Mwizukulu mgikuru
JF-Expert Member
- Oct 21, 2021
- 5,715
- 13,739
Sio vizuri kumchomesha mwenzio....jamii forum ni dude kuuuubwa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Itakuwa hivyo tuInawezekana aisee maana yule Mwanamke alivyokuwa anaangaliana na yule Dereva halafu Dereva alikuwa anatumia Kishikwambi akampa yule Mwanamke , Yeye ndio akaja kunywa Soda na Egg Chop
Alikuwa anaogopa kuchapwa makofi , wabongo wamezoea umbea umbea tu.Ulishindwa nini kumhoji haya yote mkuu au ndio wanaume wa Dar mmejaa uoga uoga tu mnakuja kulia mitandaoni.
hata picha UKAOGOPA kupiga masikini[emoji28][emoji28][emoji28]
Kama upo Dar pitia maeneo ya Kimara Temboni upande wa kuelekea Mbezi, Ukishuka pale ifuate barabara ile kama 300 mita kuna Mgahawa utauona pale ni mzuri kiasi chake na unatengeneza vyakula vizuri tu. Pita pale mida ya saa 2:30 asubuhi unaweza ukaliona hilo gari la Mwendokasi linavyopaki pale bila abiria na ataingia Mwanamke na Dereva atashuka kwenye gari kunywa soda zaidi ya nusu saa, na ile njia kuna kama kona lile basi la Mwendokasi ni lile refu kabisa linasababisha foleni sana.Duu, anaziba njia kwa kwenda kuosha na libasi la mwendokasi?!
Duu.., huyo harudii tena, si unajua JF tena 😂😂Kama upo Dar pitia maeneo ya Kimara Temboni upande wa kuelekea Mbezi, Ukishuka pale ifuate barabara ile kama 300 mita kuna Mgahawa utauona pale ni mzuri kiasi chake na unatengeneza vyakula vizuri tu. Pita pale mida ya saa 2:30 asubuhi unaweza ukaliona hilo gari la Mwendokasi linavyopaki pale bila abiria na ataingia Mwanamke na Dereva atashuka kwenye gari kunywa soda zaidi ya nusu saa, na ile njia kuna kama kona lile basi la Mwendokasi ni lile refu kabisa linasababisha foleni sana.
Kuna siku nilishawahi kuuliza kwanini askari huwa wanaendesha magari ya mwendokasi wakati kuna watu(raia) hawana kazi na wanazo leseni tena za NIT?Wakuu!
Jana asubuhi nilikuwa maeneo ya Kimara Temboni Upande wa kuelekea Mbezi huwa zinapaki Bajaji pamoja na Bodaboda kwa wingi, Kwa ndani kidogo kuna round about halafu kuna Mgahawa, nilienda kujipatia kifungua kinywa. Baada ya muda mfupi lilikuja basi la Mwendokasi lenye namba T 557 DWR halina abiria hata mmoja yupo dereva tu akashuka mule kwenye basi baada ya kulipaki.
Yaani alilipaki kwenye Kona na akauziba mpaka ule Mgahawa, aliposhuka kuna Jamaa akasema huyu naye kila Siku na huwa anamfuata Mwanamke na kweli baada ya kama dk 10 hivi akaja Mwanamke wakasallimia kwa kukumbatiana na alikuwa na Kishikwambi akampa yule Mwanamke , Yeye akaenda kwenye friji akachukua Pepsi baridi na Egg Chop akawa anakula , huko kwenye kona ikaanza foleni na yule Mwanamke aliyemfuata yupo kwenye gari kakaa. Na dereva alitumia karibu dakika 25 pale kwenye Mgahawa , anazunguzunguka anapiga porojo tu na wale Wafanyakazi wa ule Mgahawa.
Maswali yangu.
1. Huyu Dereva ni nani? Mbona anafanya vitu ambavyo kama Dereva anayeendesha usafiri wa abiria hasitahili kufanya?
2. Na yule Mwanamke aliyemfuata ni nani? Maana inasemekana mara nyingi sana huwa anaenda kumfuata pale?
3. Kwanini huyu Dereva analitoa basi la Mwendokasi na kulipeleka kwenye Barabara ambayo sio njia yake ? karibu 300 mita kutoka Morogoro road njia ya kuu na njia ya mwendokasi.
4. Kuna sheria gani inayomlinda huyu Dereva maana Sheria zilizopo kazivunja kwa makusudi
5. Je huyu ndio wale Wazee wa unanijua Mi nani?
6. Au ni ndugu wa Kigogo Mkubwa Serikalini?
Naomba Wahusika mlifuatilie pale Kimara Temboni, Upande wa kuelekea Mbezi unaingia ndani kidogo kuna round about na Mgahawamjaribu kupata maelezo ya kutosha. Anachokifanya huyo dereva sio sahihi kabisa.
Nawasilisha