba wanaweza wakauza na wakaondoka bila hao watu kulipwa
 
Back
Top Bottom