Waislam tulio wengi wetu tunamchukia nguruwe kuliko zinaa, kuliko pombe, kuliko usengenyaji n.k

Ila najiuliza, kwenye Biblia imeandikwa kwamba Yesu alimtoa mtu mapepo na yakakimbilia kwa nguruwe, wakazama wote baharini. Ukila kiti moto umekula mapepo. Wakristu tulio wengi tunaishi na mapepo kwenye damu kwa kula kiti moto.
 
Mdudu yupo hadi huko UAE.. wanajua kumtengeneza vizuri,hana shombo.. wenye dini yao wala hawana shida naye.. kuna mwarabu wa uvinza,mweusi kuliko mkaa anasikia kichefuchefu,ila anakuywa gongo, hatunzi/ hawajibiki kwa familia..ACHENI UNAFIKI WA MAISHA
 
Ila najiuliza, kwenye Biblia imeandikwa kwamba Yesu alimtoa mtu mapepo na yakakimbilia kwa nguruwe, wakazama wote baharini. Ukila kiti moto umekula mapepo. Wakristu tulio wengi tunaishi na mapepo kwenye damu kwa kula kiti moto.
Umeshasema waliingia baharini. It means walizama wote huko. Wakizama watazaliana vipi mpaka mimi wa huku namtumbo wanifikie na niwale.

Au unataka kutuambia kuwa hao nguruwe baada ya kuingia baharini waliibuka katika kila nchi duniani wakiwa na hayo mapepo na kila uzao wake unarithi mapepo.
 
Hiyo sio injili
 
Hiyo sio injili
Kwahyo Biblia Mnasoma Vitabu Vya Injili Peke Yake??
Na Injili Inasemaje Kuhusu Nguruwe?
Injili Ni Vitabu Vinne Tu kati ya Vitabu Zaidi ya 66 au 72 au 86 kwenye Biblia..
Yaani Mathayo,Marko,Luka na Yohana..
 
Magomeni wali andaman ndugu zako katika imani ya nyaazi kwenda kuvunja mabucha ya nyama ya nguruwe je huo ni upendo au chuki dhidi ya kitimoto.
Walivunja mabucha Kwahiyo mimi sijui mabucha yalikuwa na shida gani wao ndio wanajua kero zake, maana wakati mwengine labda harufu mbaya
 
Fafanua wapi kazuiwa,maandiko please

Kumbukumbu la Torati 14:7-8

7. Lakini, hawa msile katika wale wenye kucheua, na hao waliopasuliwa ukwato; ngamia, na sungura, na kwang'a, kwa kuwa hucheua, lakini hawakupasuliwa kwato, ni najisi kwenu;
8 na nguruwe, kwa kuwa amepasuliwa ukwato lakini hacheui, huyu ni najisi kwenu msile nyama zao, wala mizoga yao msiiguse.
 
Usitusingizie ubaya ...wataka tumpende vip ? Huyo mbuzi na kuku tunawala ila hatukai nao nyumba Moja wao wanakaa bandani
 
Uko sahihi sana mkuu
Kongole
 
Kwanini wagalatia waislamu kutokula nguruwe kuna wauma saana?
Hata hawawawazii ila wanashangazwa na mnavyoforce kila mtu asile! Nguruwe aliwafanya nini kiasi kwamba awe chukizo zaidi ya pombe, ufiraji, zinaa, wizi n.k? Kiumbe aliyeumbwa na Mungu anakuwaje haramu? Mmekatazwa kula nyama nyingi tu lakini sijawahi kuona chuki zenu kwa wanyama wemgine mliokatazwa isipokuwa kwa kitimoto tu! Nahisi chuki zenu ni kwa wanaokula kitimoto (Wakristo) na si kwa kitimoto mwenyewe.
 
Kenge ni halali? Vipi kuhusu Mbwa, Paka, Nyoka na sungura? Mbona chuki ni kwa kitimoto tu!? Kuna jambo la ziada nje ya huo uharamu mnaohubiri.
 
Kwani Nguruwe kiumbe cha Mungu kakiumba,nyie waislamu hiki kiumbe kimewakosea nini hasa?
 
Haya ni maagizo ya agano la kale,Agano jipya kila kiumbe kimetakaswa kinafaa kwa matumizi ya Binadamu
 
Amekatazwa Sungura na viumbe wengine kibao mbona huwazungumzii hao? Kwa wengine Ngamia ni haramu ila nyie mnakula lkn hawamsemi vibaya wala kuomesha chuki kwa ngamia! Hizo chuki kwa nguruwe mbona hamuoneshi kwa paka, mbwa na sungura? Au wao mmeruhusiwa kula?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…