Wahubiri wangu wa mfano Tanzania

Hata mwamposa,watu wanapona watu wanataka vitendo sio maneno tu
 
bora hata kuhani musa
Yule kwa mtu mwenye akili timamu hawezi kaa chini na kumsikiloza Kuhani Musa. Ni bora mara sabini nirudi kunuwa ulanzi kuliko kwenda kusali kwa Kuhani Musa,Mwamposa, Sijui shilla au Bashando au Yule mama Shaboka au mtalemwa au Masanja. Bora nirudi kwenye umalaya wangu wa zamani tu kuliko kukaa pale niwasikilize. Eti unamsikiliza Maboya, Mgogo, Kapora, Mashimo, Geordavie, Malisa au mchungaji sijui Mtume au nabii wa namna hii.
 
Mkuu kitabu chake napata wapi?
 
Hao wote ni matapeli wa kidini wanatumia dini kujinufaisha
 
Kwenye list yako, wa kimataifa 90% ni fake. Local 70% fake.
Tusaidie na majina yao tuwatambue kama walivyoandikwa hapa. Usiishie kuandika %. Hivi hutusaidii tunaofuatilia Kutaka kujua tofauti yao: real&fake.
 
Uko sahihi sana. Nafkiri mada ilitakiwa kuzitaja kazi za watumishi na si kulinganisha sifa bila vigezo.
Nitatoa mfano, Paulo, mtumwa wa Yesu Kristo anasema yeye ni zaidi ya wale thenashara. Lakini zaidi katika nini? Ni katika kufungwa, katika kufunga, katika dhoruba na katika mapigo. Yaani zaidi katika taabu ya injili. Lakini pia yeye ndiye aliyefanya kazi ya kusambaza injili zaidi kwa mataifa. Lakini pamoja na yote hakuwadharau wenzake, isipokuwa aliwaonya kwa upendo.

Pia, ikumbukwe hizi karama za roho hutolewa na roho kadri apendavyo roho mtakatifu. Mwingine mwalimu, mwinjilisti, utume na unabii.

Neno linatuagiza tuzijaribu kila roho, tupime au tuwatambue watumishi kwa matunda yao na maisha yao kwa ujumla. Na pia tuangalie nani kawaachia joho, yaani tuangalie baba zao wa kiroho.

Paulo aliitwa na Yesu akapewa Philipo, kuna Elisha na Eliya, kuna Musa na Haroun, Joshua na Caleb, kuna Paulo na Timotheo. Watoto wa Kulola na Lazaro unapata TAG / EAGT hapo kwa DSM hapo ma nguli kama Katunzi, Kakobe na wengi ambao wameanzisha huduma na zimesimama imara mpaka sasa.

Hivi ndivyo vipimo vya kibiblia. Ni muhimu kukumbuka kuwa hiyo ni mifano michache. Wapo watumishi wa Mungu wanafanya kazi kubwa hasa vijijini na wanatumika kweli kweli lakini hawaimbwi sana masikioni mwa watu. Ukiwa mfatiliaji wa injili utalielewa hili.
 
Alikujibuje?
 
Kasikilize mkuu utafaidika zaidi ina part one na two ni kitu kizito kuandika inachukua muda.
Huu ni ujinga wa kiroho. Neno la Mungu halifichwi. Neno ni gharama lakini tunalitoa bure kwa kuwa tumepewa bure na Mungu.
 
Pastor Daniel Mgogo
Yuko vizuri sana ila kuna ujasiliamali wa injili huwa wanaufanya. Yaani wanaangalia watu wanataka kusikia nini. Yaani wanafata masikio ya utafiti ya watu. Wanagusa matatizo ya ndoa na mahusiano kuliko dhambi.
 
Je? Kuna watumishi wa mungu ukifka tu wanataja matatizo yako before ujawaelezea? Hii imekaaje wataalam??

Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app
Kuna contest.
Mungu akimfunulia hivyo mtumishi lazima utukufu uende kwa Mungu na si kwa Mtumishi. Ukiona hiyo ndiyo inakuwa huduma maalumu tena mathalani ikawa inalipiwa kwa kiasi fulani cha pesa. Ujue kuna hila hata kama kuna injili ya kweli.
 
Dhambi hata ukimtamani mwanamke hakika umekwisha kuzini nae.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…