Waimbaji wa Nyimbo za Dini za Zamani Walikuwa na Ujumbe Zaidi Kuliko Sasa

Waimbaji wa Nyimbo za Dini za Zamani Walikuwa na Ujumbe Zaidi Kuliko Sasa

Mchana unaweka albamu ya nyimbo za Tabata Mennonite Choir na usiku mkiwa mnakula unasikiliza nyimbo za Mtoni Evangelical Choir na sauti ya kipekee ya Marehemu George Njabili.
Huyu njabili ndo yule kibonge aliyeimba around the corner, jesus is coming..? Alizikwa tukuyu
 
Umenikumbusha mbali sana mkuu! Marehemu Mama Mkubwa alikuwa ni vocalist sauti ya kwanza kwenye kwaya ya Muungano Kwaya Christian Nasa Magu 😔 yaani walikuwa wanasoma biblia halafu ndo wanatengeneza wimbo kutoka humo 😊 safi sana
Ulokole (wokovu)wa zamani ulikua wokovu kweli kweli, mtu akitengwa na kanisa anaona ametengwa na Mungu na vilio juu, siku hizi ni kanyaga twende 😀😀😀😀
 
Wewe sema tu zamani walilenga zaidi injiri siku hizi ni uwanja wa majungu, vijembe na tambo na zaidi sana vibunda. Au unawaogopa Mkuu?
 
Ukweli ni kwamba tukatae ama tukubali ni kwamba wokovu unazidi kubaki mdomoni na sio rohoni so hata nyimbo zimebaki kinywani ila moyoni hazipo.

Wapi Kwaya hizi
1.Bulyankulu Barabara ya 13
2.Bulyankulu Mwenye Mamlaka
3.Nkinga Christian
4.St James Anglkana Arusha
5.Muungano Kwaya Christian Nasa Magu
6.Sauti ya Jangwani Wasabato Shinyanga
7.Kila Goti Litapigwa EAGT Singida utemini
8.KKKT Chunya Makongolosi
9.Mke Mwema Kasulu
10. Rev Mwansansu
11.Rev Charles Jangalason
12. Fanuel Sedekia
13. Upendo Kwaya Agape Moshi TAG
14.St Maris Kitimutimu chimuli Dodoma
15.Efatha Uhuru Moraviani Wimbo wao amani
16. kinondoni Kwaya TAG
EAGT Utemini Gospel Singers (UGS)Singida, KILA GOTI LITAPIGWA ilishasambaratika, waimbaji wake wengine wanaimba kwa kujitegemea kama Elineema Babu, Sarah Nkumbi ambaye pia ni daktari wa binadamu ni mtumishi wa umma, kuna Emanuel Enock yeye ni producer mwenye studio yake, waimbaji wengine walijiunga na kwaya zingine
 
Sijawahi kuwaamini au kuwatilia maanani waimbaji wa nyimbo za dini hata siku moja na sitokuja kubadilika juu ya hili
 
Back
Top Bottom