Wafanyakazi wameandaa mabango na T-shirts zao lakini wanapita mbele ya Rais Samia kwa kukimbizwa kama mbwa mwizi

Sexless

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2017
Posts
23,683
Reaction score
55,898
Kama Rais hana muda wa kupokea waandamanaji wote basi waratibu wa sherehe hizi za Mei Mosi walipaswa kupunguza makundi ya waandamanaji.

Watu wamepoteza muda wao kujiandaa, wakatafuta na t-shirts halafu wanapita mbele ya mhe rais wakikimbizwa kama kuku wa mgeni ama mbwa mwizi.

Watu wazima wanakimbizwa kama watoto wa shule za msingi. Inachefua hata kuangalia kupitia runinga.

Aibu naona mimi.
 
Wanawahi muda ili wasicheleweshe ratiba nyingine, ajabu hata kama tukio linawahusu wao!.

Watu walioshikwa akili namna hiyo ndio waweze kuitisha migomo ya kudai haki zao?!

Never.

Hao ni kondoo wa serikali, ndio maana wako hapo kwa bosi wao kumlilia awaongezee mshahara.
 
Aahhaaaaaa

Nipo hapa na jezi la kijivu hapa stejini napunga mkono

Mkuu hujaniona!?
 
Tanzania hamna Wafanyakazi....
 

Ajira ni kama ndoa, hakuna cha kulalamika
 
Kwa nini wafanyakazi wamejichokea sana?tatizo nini?au mishahara yenu haiwatoshi?Ninawaangalia hapa kwenye tv,nawaona wamechoka sana na kibaya zaidi mabango yao ni ya kumsifia rais tu.
 
πŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒ
 
Sasa kama unasema wanakimbizwa je wanapokuwa kwenye mazoezi yao binafsi kuweka miili yao fit kwa jogging au gym utasemaje.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…