Wahudumu na Uongozi wa Fish Market mnaishiriki dhambi mbaya ya ubaguzi pasipo kujua malipo ni hapa hapa

Wahudumu na Uongozi wa Fish Market mnaishiriki dhambi mbaya ya ubaguzi pasipo kujua malipo ni hapa hapa

Huko wavuvi camp kukoje.
Maana dogo kaniambia jana twende huko coco beach panaitwa wavuvi camp.
Sasa nisije kupata tena maumivu ya kichwa wiki nzima.
Hakuna hata maajabu sema tu ndo vile kiwanja kikiwa kipya watoto wote wa mjini wanaenda,
Bei zao ni kama za Samaki Samaki ila wao zimezidi kidogo, wana MENU yao pia angalia akaunti yao Insta Wavuvi Kempu.
 
Hii ni common experience migahawa mingi ya Masaki ambayo ni upscale. Bei za ajabu kwenye menu items. Utegemee kupata huduma mbovu kama ni Mtanzania mweusi. Wahudumu watajifanya hawakuoni, wapo busy na wateja wazungu. Order yako itachukua muda sana, unaweza kuja kabla ya mzungu, lkn mzungu akaanza kula kabla yako.
 
Kiwanja cha wajanja kwa sasa ni Dar es salaam Johari Rotana,(a 5 star hotel)
Pananoga pale asikwambie mtu esp Fridays...ila tu uwahi 8th floor swimming pool by 6-7 uwe umekalia seat otherwise utakaa bar ndani..maana ni fire

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
soon wadada wadangaji wa mujini wataenda kuweka kambi hapo johari rotana.

mbinu yao ni ilele ya zamani tangu enzi za kina
jacqueline ntuyabaliwe kipindi hicho wanadanga kwenye mahotel kuvizia wazungu.

watawahi seat, wataagiza savana au serengeti lite mojamoja na kuinywa masaa matatu.

siku nyingine wakirudi halafu wahudumu wakapuuza kuwauhudumia kwa wakati,watakimbilia tiktok kwenda kulalamika.
 
Hakuna aliyebaguliwa hapo CTFM bali hao ni makahaba wanaoenda kujaza viti na kusumbua wateja na kuwaibia wakiwa wamelewa,

Ndio maana sasa hivi viwanja vingi kuna utaratibu wa Table Reservation kama hujaweka meza huingii ndani na kuanzia saa moja ndio wateja halisi huanza kuingia kwa hiyo hao makahaba unaowatetea huambiwa wapishe meza za wateja waliozizuia kitendo hicho hukiita ubaguzi ila deep down wanajua kabisa wanakosea (ilishatukuta hii Wavuvi Kempu baada ya wadada kunyanyuliwa sie tukae wakagoma hadi walipokuja walinzi ndio wakatoka) kiufupi wahudumu wanawajua vema hao wadangaji na usumbufu wao,

Tanzania hakuna Ubaguzi wa Rangi sio kwa karne hii.
Kama huyo aliekuwa analalamika hayo malipshine anaonekana ni kahaba mzoefu
 
Huku kwetu wali nazi 100 ukifika unakutana na tabasamu la Odo Mammi, hujakaa sawa unafuatwa na Chonge mrembo mweupe, hapo Saumu Mashauzi anakukonyeza kwa kukuminyia jicho, Miza nae anakuegemea bega anakuuliza utakula samaki wa kupwaza na maharage ya kukata au samaki makange Maarufu kama Samaki Makange Nuksi..... unaulizwa utakula na wali wa nazi ngapi 3, 6, 9 kbl hujajibu Mama mkubwa anajibu huyo anakulaga wali wa nazi 3, mwingine anadaki mchicha je unataka wa kuloweka kwa tui au wakulowekwa kwa maji ya madafu...
Njooni huku kwetu barabara ya 17 ali maarufu kwa jina la wali nazi 100 hutalalamika, unahudumiwa hadi unahisi kabisa unamlipa pesa pungufu. Mbarikiwe nyie kina mama hapo Barabara ya 17, nazunguzia Tanga hiyo wazeee, njooni!!!
....
giphy.gif
 
Back
Top Bottom