Waislam tunapaswa kuondokana na upofu wa dini la sivyo tutaonekana wote hatuna akili

Waislam tunapaswa kuondokana na upofu wa dini la sivyo tutaonekana wote hatuna akili

Uko sahihi. Masheikh wapo kwenye majibizano ya kushindana, wakati maaskofu wanaweka mbele mustakbali wa Taiifa zima ndiyo maana huoni maaskofu wakiandika neno "sheikh", "uislamu", "waislamu" katika waraka wao.

Hao DP World wametimuliwa Djibouti nchi ya asilimia 98 waislamu tupu sembuse hapa kwetu!

Ishu hapa ni mkataba mbovu, siyo habari za uislamu wala Ukiristo

Mbona waislamu wa Uturuki wanajenga SGR maaskofu hawajatoa waraka?
Mbona Waislamu wa Misri wanajenga bwawa la Stieglers maaskofu hawajatoa waraka?

Qur'an inasema simamia haki na sema ukweli hata kama ukweli unakutandika wewe mwenyewe!

Usiposimamia haki na ukweli utaonekana kituko tu, bali yule asimamiaye ukweli atapata heshima!

Na ukweli haujalishi kausema paroko, askofu au imamu na sheikh!

Kwenye hili la bandari, maaskofu wapo katika ukweli na haki!
Wew umeleta hoja Kali baada ya mleta hoja wee Ni nambari mbili uko vzr ubarikiwe [emoji120]
 
Hawajifunzi tu, Waislamu walimpigania Kikwete, Muislamu mwenzao kwenye uchaguzi wa mwaka 2010, akaishia kuwalipa kwa kuwasweka ndani mamia ya masheikh wao kwa makosa ya ugaidi. Kuna masheikh wamekaa jela huko Arusha na nchi nzima tangu wakati wa Kikwete, wengine wametolewa na Samia majuzi tu, wengine bado wako ndani!.

Badala waangalie faida za nchi na watu wake, wao wanaangalia kutetea wanasiasa eti kwa sababu ana jina linalojishabihiana na dini yake.

Kwani kuwa Muislamu ni halali kuuza nchi ilmradi unayemuuzia ni Muislamu mwenzio, ni nini maana sasa ya kulinda dhamana uliyopewa?
Inasekitika sna mkuu

HV mzee Mohamed Said Yuko api mnk. Nae kupigania uislmu Ni hodari
 
TEC wenyewe ndio waasisi wa udini nchi hii. Mbona hatuwaoni TEC wakipinga mkataba wa Swissport wa kuendesha viwanja vya ndege nchi nzima? Mbona nyie wapinzani wa ubinafsishaji wa bandari hatuwaoni mkipinga mikataba mingine mibovu waliyopewa Wakristo wenzenu ambao ni Wazungu? Udini na chuki vimewafanya badala ya kupinga vipengele vya mkataba sasa mnapinga mwekezaji! Nyie semeni kuwa hamuwataki Waarabu wapewe bandari maana hata hivyo vipengele mnavyolalamikia vikibadilishwa midhali bado anapewa Mwarabu mtapinga tu.
Kama ungelijua kwanini Nyerere na Karume waliviunganisha hizi nchi. Ni kumdhibiti muarabu asirudi kuipindua tena zanzibar. Na ibaki salama. Lakini naona walioachiwa urithi wanalazimisha kumrudisha muarabu huyo huyo kwa kigezo cha dini na imani. Hata kama anakuja kututawala bandarini milele.

Mkataba urekebishwe. Aingilie mlango wa mbele wa uwekezaji. Na si kwa kigezo cha imani wala dini yake.
 
Kama ungelijua kwanini Nyerere na Karume waliviunganisha hizi nchi. Ni kumdhibiti muarabu asirudi kuipindua tena zanzibar. Na ibaki salama. Lakini naona walioachiwa urithi wanalazimisha kumrudisha muarabu huyo huyo kwa kigezo cha dini na imani. Hata kama anakuja kututawala bandarini milele.

Mkataba urekebishwe. Aingilie mlango wa mbele wa uwekezaji. Na si kwa kigezo cha imani wala dini yake.
Kama hujui historia kaa kimya. Umeongea utumbo mtupu hapa usio na hoja za kisomi.
 
Hakuna mantiki yoyote hapo

Nyie wenye formal education mna msaada gani kwa nchi? Mfano wa aliyesoma ilhali elimu aliyonayo haina manufaa ni sawa na punda aliyebeba furushi la vitabu ambavyo havimnufaishi. Mmesoma lakini ndiyo wezi na mafisadi wakubwa. Mmesoma lakini ndiyo mna udini wa hali ya juu na kueneza chuki dhidi ya wengine. Toka tumepata uhuru nyie ndio wengi serikalini lakini kila siku ni afadhali ya jana. Elimu yenu inawafundisha uharibifu badala ya ujenzi wa nchi na watu wake.
Unayo hoja mkuu! Ila hapa nadhani siyo mahala pake
 
Ni aibu na fefhea endapo bandari hi watapewa wale jamaa kwa IGA na mkataba huo

Hamaza johari ndie aliendesha .majadiliano ya mkabta huo
 
Wanadhani wakatoliki wanapokosoa bandari wanatumia kigezo cha dini, nilitegemea na mashee nao waunge mkono maana ni jambo lililowazi au kama kupinga wapinge kwa mitazamo ya kimaslahi na sio kidini. Mashee wetu wanatudhalilisha tuonekane waislamu wote ni viande wanaropoka ropoka tu mambo
 
Hadi sasa hakuna taasisi yoyote ya Kiislam iwe BAKWATA, Baraza Kuu, TAMPRO, Shia, Ibaadhi, Sunni, Salafi na wengineo walitoa tamko rasmi iwe kuunga mkono au kupinga uwekezaji wa bandari. Waislam wanaozungumza iwe kuunga mkono au kupinga wanafanya hivyo sawa na watu wa dini nyingine ambao wapo wanounga mkono na wapo wanaopinga. Kwanini iwe nongwa Waislam kutoa maoni yao? Kwanini kuunga mkono iwe ni kosa na kupinga iwe ni sawa?
 
Wale wazungu wa kahama barick wanachota dhahabu kila siku lakin sijasikia tamko lolote la TEC

Waraka wa TEC umegusa yote we mvaa kibandiko + kobazi. Soma acha kuishi kwa hisia na kuendekeza imani kwenye masuala ya kijamii na kiuchumi. Wale huna DPW huna undugu nao sio wenye rangi yako wale. Waliwafunga minyororo babu zako na kuwauza kama mifugo leo unawatetea?
 
Hakuna mantiki yoyote hapo

Nyie wenye formal education mna msaada gani kwa nchi? Mfano wa aliyesoma ilhali elimu aliyonayo haina manufaa ni sawa na punda aliyebeba furushi la vitabu ambavyo havimnufaishi. Mmesoma lakini ndiyo wezi na mafisadi wakubwa. Mmesoma lakini ndiyo mna udini wa hali ya juu na kueneza chuki dhidi ya wengine. Toka tumepata uhuru nyie ndio wengi serikalini lakini kila siku ni afadhali ya jana. Elimu yenu inawafundisha uharibifu badala ya ujenzi wa nchi na watu wake.

Wanaokutibu ukiugua kaswende na gono huko mahospitalini elimu yao waliipata madrasa,unatumia huu mtandao kwa kujinafasi kabisa je hawa wanaokufanya uutumie huu mtandao elimu yao waliipatia madrasa?
 
Wanaokutibu ukiugua kaswende na gono huko mahospitalini elimu yao waliipata madrasa,unatumia huu mtandao kwa kujinafasi kabisa je hawa wanaokufanya uutumie huu mtandao elimu yao waliipatia madrasa?
Popote mlipo wengi wenu mpo kwa maslahi binafsi kama vile wizi, ufisadi na dili chafu. Ndio maana nchi haiendelei. Elimu mnayojivunia tija yake kwa Taifa ni ndogo sana. Hata huko hospitali ulikosema mnauza madawa na vifaa tiba na mnatoa huduma mbovu. Kwa ufupi hamna msaada wowote wa maana.
 
Kama kuna kitu Waislamu tunapaswa kukifanya katika kuandika HISTORIA yetu na ikasomwa kila baada ya sala ni hii ya Ikulu ya Magogoni hapa Dar es salaam maana ni historia yetu na ni halali kwetu kufanya hivyo ila sio kwenye suala la Mkataba wa Bandari; huko tunahitaji kuwa na ufahamu wa kutosha kuhusu mikataba ya kimataifa.

Viongozi wetu hasa Ma-Imamu wetu na wengine wanaokaribishwa kutoa neno, wakumbuke kwamba suala la Bandari
Tangu lini umerudi kwenye uislam,baada ya kubadilishwa dini na huyo mzungu mwanamke (angel) na kuwa mkatoliki leo ndo unakuja kuusema uislam.
 
Kama kuna kitu Waislamu tunapaswa kukifanya katika kuandika HISTORIA yetu na ikasomwa kila baada ya sala ni hii ya Ikulu ya Magogoni hapa Dar es salaam maana ni historia yetu na ni halali kwetu kufanya hivyo ila sio kwenye suala la Mkataba wa Bandari; huko tunahitaji kuwa na ufahamu wa kutosha kuhusu mikataba ya kimataifa.

Viongozi wetu hasa Ma-Imamu wetu na wengine wanaokaribishwa kutoa neno, wakumbuke kwamba suala la Bandari lin

Kwa hiyo katika mambo tunayoweza kuyafundisha kama historia ni haya lakini sio huku tunakotaka kwenda.


Tujisahihishe
Barikiwa
 
Back
Top Bottom