Wahudumu na Uongozi wa Fish Market mnaishiriki dhambi mbaya ya ubaguzi pasipo kujua malipo ni hapa hapa

Huyu hata mimi ngemnyima kukaa. Akakae huko kwake.... Jinsi anavyoongea....ana mdomo sana. Na hana hata point. Anasema amenyimwa kukaa kisa hali. Sasa yeye alitaka aende pale akapige picha mezani atume insta " nasubiria chakula hapa fish market" kisha ainuke aondoke..... Huyo dada sitaki hata awe mteja wangu na mimi
 
Huko wavuvi camp kukoje.
Maana dogo kaniambia jana twende huko coco beach panaitwa wavuvi camp.
Sasa nisije kupata tena maumivu ya kichwa wiki nzima.
 
Kama wanaume hawajaja kulalamika hapa, hizo zitabaki kuwa ishu za wanawake kwenye mambo yao ya kuoneana wivu kwa wanaume, hii inatokea hata kwenye baa na migahawa ya huku uswahilini.......ukienda na demu wahudumu wa kike huwa wanajizungusha sana kutoa huduma, tofauti na kama umeenda peke yako au mpo njemba watupu.​
 
Hapa Cape town fish market si ndio pale pembeni ya jengo la vipepeo mwewe hausi.
 
Nimezungumzia Bambalaga bar & grill.
i don't see you mentioning bambalaga in your previous post.[emoji1370][emoji1370][emoji1370][emoji1370]
Sehemu ya Starehe watu wanakuja kutumia pesa sio kuonyeshana mavazi, tembea upanue maarifa
i insist, if you go out for a party or any enjoyment gathering, please dress well and look smart per organizers description. otherwise you will be embarrassed then kicked out like a dog.
 
Sasa wapendwa, watu wamelalamika kubaguliwa mmeshawapa title ya udangaji, mnajuaje wanadanga ikiwa hamjawahi kuwaona wanadanga? Tuache tabia ya kulaumu victims.

Kuna namna ya kuwaondoa wateja ambao hauwahitaji kwenye biashara yako hasa kwa kutumia policy mbalimbali ikiwepo over pricing. Ikiwa umeweka soda elfu 4 na kuna mtu akapita hapo akakaa akanunua soda labda akimsubiri mwenzie aje, Inakuwaje afanyiwe harassment ilihali ameweza kuafford mnachouza?

Sijawahi kukutana na hiyo hali lakini nadhani kubaguliwa ni feeling mbaya sana.
 
Kuna wanawake tunaafford kula na kunywa kwa pesa zetu, na wala hatuna uchoyo ukipata huduma nzuri unamtip mhudumu kuappreciate au kumtia moyo aendelee kutoa huduma namna hiyo.

Je nikienda sehemu sijulikani, ni haki kubaguliwa sababu mhudumu hajui nitampa tip au sitampa? Hiki kitu mnakiangalia kwa wepesi sana.

Wanawake hatupati shida tukienda sehemu na wanaume zetu, kimbembe uende mwenyewe au na mashost. Watoa huduma mbadilike si kila mtu mdangaji. Najaribu tu kuvaa viatu vya wanawake wenzangu.
 
Tatizo wanaharibiwa na wale wanao enda kudanga ...

Sasa wahudumu wanaona kila dem akiwa alone basi anadanga.
Poleni sana
 
Huku kwetu wali nazi 100 ukifika unakutana na tabasamu la Odo Mammi, hujakaa sawa unafuatwa na Chonge mrembo mweupe, hapo Saumu Mashauzi anakukonyeza kwa kukuminyia jicho, Miza nae anakuegemea bega anakuuliza utakula samaki wa kupwaza na maharage ya kukata au samaki makange Maarufu kama Samaki Makange Nuksi..... unaulizwa utakula na wali wa nazi ngapi 3, 6, 9 kbl hujajibu Mama mkubwa anajibu huyo anakulaga wali wa nazi 3, mwingine anadaki mchicha je unataka wa kuloweka kwa tui au wakulowekwa kwa maji ya madafu...
Njooni huku kwetu barabara ya 17 ali maarufu kwa jina la wali nazi 100 hutalalamika, unahudumiwa hadi unahisi kabisa unamlipa pesa pungufu. Mbarikiwe nyie kina mama hapo Barabara ya 17, nazunguzia Tanga hiyo wazeee, njooni!!!
 
Muhudumu afanye kazi yake kwa kuzingatia maadili ya kazi yake na matakwa ya mteja,ikiwa muhudumu anatoa huduma nzuri kisa kuna tips au kutoa huduma mbaya kisa hakuna tips basi eneo hilo lina tatizo kubwa sana la kiuendeshaji,mmiliki ndio anawajibika zaidi kuwapa motisha wafanyakazi wake kuliko wateja kutoa tips,

Tips ni uamuzi wa mteja kama karidhishwa na huduma,sasa umepewa huduma mbovu hiyo tips unatoa kwa misingi ipi? kufurahia kubaguliwa au kutokuthaminiwa?
 
Baa kibao tu unafukuzwa na mabaunsa hata kabla ya mmiliki/meneja kwa uvaaji wako tu mbovu wanaweza pata hisia wewe ni kibaka. Hilo nimeshudia kwa macho mara kibao
 
Ni wajinga kwakweli....na utakuta hawana hela kama Evelyn hapa, glass moja ya juice masaa matatu ni kunywa kulamba yani....hebu waishie huko

Uzuri ni kwamba viwanja dar nzima ni vingi na ni vizuri unahama tuu bila kusumbuana na mtu..atashangaa hakuoni...kwanza mimi sina tabia ya kwenda sehemu hadi watu wanakuzoea........

Mtu soda moja hadi mpira unakwisha!
 
Kiwanja cha wajanja kwa sasa ni Dar es salaam Johari Rotana,(a 5 star hotel)
Pananoga pale asikwambie mtu esp Fridays...ila tu uwahi 8th floor swimming pool by 6-7 uwe umekalia seat otherwise utakaa bar ndani..maana ni fire

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Pesa tu ndio ishu kubwa, ngozi nyeusi zinaonekana zimejaa shida hata kama ukiwa na pesa, bora hata sijawahi enda huko maana unaweza piga mtu kwa hasira yakawa mengine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…