TANZIA Wafanyakazi watano wa TRA wafariki dunia kwenye ajali

TANZIA Wafanyakazi watano wa TRA wafariki dunia kwenye ajali

Papaa Mobimba

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2018
Posts
882
Reaction score
3,337
Wafanyakazi watano wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) kikosi kazi cha Fast Track wamefariki dunia kwa ajali ya gari aina ya Landcluser lililogonga kwa nyuma Lori aina Fuso. Walikuwa wakifukuzana na gari iliyodhaniwa kubeba magendo

Ajali hiyo imetokea leo Agosti 23, 2021 saa 11 alfajiri katika barabara ya Mbeya Tunduma eneo la Hanseketwa Wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe.

Kaimu Meneja wa Forodha wa TRA wa Tunduma, Omary Mnzava amewataja watumishi watano wa mamlaka hiyo kikosi kazi cha fast track waliofariki ajalini leo asubuhi Jumatatu mkoani humo ni Azari Shifonike ambaye ni dereva, Joel Mitondwa, Saidi Buddy, Fahad Hassan na Benard Mashingi.
1.jpg

3.jpg

2.jpg

TRA.jpg

waagwa.jpg
 
Wapumzike kwa amani ila madereva wa serikali wako rough sana.

Juzi kidogo waue familia ya ndugu yangu nzima. Wana overtake mlimani halafu hawaoni mbele na wako spidi wanafukuzana.

Ndugu yangu alipoona msalaa wa kugongana ilibidi aingie vichakani usiku.
 
Ki
Wapumzike kwa amani ila madereva wa serikali wako rough sana.

Juzi kisogo waue familia ya ndugu yangu nzima. Wana overtake mlimani halafu hawaoni mbele na wako spidi wanafukuzana.

Ndugu yangu alipoona msalaa wa kugongana ilibidi aingie vichakani usiku.
akajiokoa kwa style hio 😹😹😹 hawa madereva wa SU na ST wanazingua sana wakiwa highway
 
Wafanyakazi watano wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) wamefariki dunia kwa ajali ya gari aina ya Landcluser lililogonga kwa nyuma Lori aina Fuso.

Ajali hiyo imetokea leo Agosti 23, 2021 saa 11 alfajiri katika barabara ya Mbeya Tunduma eneo la Hanseketwa Wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe.

Polisi imethibitisha.
Mi sio trafiki, ila hawa jamaa wanaonekana walikua wana overtake wakakutana face to face.. maana wapo upande wa kulia.. yaan ugonge gari kwa nyuma uchakae hivo?
 
Back
Top Bottom