Waganga wa kienyeji na wachawi ni mawakala wa shetani, kwanini wanapingana

wakuu hebu tusaidiane.
waganga na wachawi ni wakala/agents wa ibilisi/shetani
kwanini wanapingana
mchawi anakuroga ufe, mganga anakutibu usife
cc rakims
ccmshanajr
walker water
Hawapingani, wanazuga tu
Chama lao Moja!

Infact Kila mganga ni mchawi pia!
Haiwezekani watu wako kwenye himaya Moja halafu wapingane..ndo maana unaambiwa waongo..👇👇👇
 

Attachments

  • Screenshot_20240412-102353.jpg
    402.1 KB · Views: 20
Ukienda Kwa mganga, mchawi Huwa anampigia simu kichawi, wanajadiliana,

Ni kama tu biashara, ukipata mteja akaulizia Kisha akaondoka kwenda duka la Jirani, unampigia Jirani Ili terms ulizompa mteja zisibadilike.

Ukitupiwa jini Moja na mchawi, mganga atakuongezea mengine Saba ya kulituliza Hilo Moja Kwa muda, baadae utapata shida mara Saba ya uliyopata mwanzo, au anakuweka kwenye mikataba itakayokufuata Hadi vizazi vijavyo Ili muendelee Kutoa sadaka na kuyaabudu mashetani.

Kwa Mungu ndipo pazuri, Pana Kila kitu.

Amen
 
Ufalme wao pia una ranks....
Kinachofanyika ukienda anaangalia hayo makitu uliyonayo km Yana kiwango Cha chini kuliko aliyonayo yeye ,akiona hizo spirit zinazokusumbua ziko chini anayanyanazisha tu Kwa kukuwekea yenye uwezo zaidi Ili Yale uliyonayo yasikusumbue.....

Ndo maana kuna wengine ukienda anaangalia, utasikia hii siwezi nenda sehem Fulani,ujue yamemzidi kiwango 😅

Wengine sikuhizi hawafichi akichungulia akiona huu mziki mnene anakwambia katafute wale Wana maombi watakusaidia....(Nina watu washaambiwa hivyo baada ya kuhangaika ,tabora zenj huko😅)
 
umenifungua akili mkuu
ila niulize kitu. waganga wote wanatumia majini?
 
kumbe unaweza kwenda kutafuta tiba, ukatuliza tu maumivu kama kumeza panadol
 
Kwa Mungu wapi kwa sababu tunasikia tuhuma za baadhi ya manabii hutumia nguvu za giza kama source ya nguvu zao katika kutenda miujiza.
 
Walokole wahaheshimika sana huko katika medani za Ulimwengu wa Roho.

Kwa nje utawaona wa kawaida, ndani ni giants hatari.
 
Mganga wa kweli ana lengo la kuondoa matatizo, mchawi anayaweka, tatizo waganga wengi sikuhizi wameingia tamaa wamegeuza matatizo yawe fursa na hapa ndio huingiza uchawi wa kupunguza matatizo kidogokidogo ili wenye nayo warudi kila muda, kuyaongeza, kuchukua rushwa kwa walioroga ili mhanga asipone, n.k.
 
Wote wanatumia, ila viwango vinatofautiana.

Kuna majini, mapepo, Mizimu na mashetani,

Ni Yale Yale lakini katika levels tofauti.
Yale yale kwa maana ipi ya asili yao au tabia zao?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…