Watu wabishi sana. Nendeni Ziwa Rukwa mkawaulize wavuvi wanavua vipi samaki kwenye ziwa chafu,maji mazito lenye mamba wengi kuliko samaki.
Waulizeni wavuvi wanatega vipi nyavu zao chini ya maji na wanaonaje?
Inazama boti ziwa Rukwa wasela wanaenda kuchukua injini yao Yamaha enduro wanakuja nayo juu wanafunga boti nyingine.
Hapo wami baada ya kumtoa suka ilionekana hamna namna na mama akajikatia tamaa kusepa zake dar.
Maza aliposepa zake dar ndipo alipofanya makosa ya kiufundi. Wanaosema walilinda "utalindaje kitu mwenye nacho amekikatia tamaa".
Kosa kubwa ilikuwa ni kuweka wazi kwamba imeshindikana na mama akasepa zake dar,ikatoa mwanya kwa wajuba kufanya yao si mwenyewe kasanda.
Baada ya hapo wanyamwezi walifanya yao,badae sana ndio baadae CDF akatuma mabakamabaka wake wakaenda wakakuta kifuu,nazi washasepa nayo wenye maarifa yao.
Hao wajeda sio walienda mikono mitupu walienda na vifaa na ni wanamaji. Hicho walichokikuta ndio uhalisia na wanajua wamevunga tuu.