Wagner wamepewa kazi ya kuishughulikia Poland?

Wagner wamepewa kazi ya kuishughulikia Poland?

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Mpaka sasa haijakuwa wazi sana juu ya kilichotokea pale kiongozi wa Wagner, Prigozhin alipofanya uasi na kuelekea kama kutaka kuipindua serikali ya Urusi.

Nchi rafiki za Ukraine zilionenaka kufurahia tukio lile japokuwa wachache walitilia mashaka mtiririko mzima wa matukio.Jambo lililowashangaza wengi ni makubaliano ya ghafla ya kumpeleka kiongozi huyo uhamishoni nchini Belarus ambaye ni mshirika mkubwa na jirani na Urusi.

Pamoja na zawadi hiyo aliyopewa Rrogozhin baada ya uasi bado akaongezewa kupelekewa askari wa vikosi vyake na baadae silaha na pesa.

Belarus pia ni jirani na nchi ya Poland ambayo nayo ni mshirika mkubwa na mjumbe wa jumuiya ya NATO. Nchi hiyo vile vile ni njia kubwa ya kupitishia silaha zinazotolewa kama sadaka na zinazonunua Ukraine kwa ajili ya kuendesha vita hivyo na Urusi.

Kabla hata miezi miwili kufika tayari vikosi vya Wagner vimeonekana kwenye mpaka wa Poland na Belarus na hapo juzi helkopta za Wagner zimelalamikiwa na Poland kwamba zimeingia ndani ya maeneo ya mipaka yake.

Harakati hizo za kuongezeka harakati za Wagner inavyoonekana zimeanza kuishtua Poland mbapo sasa imeanza kutoa kauli za kupingana na mipango ya Ukraine katika vita vyake ambazo nyengine Poland imesema zinafanyika bila kushauriana nao.
 
Huoni toka Wagner waende Belarus Poland kama wameikacha Ukraine?, Putin ni mtu wa akili sana amewapelekea Wagner ili nguvu zote waelekeze Belarus.

Ila tuache masikhara hawa Wagner ni hatari wanaogopeka na Upinde balaa
Ni ujinga kuamini kikundi kama Wagner kinaweza kuifanya Poland chochote. Belarus mwenyewe kwa Poland hachukui round sembuse kikundi cha askari sijui elfu 30. Hofu iliyopo ni kuwa wanaweza kujifanya ni wakimbizi na kwenda kufanya vitendo vya kigaidi kwenye nchi za Ulaya, nje ya hapo hapo hakuna tishio lingine lolote.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Ni ujinga kuamini kikundi kama Wagner kinaweza kuifanya Poland chochote. Belarus mwenyewe kwa Poland hachukui round sembuse kikundi cha askari sijui elfu 30. Hofu iliyopo ni kuwa wanaweza kujifanya ni wakimbizi na kwenda kufanya vitendo vya kigaidi kwenye nchi za Ulaya, nje ya hapo hapo hakuna tishio lingine lolote.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
Lkn hapo hapo ulikua unaamini hao mamluki wanaweza kumpindua putin? Nyie watu huwa mna matatizo gani?
 
Ni ujinga kuamini kikundi kama Wagner kinaweza kuifanya Poland chochote. Belarus mwenyewe kwa Poland hachukui round sembuse kikundi cha askari sijui elfu 30. Hofu iliyopo ni kuwa wanaweza kujifanya ni wakimbizi na kwenda kufanya vitendo vya kigaidi kwenye nchi za Ulaya, nje ya hapo hapo hakuna tishio lingine lolote.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app

Sasa mbona wanalialia kama ni kweli haya unayozungumza??, si waivamie Belarusi?
 
Ni ujinga kuamini kikundi kama Wagner kinaweza kuifanya Poland chochote. Belarus mwenyewe kwa Poland hachukui round sembuse kikundi cha askari sijui elfu 30. Hofu iliyopo ni kuwa wanaweza kujifanya ni wakimbizi na kwenda kufanya vitendo vya kigaidi kwenye nchi za Ulaya, nje ya hapo hapo hakuna tishio lingine lolote.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
Ni ujinga zaidi kushindwa kuona NATO anavyotaabishwa na kuadhiriwa huko Ukraine na hao hao Wagner. Halafu uamini Poland hatishwi..!

Usidhani Poland atapigwa kishkaji ka Ukraine, yule atashushiwa vitu vizito kweli kweli na Russia atajifanya hayuko nyuma yao
 
Ni ujinga zaidi kushindwa kuona NATO anavyotaabishwa na kuadhiriwa huko Ukraine na hao hao Wagner. Halafu uamini Poland hatishwi..!

Usidhani Poland atapigwa kishkaji ka Ukraine, yule atashushiwa vitu vizito kweli kweli na Russia atajifanya hayuko nyuma yao
Hizi akili za kijima za namna haziwezi kukusaidia kwenye jambo la maana maishani.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Ni ujinga zaidi kushindwa kuona NATO anavyotaabishwa na kuadhiriwa huko Ukraine na hao hao Wagner. Halafu uamini Poland hatishwi..!

Usidhani Poland atapigwa kishkaji ka Ukraine, yule atashushiwa vitu vizito kweli kweli na Russia atajifanya hayuko nyuma yao
Vita ni akili.Bila shaka Putin amejua kuwa nguvu ya Ukraine katika vita inatokana sana na ushirikiano na Poland kwa vile anavyoruhusu ardhi yake kuwa mapitio makubwa ya silaha.Kwa vile Poland ni mwanaachama wa NATO ni kuwa Urusi ikiipiga moja kwa moja kutapatikana kisingizio kuwa ameipiga NATO na makele kuongezeka.
Dawa ni Wagner wafanye vitu vya kuitaabisha Poland kwa niaba ya Urusi na uwezo wa kuzonga zonga Wagner wanao.Urusi itajifanya kama haioni na ikiulizwa itasema haijui wala haihusiki na kikundi hicho ambacho wao NATO wanajua kiliwahi kutaka kuiteka Moscow. Mbinu hii kwa vita ya muda mrefu itaipa Urusi nafasi nzuri ya kurudisha nguvu na kujiimarisha kuipiga Ukraine.
 
Vita ni akili.Bila shaka Putin amejua kuwa nguvu ya Ukraine katika vita inatokana sana na ushirikiano na Poland kwa vile anavyoruhusu ardhi yake kuwa mapitio makubwa ya silaha.Kwa vile Poland ni mwanaachama wa NATO ni kuwa Urusi ikiipiga moja kwa moja kutapatikana kisingizio kuwa ameipiga NATO na makele kuongezeka.
Dawa ni Wagner wafanye vitu vya kuitaabisha Poland kwa niaba ya Urusi na uwezo wa kuzonga zonga Wagner wanao.Urusi itajifanya kama haioni na ikiulizwa itasema haijui wala hihusiki na kikundi ambacho wao wanajua kiliwahi kutaka kuiteka Moscow. Mbinu hii kwa vita ya muda mrefu itaipa Urusi nafasi nzuri ya kurudisha nguvu na kujiimarisha kuipiga Ukraine.
Ebu niweke sawa[emoji1787],

[emoji117]Wagner wakimchapa Poland,Poland atajibu mapigo Kwa kuichapa Belarus Kwa kuwa wanatokea humo?

[emoji117]Kwa kuwa Poland ni mwanaNato,je NATO wataingia rasmi kijeshi na Belarus.
 
Ebu niweke sawa[emoji1787],

[emoji117]Wagner wakimchapa Poland,Poland atajibu mapigo Kwa kuichapa Belarus Kwa kuwa wanatokea humo?

[emoji117]Kwa kuwa Poland ni mwanaNato,je NATO wataingia rasmi kijeshi na Belarus.
Kitrndawili rahisi hicho kuteguliwa.
Angalia kwamba taarifa zipo za uhakika kuwa Marekani na NATO yote wako hali mbaya kutokana na vita vya Ukraine.Uchumi umeporomoka na hata silaha za kuisaidia Ukraine zimewaishia.Kumbuka raisi Biden amesema sababu ya kuipa Ukraine mabomu haramu (cluster bombs) ni kwa vile wameishiwa na marisasi ya mizinga mpaka hapo baadae. Sasa iwapo Polanda atashughulikiwa na kikundi kisichojulikana kimataifa basi Nato haitoweza kuikoa Poland wakati tayari wameshindwa kule Ukraine.
 
Ni ujinga kuamini kikundi kama Wagner kinaweza kuifanya Poland chochote. Belarus mwenyewe kwa Poland hachukui round sembuse kikundi cha askari sijui elfu 30. Hofu iliyopo ni kuwa wanaweza kujifanya ni wakimbizi na kwenda kufanya vitendo vya kigaidi kwenye nchi za Ulaya, nje ya hapo hapo hakuna tishio lingine lolote.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
huo ndio uhatari na kuogopwa kwenyewe.
 
Huoni toka Wagner waende Belarus Poland kama wameikacha Ukraine?, Putin ni mtu wa akili sana amewapelekea Wagner ili nguvu zote waelekeze Belarus.

Ila tuache masikhara hawa Wagner ni hatari wanaogopeka na Upinde balaa
Kichapo walichomeza Backmut hadi walianza kulia lia na kuona heri wampindue putini kuliko kupambana na Zele Atawamaliza
 
Lkn hapo hapo ulikua unaamini hao mamluki wanaweza kumpindua putin? Nyie watu huwa mna matatizo gani?
Putini imebidi amtake radhi! Bila belarus kuingilia kati putin hatunae!
 
Back
Top Bottom