Randy orton
JF-Expert Member
- Apr 29, 2019
- 1,338
- 3,561
Hawa majamaa wana matatizo sana.Aliyoyapitia hayatupi sisi uhalali wa kum'judge..
Kila mtu ana mapito yake...tunaanguka ila Neema ya Mungu inatunyanyua tena....
Kwanza umeshausikiliza au kuuona wimbo wake wa 'Simba'? She is back like nothing happened.
Ni muhimu sana kupima kazi ya mtu, huduma na ushuhuda. Hakuna mahali pataweza kudumu bila kusimamia misingi.Albam ya Jipange sawasawa kuna ule wimbo Amina hatari....Mtoa mada wewe ni nan mpaka uanze kuwahesabia watu dhambi kwamba unasema Rose mhando sio mcha Mungu
Sent using Jamii Forums mobile app
Faustine Munishi...huyu anaimba real gospelVigezo vilivyotumika:
1. Nyimbo zinazoendana na neno la Mungu
2. Kuwepo kwenye imani thabiti ndani ya Kristo
3. Kuwa na malezi ya kiroho na kanisa analohudhuria kama mshirika
4. Muendelezo wa ukuaji wa huduma, ujuzi na ubora wa kazi.
Kumbuka, hatulinganishi karama bali namna karama ilivyotumiwa kwa ustadi.
Twende pamoja sasa:
1. Abihudi Misholi
2. Fanuel Sedekia
3. Christina Shusho
4. Ambwene Mwasongwe
5. John Lisu
6. Paul Clement
7. Joel Lwaga
8. Upendo Nkone
9. Martha Mwaipaja
10. Ipyana Kibona
Ambao hawakuingia lakini ni wazuri pia hawa hapa:
Christopher Mwahangila, Ephraim Mwansasu, Beatrice Mwaipaja, Walter Chilambo, Paul Mwangosi, Boaz Danken, Safari Paul, Upendo Kilahiro, Jennifer Mgendi, Edson Mwasabwite, Gwamaka Mwakalinga, Beatrice Muhone, Faustin Munishi, Rehema Simfukwe
Kuna wale maarufu sana ambao hawakuingia kwa kushindwa kukidhi baadhi ya vigezo hapo juu kama Rose Muhando, Bahati Bukuku, Bonny Mwaitege, Goodluck Gozbert, Angel Benard, Flora Mbasha, Neema Mwaipopo
ndio tunashangaa hapa.Albam ya Jipange sawasawa kuna ule wimbo Amina hatari....Mtoa mada wewe ni nan mpaka uanze kuwahesabia watu dhambi kwamba unasema Rose mhando sio mcha Mungu
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa vigezo hivi unavyotaja lazima aongoze yeye. Hakuna wa kukupinga. Hapa tumewapima kwa vigezo tajwa hapo juu.Hakuna anayekuwa namba moja miaka yote.
Legacy ya Rose Mhando Afrika Mashariki na kati inajulikana.
Labda umshindanishe na kwaya, ila mtu mmoja mmoja utakuwa unawaonea tu.
Rose Mhando ndiye msanii pekee ambaye nyimbo zake ziliwafunika hata Bongo Fleva kwenye mauzo ya caller tunes, enzi hizo Diamond na nyimbo yake ya mbagala anapigwa chini kimauzo na nyimbo ya 'utamu wa yesu' .
Kama ni kweli hawajui waimbaji hawa,bandiko lake linakosa uhalali.Braza ww ni mfatiliaji wa nyimbo za injili wa miaka ganii humjui Jangalasoni.....
Umewahii kusikiliza hizi nyimbo hizi chini...
1. Wachungaji tuelezeni ukweli
2. Usimuige mbuzi
3. Undugu siku ya msiba
4. Usaliti wa ndoa
5. Okoka kiukweli
6. Jikongoje
7. Taifa Teule
8. Malaya wameoza
9. Mbiguni sio Mochwari
10. Amezaliwa Yesu
11. Wokovu ni Safari
12. Dungwa Sindano
13. Vaa viatu
Huyu mwamba anaimba Gospal Katuni ujumbe unafikaa hakuna kupamba pamba watu...
Usimuige Mbuzi ndo Kiboko, huyu ni veterani wa Gospal enzi za kijitonyama kwaya, Kwa viumbe vyote, lulu, Sauti Ikatoka
Kuna yule Mchungaji kwa sasa marehem Ephrahim Mwansasu aliimba nyimbo kama Kutesa kwa Zamu, Nikimaliza kazi, Kifo na nyingine Nyingii....
Inashangaza kusema huwajuii....
Sent using Jamii Forums mobile app
Umesoma vigezo pale juu? Unaweza kuleta list nyingine kwa vigezo vingine mkuu. Wala hakuna kulazimisha chochote.Haujistulkii kila mtu anamtaja Rose.
Mnyonge Mnyongeni , ila hakuna wa kushindana nae hapo.
Nimeitafuta Sana album yake ya usiwe kama popo iliyo katika mfumo wa CD, Kwa bahati mbaya niliikosa, Nilikuwa nayo cassette yakeUnamfahamu Charles Jangalasoni wewe jamaa anapita mle mle kama Abiudi
Kwa kufuata vigezo vilivyotumika hapo juu anazidiwa kwa mbali.Bahati anazidiwa na Martha? Sio kweli
Hujawahi msikia labda kwa sababu ya umri wako,kuna waimbaji wengi wazuri,Jangalason,Mzungu four japo kwa sasa nafikiri yuko busy na kuchunga zaidi...huyu mzungu 4 miaka ya 90 mwishoni nyimbo zake ilikua lazima ufufuke kiroho.Sijawahi kumsikia.. ajitahidi sasa na neema ya Mungu imsaidie afikie viwango vya kitaifa.
Vigezo ulivyoweka hapo juu vinatakiwa vitumiwe na Mungu sio wewe mwanadamu.Kwa vigezo hivi unavyotaja lazima aongoze yeye. Hakuna wa kukupinga. Hapa tumewapima kwa vigezo tajwa hapo juu.
Standard ya morality na christian ethics ipo kwenye biblia. Neno la Mungu linaturuhusu kupima mambo yote.Hawa majamaa wana matatizo sana.
Wao ni kina nani mpaka waweke standards za kupima morality ya watu.
Huku ni kujiona watakatifu
Tukizingatia vigezo tajwa hapo juu hawezi kuingia.Hakuna kama Rose Muhando finish!
Vigezo vyako ni vya kibiashara zaidi. Hapa hatuangalii hivyo.ndio tunashangaa hapa.
Album ilikuwa inaitwa 'uwe macho' , ni one of the best selling albums katika muziki wa Tanzania
Wewe humfahamu Jangalasoni...huyu ni mtumishi wa Mungu ambaye ameimba ktk upako kwa miaka mingi kabla hajaondoka nchini,kizazi cha miaka ya 80' mpk 90' +2000 mwanzon kinamjua vzrMwansasu yupo kwenye list ya pili pale maana namfahamu sana.. ila huyo Jangalason hajafikia level ya kitaifa.
Kumbuka hapa hatupimi kipawa, tunapima namna alivyoweza kukua kwenye kipawa na kugusa watu wengi nchini.
Hapa tumeangalia mwimbaji mmoja mmoja na sio vikundi. Mwansasu yupo pale kwenye list ya pili ametajwa. Huyo mwingine hajawahi kufikia viwango vya kitaifa.Kama ni kweli hawajui waimbaji hawa,bandiko lake linakosa uhalali.
Ni muhimu awafahamu kwa
kina waimbaji mashuhuri&maarufu,ili aweze kuweka fair judgement.
Sijui ilikuwaje kwamba sikuwahi kuwasikia hao miaka ile ingawa nilikuwa mfuatiliaji sana.Hujawahi msikia labda kwa sababu ya umri wako,kuna waimbaji wengi wazuri,Jangalason,Mzungu four japo kwa sasa nafikiri yuko busy na kuchunga zaidi...huyu mzungu 4 miaka ya 90 mwishoni nyimbo zake ilikua lazima ufufuke kiroho.
We mfatilie au nikutajie baadhi ya kazi zakeSijawahi kumsikia.. ajitahidi sasa na neema ya Mungu imsaidie afikie viwango vya kitaifa.
Biblia inasema mtawatambua kwa matendo yao. Sasa hapa hatuhukumu mtu yeyote maana kila mtu anakosea na kutubu.Vigezo ulivyoweka hapo juu vinatakiwa vitumiwe na Mungu sio wewe mwanadamu.
We unajuaje mtu ana imani thabiti au la ?
We umekuwa Mungu mpaka uthibitishe imani ya mwanadamu mwenzako ?