Waislam tunakuomba Rais Samia umshauri mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Petro Magoti aache kebehi dhidi ya Waislam

Waislam tunakuomba Rais Samia umshauri mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Petro Magoti aache kebehi dhidi ya Waislam

Mleta hoja punguza MUNKARI, alichofanya Mh DC yupo sahihi..ungepitia taratibu na sheria za kuanzisha kituo/shule,sheria ya Mtoto na haki za Mtoto za UN bila kusahau Sheria ya Afya ta Jamii ya mwaka 2009 ungemuelewa DC

Kuwa na nia nzuri sio sababu ya kuvunja sheria na taratibu za nchi
 
Shada uslam umejificha na mambo mengi ya sirini, ulawiti na zinaa zimetawala sana, mzazi mwenye akili sawa sawa hawezi ruhusu mtoto wake kwenye hayo mazingira
 
Amani iwe nanyi.

Hivi karibuni Mkuu wa wilaya ya Kisarawe ameonekana akizua taharuki na sintofahamu kwa waislam wa wilaya ya kisarawe na Tanzania kwa ujumla baada ya kuvamia msikiti huko Kiluvya na kufungia kituo cha kuhifadhisha Quran. Huku akiamuru kuwa wanafunzi warudi makwao na kuita kitendo cha wanafunzi wa kiislam kukusanyika na kuisoma dini yao ni udhalilishaji.

Hii tunaita ni chokochoko dhidi ya Uislam na waislam .Jamii ambayo kwa miaka mingi imekuwa ikijenga amani na maadili mema katika nchi hii. Masuala ya Imani sio masuala ya kuyafanyia mzaha kwa kuwa yanagusa mioyo ya watu wengi na ni rahisi sana kuivuruga amani endapo atatokea mtu akaichezea ama kuidhihaki dini ya watu fulani.

Watanzania tumelelewa katika misingi ya amani,upendo,umoja na mshikamano. Ndio mizizi iliyoasisiwa na wapigania uhuru wa nchi hii na tumeweza kudumu katika misingi hiyo kwa miongo kadhaa sasa.

Anapotokea mtu awe kiongozi ama yoyote yule akafanya dhihaka ,kukashifu ,kubeza na kuingilia imani za dini fulani basi bila ya shaka anapaswa kukemewa kwa nguvu zote.

Serikali ya Rais Mama Samia ni serikali sikivu na weledi inayosimamia misingi iliyowekwa na waasisi wa Taifa hili. Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe hakupaswa kuzua taharuki kwenye vyombo vya habari kwa kufanya ziara ya kushtukiza Usiku wa manane msikitini ,ambayo waislam wameitafsiri kama uvamizi dhidi ya msikiti huko kisarawe na kuamuru kituo cha kuhifadhisha Quran kifungiwe huku akiita kuwa ni udhalilishaji.

Na pia akidai kuwa misikiti ni sehemu ya watu kuswali na kuondoka tu huku akitumia kauli za kebehi na dharau kuwa watoto wanalala kama nyanya ,wamepangwa kama tofali za block, hata nguruwe hawezi kulala katika mazingira hayo.Mara aseme watoto hao walipaswa wachapwe viboko wote na wazazi wao wawekwe gerezani kwa kuwa wameshindwa kuwalea! Hizi ni dharau kwa wazazi wa kiislam! Mzazi anayempeleka mwanae kuisoma dini yake ili awe na maadili mema katika jamii yake aonekane ameshindwa kumlea mwanae!

Leo hii mkuu mpya wa Wilaya ya kisarawe aje kuwafundisha waislam tafsiri na kazi ya msikiti.Ni jambo la ajabu na aibu sana.

Waislam nchini Tanzania wana taasisi yao ya BAKWATA, ambayo inashirikiana na taasisi nyingine ndogondogo kusimamia masuala ya waislam kwa ujumla. Petro Magoti alishindwa nini kuongea na uongozi wa BAKWATA unaoongozwa na Mufti Abubakar bin Zuber kuwa waboreshe kituo hicho cha msikiti wa kiluvya ili kuweka mazingira rafiki ya vijana wa kiislam kuisoma dini yao na jambo hilo lisifike kwenye mitandao na kuzua sintofahamu kama alivyofanya yeye?

Msimamizi wa kituo cha msikiti wa Kiluvya alionekana akimueleza Mkuu huyo wa wilaya kuwa wanafunzi wanaishi katika hali hiyo kwa dharura tu huku jitihada mbalimbali za kuanzisha ujenzi wa mabweni zikiendelea.Nondo,mchanga,cement na matofali tayari vimeshakusanywa na jitihada za kuomba vibali vya ujenzi zikiendelea kufanyika ili kuhakikisha wanafunzi wanaishi katika mazingira rafiki

Wito wangu kwa Rais ni kuhakikisha kuwa wateule wake kama Petro Magoti hawaingilii masuala ya kidini moja kwa moja kwasababu ni eneo nyeti linaloweza kuvunja amani ya hii nchi kwa haraka sana. Awashauri wateule wake wawe na busara katika masuala ya utawala.

Alilofanya Petro Magoti ni kutafuta "kiki" tu, na kuleta kebehi na kudhalilisha waislam na uislam kwa ujumla. Jambo la hatari sana.

Video ya sheikh akitoa mapendekezo kwa serikali nini kilipaswa kufanyika.


Pia soma:Kisarawe: DC Petro Magoti ameutaka Msikiti unaotoa elimu ya dini kwa watoto 96, kuwarudisha walipowatoa sababu ya Mazingira Mabovu ya malazi
Tatizo lenu mnakuwa wajinga wajinga sana, mpaka madhara yatokee ndipo muanze kusikitika

Kwanini msiweke mazingira sawa kwanza kisha ndio mengine yafuatie??

Ni sehemu ngapi hapa Tanzania wanatoa mafunzo kama hayo na hawajabughudhiwa iweje hapo tu? Basi ndio ujue mazingira sio rafiki huwezi kusunda vijana hao wote kisa masomo ambayo unaweza kukamilisha na kisha kuwaita tena uwape mafunzo


Wajifunze kwa wengine ambao wameweka mazingira sawa kwanza
 
Dhihaka na dharau alizozifanya je!?..
Kufanya vamizi za usiku na vyombo vya habari ni sahihi?

Alishindwa nini kuita viongozi wa msikiti na taasisi ya BAKWATA walimalize jambo hili bila ya kuzua taharuki? Huoni kama ni tukio linaloweza kuamsha hisia za waislam?
Hakuna taharuki yoyote iliyotokea, acheni kukuza Mambo bwana
 
Mwamposa aliua watu moshi uliona akifungiwa huduma?
Mkutano wa Mwamposa ulikuwa na kibali cha Polisi! Vipi hiyo Madrasa ya kurundika watoto wa miaka 3 kwenye mazingira hatarishi tena bila kibali cha serikali ni sawa?
 
We kweli mkono nusu...au anaandikia miguu?? Mazingira kwa watoto ni mabaya sote tumeona...sasa unatetea nini? Tunajenga Taifa gani la Kesho? Ni upuuz mtupu mnafanya...yaan tokea uhuru mmejenga shule ngapi? Vyuo vingapi? Zaidi ya kuwachanganya watoto? Viongozi wangapi Tz wamesoma shule na vyuo vya mission japokuwa ni muslims?....hebu tafakari tena..
 
Amani iwe nanyi.

Hivi karibuni Mkuu wa wilaya ya Kisarawe ameonekana akizua taharuki na sintofahamu kwa waislam wa wilaya ya kisarawe na Tanzania kwa ujumla baada ya kuvamia msikiti huko Kiluvya na kufungia kituo cha kuhifadhisha Quran. Huku akiamuru kuwa wanafunzi warudi makwao na kuita kitendo cha wanafunzi wa kiislam kukusanyika na kuisoma dini yao ni udhalilishaji.

Hii tunaita ni chokochoko dhidi ya Uislam na waislam .Jamii ambayo kwa miaka mingi imekuwa ikijenga amani na maadili mema katika nchi hii. Masuala ya Imani sio masuala ya kuyafanyia mzaha kwa kuwa yanagusa mioyo ya watu wengi na ni rahisi sana kuivuruga amani endapo atatokea mtu akaichezea ama kuidhihaki dini ya watu fulani.

Watanzania tumelelewa katika misingi ya amani,upendo,umoja na mshikamano. Ndio mizizi iliyoasisiwa na wapigania uhuru wa nchi hii na tumeweza kudumu katika misingi hiyo kwa miongo kadhaa sasa.

Anapotokea mtu awe kiongozi ama yoyote yule akafanya dhihaka ,kukashifu ,kubeza na kuingilia imani za dini fulani basi bila ya shaka anapaswa kukemewa kwa nguvu zote.

Serikali ya Rais Mama Samia ni serikali sikivu na weledi inayosimamia misingi iliyowekwa na waasisi wa Taifa hili. Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe hakupaswa kuzua taharuki kwenye vyombo vya habari kwa kufanya ziara ya kushtukiza Usiku wa manane msikitini ,ambayo waislam wameitafsiri kama uvamizi dhidi ya msikiti huko kisarawe na kuamuru kituo cha kuhifadhisha Quran kifungiwe huku akiita kuwa ni udhalilishaji.

Na pia akidai kuwa misikiti ni sehemu ya watu kuswali na kuondoka tu huku akitumia kauli za kebehi na dharau kuwa watoto wanalala kama nyanya ,wamepangwa kama tofali za block, hata nguruwe hawezi kulala katika mazingira hayo.Mara aseme watoto hao walipaswa wachapwe viboko wote na wazazi wao wawekwe gerezani kwa kuwa wameshindwa kuwalea! Hizi ni dharau kwa wazazi wa kiislam! Mzazi anayempeleka mwanae kuisoma dini yake ili awe na maadili mema katika jamii yake aonekane ameshindwa kumlea mwanae!

Leo hii mkuu mpya wa Wilaya ya kisarawe aje kuwafundisha waislam tafsiri na kazi ya msikiti.Ni jambo la ajabu na aibu sana.

Waislam nchini Tanzania wana taasisi yao ya BAKWATA, ambayo inashirikiana na taasisi nyingine ndogondogo kusimamia masuala ya waislam kwa ujumla. Petro Magoti alishindwa nini kuongea na uongozi wa BAKWATA unaoongozwa na Mufti Abubakar bin Zuber kuwa waboreshe kituo hicho cha msikiti wa kiluvya ili kuweka mazingira rafiki ya vijana wa kiislam kuisoma dini yao na jambo hilo lisifike kwenye mitandao na kuzua sintofahamu kama alivyofanya yeye?

Msimamizi wa kituo cha msikiti wa Kiluvya alionekana akimueleza Mkuu huyo wa wilaya kuwa wanafunzi wanaishi katika hali hiyo kwa dharura tu huku jitihada mbalimbali za kuanzisha ujenzi wa mabweni zikiendelea.Nondo,mchanga,cement na matofali tayari vimeshakusanywa na jitihada za kuomba vibali vya ujenzi zikiendelea kufanyika ili kuhakikisha wanafunzi wanaishi katika mazingira rafiki

Wito wangu kwa Rais ni kuhakikisha kuwa wateule wake kama Petro Magoti hawaingilii masuala ya kidini moja kwa moja kwasababu ni eneo nyeti linaloweza kuvunja amani ya hii nchi kwa haraka sana. Awashauri wateule wake wawe na busara katika masuala ya utawala.

Alilofanya Petro Magoti ni kutafuta "kiki" tu, na kuleta kebehi na kudhalilisha waislam na uislam kwa ujumla. Jambo la hatari sana.

Video ya sheikh akitoa mapendekezo kwa serikali nini kilipaswa kufanyika.


Pia soma:Kisarawe: DC Petro Magoti ameutaka Msikiti unaotoa elimu ya dini kwa watoto 96, kuwarudisha walipowatoa sababu ya Mazingira Mabovu ya malazi
Mbona baadhinya waislamu huwa mnakomalia ujinga sana?Hapo kosa la DC lipo wapi
 
Watangulizi wa Petro Magoti mbona hawakuleta taharuki hizi.

Wamepita ma DC, Mh Jokate mwegelo na Nikki wa pili wameishi vizuri tu na wana kisarawe ila yeye toka aje kisarawe amekuwa ni mtu wa kuzua taharuki.

Kwanza kaanza kwa kutoa matamko kuwa mabinti wa kizaramo wasichezwe, pikipiki zisitumike kubeba mkaa pikipiki ikikamatwa anaitaifisha , hajakaa vizuri kaja na haya
Huenda hawakuwa na taarifa!
 
Lete ushahidi wa mtoto wa miaka 3 aliyekutwa hapo msikitini.
Mimi sio DC, TISS, Polisi, wala Mkazi wa kisarawe...nikuletee aushahidi kama nani kutoka wapi?

Wewe umeweka Ushahidi kuwa wale wote sio watoto na wamezidi miaka 18 ili wajitegemee?

Jibu kinagaubaga
 
Waislamu ni watu washari shari sana, yaani muda wote wamekaa kwa kujitega ukimgusa hata kwa bahati mbaya analipukaaaa!!

Kila kitu kipo wazi tumeona na kusikia pia,hata chizi atakwambia mazingira Yale sio rafiki kbs kwa watoto wadogo, huwezi kukusanya watoto wadogo na ukawaweka ktk mazingira ya vile.

Sasa naanza kuwa na mashaka pengine kweli Kuna kitu hakikuwa sawa.
 
Watangulizi wa Petro Magoti mbona hawakuleta taharuki hizi.

Wamepita ma DC, Mh Jokate mwegelo na Nikki wa pili wameishi vizuri tu na wana kisarawe ila yeye toka aje kisarawe amekuwa ni mtu wa kuzua taharuki.

Kwanza kaanza kwa kutoa matamko kuwa mabinti wa kizaramo wasichezwe, pikipiki zisitumike kubeba mkaa pikipiki ikikamatwa anaitaifisha , hajakaa vizuri kaja na haya
Kwahiyo kufichua uchafu na madhaifu katika Wilaya ndio kunamfanya kuwa anaishi na watu vizuri?

Je kama hao waliopita walikuwa wanajua hayo lakini wakaacha ili kujipendekeza kwa Wananchi?

Kiongozi mzuri ni yule asiyetaka sifa kwa kumridhisha kila Mtu, mfano mzuri ni J.P.Magufuli
 
Mkuu wa wilaya ya kinondoni nae aende kwa mwamposa akaufunge uwanja wa Tanganyika packers pale kawe kwasababu analaza maelffu ya wananchi wa Tanzania nje wakiwemo watoto wadogo.
Tatizo Jambo la Mkuu wa Wilaya unataka kulifanya la Kidini.
 
Back
Top Bottom