Wafanyakazi wa ofisi za serikali acheni roho mbaya

Wafanyakazi wa ofisi za serikali acheni roho mbaya

mimi nilikua na watu tunaofahamiana baadhi ya ofis ila mpka sasa sijatoboa miez 3 ila nyie mliopo humu km upo kitengo chochote ebu
Tatizo sasa ivi ni kwamba hata Ofisin hawaaminiani hapo, Kwamba Eti huyu ni ndugu yangu nataka nimfanyie chap, wenzake watakwamisha wakijua kwamba Jamaa anawazuga apate cha juu; Nilikuwa namtuma bwana mdogo wangu anifuatilie Vitu flani vya Ardhi Dodoma jiji, ambako nina Uncle wangu pale; Ikawa ikawa inachukua muda kweli; Niliporud Tz nikafatilia mwenyewe ikawa hivyo hivyo, Nikaamua Kukata Pochi; hapo mambo yalienda faster. So hata kama una Ndugu, kama hutaki kupoteza muda na Pesa ipo, ni vizuri kuwasupport ndugu zetu wale; Maana mzee amebana huko nchini kwetu sasa hao ndugu zetu mambo yamewabana pia.
 
Njaaa kwao imeshakuwa Shujaa watafanyajee ss anavyokuambia njoo baada ya wiki mbili ukijaa atakwambia tenaa njoo baada ya wiki tatu usipojiongezaa utapangiwa sanaa wikii mwishowe akiona ujiongezee anakupangiaa miezii ss,maaninaa hapoo ndio miezii inaendaa hatimaee mwakaa
 
Baba lao ofisi ya Utumishi kwa anuani ya katibu mkuu utumishi, utamaliza mwaka au na zaidi hujajibiwa barua. Nimeona ni kupoteza muda kumwandikia katibu mkuu utumishi barua. Ile ofisi ilitakiwa iwe kielelezo bora lakini ni kinyume chake. Mama lao PSSSF, tuko dunia ya digitali umewapelekea mahitaji yote, mwaka unakata unaambiwa wanashughulikia. Zile ni pesa zetu tulizideposit kama tunavyoweka pesa benki, kwanini ku-withdraw au kutoa iwe nongwa? Kama mwanzisha mada alivyosema ole wako umkute mwanamke, wana roho mbaya sijawahi ona. Halafu mnasema wanawake ni waadilifu?
 
Mdogo wangu alifiwa na mumewe aliyekuwa mtumishi wa umma mwaka 2019. Baada ya kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi alianza kufuatilia mafao ya mumewe PSSSF tangia wakati huo. Mpaka wakati huu naandika hawajamlipa na ana watoto wanasoma wako sekondari na kuna moja yuko chuo. Dodoma ameenda zaidi ya mara tatu lakini bado wanamwambia wanashughulikia. Mkurugenzi mkuu ndugu yangu mpaka upigiwe simu na ndg Polepole?
 
Baba lao ofisi ya Utumishi kwa anuani ya katibu mkuu utumishi, utamaliza mwaka au na zaidi hujajibiwa barua. Nimeona ni kupoteza muda kumwandikia katibu mkuu utumishi barua. Ile ofisi ilitakiwa iwe kielelezo bora lakini ni kinyume chake. Mama lao PSSSF, tuko dunia ya digitali umewapelekea mahitaji yote, mwaka unakata unaambiwa wanashughulikia. Zile ni pesa zetu tulizideposit kama tunavyoweka pesa benki, kwanini ku-withdraw au kutoa iwe nongwa? Kama mwanzisha mada alivyosema ole wako umkute mwanamke, wana roho mbaya sijawahi ona. Halafu mnasema wanawake ni waadilifu?
Du, aisee 😄😄 nakata tamaa kbsa maana psssf nilichukua tu zile form bado kujaza na kuziludisha nikajua wao ndo watakua faster kumbe ni km nssf tu🙌
 
NSSF KIBAHA Kama unaweza kuombea mafao yako kwingine nenda huko.
NSSF kibaha Ni mwisho wa maneno kwa kusumbua watu.
Yuko mdada mmoja pale kaunta ya mbele kabisa.. sijui Hana wazee yule au bwanake Ni mstaafu. Sio kwa chuki Ile kwa wanaodai haki yao
 
pole mtumishi
Usinijadili mimi maana hunijui, jadili tatizo lilipo mezani.
Uonevu katika nchi huzaa uovu, yote ni matatizo ya uongozi mbovu, kama hali itaendelea hivi basi tutarajie mabaya zaidi.
Juzi umesikia polisi wamegawana nyama kituo cha polisi Buguruni, kuna taasisi huko kama Tanesco bila rushwa hata umeme huupati kirahisi hata kama umekamilisha taratibu,
 
Karibu 80% ya ofisi za umma wako hivo
Tra
Uhamiaji
Rita
Kitu kidogo uwahishiwe huduma

Mpaka hospitality za serikali hivohivo
Vyuo vya serikali hivohivo.usipokutana na kitu kidogo basi tarajia dharau
 
kuna wale wanasema nidhamu kazini imerejea, sijui huwa wanamaanisha nini kwa kweli. Pita pita ardhi na idara zake zote ndio utawafahamu vizuri watumishi wa Umma, Mungu awaponye huu ugonjwa kwa kweli.

Kiwanja mwekezaji amenunua 87M bado anatakiwa atoe chai ili hati itoke haraka!!!!

Mkuu salute kwako, umeniwahi nilichotoka kusema kuhusu uwajibikaji. Majizi ya kura yakipanda jukwaani wanasema nidhamu imerejea kwenye ofisi za umma ili kuhadaa umma, wakati uhalisia ni kinyume chake kabisa.
 
Usinijadili mimi maana hunijui, jadili tatizo lilipo mezani.
Uonevu katika nchi huzaa uovu, yote ni matatizo ya uongozi mbovu, kama hali itaendelea hivi basi tutarajie mabaya zaidi.
Juzi umesikia polisi wamegawana nyama kituo cha polisi Buguruni, kuna taasisi huko kama Tanesco bila rushwa hata umeme huupati kirahisi hata kama umekamilisha taratibu,
relax mtumishi.
 
Back
Top Bottom