Waimbaji kumi bora wa nyimbo za injili kuwahi kutokea hapa Tanzania mpaka sasa

Waimbaji kumi bora wa nyimbo za injili kuwahi kutokea hapa Tanzania mpaka sasa

Kuna mwimbaji mmoja ametajwa hapo juu kweli ana maisha ya tabu Sana saiv...sema maisha yake ameyaweka private Sana. Hivi najiuliza mwimbaji Kama yule na kiwango Cha pesa alichokuwa anaingiza zamani wakati Yuko peak alishindwa kujenga hata nyumba? Saiv Hana hata ela ya Kodi kulipa nyumba. sitaweza mtaja...Sana Sana namwombea Mungu amvushe kwa anayopitia

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Pole nyingi sana kwake. Pengine alijisahau enzi hizo. Mungu amrehemu na kumfungulia mlango apate kufanikiwa.
 
Alitumia mafuta mara moja tena kwa tukio maalumu na sio KILA siku kwa muendelezo. Alisema tuponje kwa jina lake na sio kwa hivyo visaidizi vyenye lengo kuu ni kumfifisha Yesu Kristo watu waache kutumainia jina lake bali hizo hirizi. Mtu mdhambi ujui kuomba hivyo vi mafuta vitafaa nini kwako uoni ni lengo la kuwaibia vipofu wa maandiko tu.
Kama Yesu na baadae mitume walitumia kwanini wewe uone tatizo wakristo wa leo wakiyatumia?
 
List imekaa poa vibaya mno, ila kuna ambao hawakutakiwa kuwepo kabisa kama joel lwaga, paul clement, Goodluck nk, kama kuna vigezo ulitumia ili kuwaondoa kina rose muhando basi na hawa ulitakiwa uwatoe kabisa.
 
List imekaa poa vibaya mno, ila kuna ambao hawakutakiwa kuwepo kabisa kama joel lwaga, paul clement, Goodluck nk, kama kuna vigezo ulitumia ili kuwaondoa kina rose muhando basi na hawa ulitakiwa uwatoe kabisa.
Asante mkuu.

Vigezo vipi vilivyotajwa hapo vitawaondoa Lwaga na Clement?
 
Kuachika kwenye ndoa ni jambo pana sana pengine linahitaji mjadala wake. Hata suala la kuoa/kuolewa upya nalo ni pana na lina theological perspectives nyingi hivyo tusiende sana huko.

Kifupi biblia imeruhusu kutengana na ukifanya hivyo ukae kwa kutulia. Na imeruhusu kumwacha yule anayeenda nje ya ndoa. Huyo ukitengana naye unaweza kuoa tena.

Msingi wa kanisa kukataa watu kuacha na kuoa upya upo zaidi kwenye kuelewa maana ya msamaha. Kwamba kama Mungu anatusamehe kila aina ya dhambi (of course isipokuwa kumkufuru Roho Mtakatifu) ni kwanini sisi nasi tusisamehe watu aina zote za dhambi?
Mkuu Biblia ipi imeruhusu wanaoachana wana weza oana tena?Math 19:9,imesema anayeacha na kuachwa akioa au kuolewa azini.
 
Katika ujumla wake ninaona maisha yao yanamhubiri Kristo. Hakuna jambo lolote la wazi ambalo linafahamika kiasi kwamba waweze kuhesabika kuwa hawafuati maadili ya kikristo.

Mkuu concept ya kuwa ndani ya Kristo haijaweza kutafsiriwa vyema na matokeo yake wengi wanaona wanaume na wanawake hawawezi kushika majukumu yanayofanana katika kanisa lakini hili sio sahihi. Pengine unaweza kuuleta huo mjadala tupeane elimu na kujengana.
Sio vizuri kuwataja kwa majina,lakini fuatilia hao waimbaji baadhi uliowataja kama wako na ndoa zao za mwanzo,...Yuko mwimbaji mmoja nimemtaja hapo mkewe alimwacha na huyo mwimbaji makanisa ya kiroho yalikataa kumpa ruhusa ya kuoa...na ndio maana tunasisitiziwa kuomba ili Mungu atupe wa kufanana,lkn ukikosea kuoa au kuolewa hilo jaribu ni kubwa na inaweza kua ngumu sana kumuona Mungu...ni.Mungu tu aingilie kati kama ilivyokua kwa Ruthu.
 
Mkuu Biblia ipi imeruhusu wanaoachana wana weza oana tena?Math 19:9,imesema anayeacha na kuachwa akioa au kuolewa azini.
Huu mstari unauelewaje?

Mathayo 5:32 SRUV
lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa sababu ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.
 
Vigezo vilivyotumika:

1. Nyimbo zinazoendana na neno la Mungu
2. Kuwepo kwenye imani thabiti ndani ya Kristo
3. Kuwa na malezi ya kiroho na kanisa analohudhuria kama mshirika
4. Muendelezo wa ukuaji wa huduma, ujuzi na ubora wa kazi.

Kumbuka, hatulinganishi karama bali namna karama ilivyotumiwa kwa ustadi.

Twende pamoja sasa:

1. Abihudi Misholi
2. Fanuel Sedekia
3. Christina Shusho
4. Ambwene Mwasongwe
5. John Lisu
6. Paul Clement
7. Joel Lwaga
8. Upendo Nkone
9. Martha Mwaipaja
10. Ipyana Kibona

Ambao hawakuingia lakini ni wazuri pia hawa hapa:

Christopher Mwahangila, Ephraim Mwansasu, Beatrice Mwaipaja, Walter Chilambo, Paul Mwangosi, Boaz Danken, Safari Paul, Upendo Kilahiro, Jennifer Mgendi, Edson Mwasabwite, Gwamaka Mwakalinga, Beatrice Muhone, Faustin Munishi, Rehema Simfukwe

Kuna wale maarufu sana ambao hawakuingia kwa kushindwa kukidhi baadhi ya vigezo hapo juu kama Rose Muhando, Bahati Bukuku, Bonny Mwaitege, Goodluck Gozbert, Angel Benard, Flora Mbasha, Neema Mwaipopo
Ongeza kigezo kingine kuwa waimbaji kutoka Makanisa ya Kiprotestant, maana ukilinganisha na waimbaji wa Kanisa Katoliki kuna vichwa hatari sana kwa utunzi na uimbaji hao uliowataja wanasubiri mbali sana.

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
 
Sio vizuri kuwataja kwa majina,lakini fuatilia hao waimbaji baadhi uliowataja kama wako na ndoa zao za mwanzo,...Yuko mwimbaji mmoja nimemtaja hapo mkewe alimwacha na huyo mwimbaji makanisa ya kiroho yalikataa kumpa ruhusa ya kuoa...na ndio maana tunasisitiziwa kuomba ili Mungu atupe wa kufanana,lkn ukikosea kuoa au kuolewa hilo jaribu ni kubwa na inaweza kua ngumu sana kumuona Mungu...ni.Mungu tu aingilie kati kama ilivyokua kwa Ruthu.
Lakini biblia inaruhusu kuacha na kuoa mwingine kwenye jambo moja tu, iwapo mtu ni mzinzi. Sasa hatujui utaratibu wa hilo kanisa.

Mimi kanisani ninaposali hairuhusiwi kuacha na kuoa mwingine kwasababu yoyote ingawa mimi naona clearly biblia haijazuia endapo mtu ni mzinzi.

Na mzinzi hapa ni hasa pale mtu anaporudia hiyo tabia na wala habadiliki.
 
Ongeza kigezo kingine kuwa waimbaji kutoka Makanisa ya Kiprotestant, maana ukilinganisha na waimbaji wa Kanisa Katoliki kuna vichwa hatari sana kwa utunzi na uimbaji hao uliowataja wanasubiri mbali sana.

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
Walete hapa hao wakatoliki ili tuwafahamu na pengine wanaweza kuingia hapo kwenye list.
 
Taja pia na kwaya bora za muda wote.
Vigezo vilivyotumika:

1. Nyimbo zinazoendana na neno la Mungu
2. Kuwepo kwenye imani thabiti ndani ya Kristo
3. Kuwa na malezi ya kiroho na kanisa analohudhuria kama mshirika
4. Muendelezo wa ukuaji wa huduma, ujuzi na ubora wa kazi.

Kumbuka, hatulinganishi karama bali namna karama ilivyotumiwa kwa ustadi.

Twende pamoja sasa:

1. Abihudi Misholi
2. Fanuel Sedekia
3. Christina Shusho
4. Ambwene Mwasongwe
5. John Lisu
6. Paul Clement
7. Joel Lwaga
8. Upendo Nkone
9. Martha Mwaipaja
10. Ipyana Kibona

Ambao hawakuingia lakini ni wazuri pia hawa hapa:

Christopher Mwahangila, Ephraim Mwansasu, Beatrice Mwaipaja, Walter Chilambo, Paul Mwangosi, Boaz Danken, Safari Paul, Upendo Kilahiro, Jennifer Mgendi, Edson Mwasabwite, Gwamaka Mwakalinga, Beatrice Muhone, Faustin Munishi, Rehema Simfukwe

Kuna wale maarufu sana ambao hawakuingia kwa kushindwa kukidhi baadhi ya vigezo hapo juu kama Rose Muhando, Bahati Bukuku, Bonny Mwaitege, Goodluck Gozbert, Angel Benard, Flora Mbasha, Neema Mwaipopo
 
Huyu Fanuel Sedekia nilimjua kwa mara ya kwanza kwa kusikia nyimbo yake ikipigwa kwenye msiba wa classmate kipindi hiki tupo university.
 
Back
Top Bottom