Waislam tunapaswa kuondokana na upofu wa dini la sivyo tutaonekana wote hatuna akili

Mnaudhalilisha uislamu. Muislamu popote alipo kazi yake ya kwanza ni kupinga maovu kama haya ya serikali ya awamu ya 6. Maovu yamevuka mipaka mpaka wanaamua kuuza ardhi na watu walioko. Ni dhihaka.
 
Ktk suala hili la Bandari, Waislamu tumejifedhehesha kidogo. Tunakurupuka. Tunatumiwa. CCM wajanja sana.
 
Kwaimani yetu waislam hatuna kitukingine chakutufunza zaidi ya kitabu tukikiacha tumekwisha
Dini ya kweli ni pesa. Pesa ndio zinaweza kufanya mambo yako mengi yakakaa sawa, sio dini boss. Waislamu, wakristo na wasio kuwa dini, wote hao maisha yao yananyooka wakiwa na pesa, na sio wakiwa wameshika sana dini.
 
Raisi akiufuta huo Mkataba atapita kwa kishindo 2025.
Pia liwe somo kwake kuwa nchi imemkabidhi raslimali zote aziongoze na kuzilinda.

"Dunia ya leo haina rafiki bali ina fulsa tele. Hakuna Tabasamu la kweli bali la mali" by Mimi,

Nchi imeahidi kumhudumia maisha yake yote.
Awe makini asiingizwe tena kwenye Mkenge na Wasaka Tonge.
 
Siku likija suala la Mahakama ya Kadhi sijui itakuajee kwakweli, ambalo kimsingi ndilo linaweza kua sura ya kidini.

Wakati huo sijui akina jakaya watasema kuchanganya bongo flavor na hip hop au itakuaje,
Maana dipi weldi wamesema ni kuchanganya dini na siasa
 
Dini ya kweli ni pesa. Pesa ndio zinaweza kufanya mambo yako mengi yakakaa sawa, sio dini boss. Waislamu, wakristo na wasio kuwa dini, wote hao maisha yao yananyooka wakiwa na pesa, na sio wakiwa wameshika sana dini.
Endelea kuamini dini yako wewe nipesa Mao asingekufa kwangu Mimi na waminio pesa nimapito
 
Ikiwa mahakama imeshauri mkataba urekebishwe nyinyi nani wa kusema mkataba haufai?
Hakuna kitu kitakachofnaywa na mwanadamu kikawa kamili kwa mwanadamu mwingine.
Ikiwa mnaona CCM inawatumia vibaya waislamu, je nitakuwa sahihi kusema na CHADEMA inawatumia baadhi ya wakristo na makanisa vibaya kwa kupinga mkataba?
 
Endelea kuamini dini yako wewe nipesa Mao asingekufa kwangu Mimi na waminio pesa nimapito
Kifo hakihusiani na dini, labda useme mtu akiwa kwenye dini yako hafi. Lakini ni dhahiri mtu mwenye pesa ama maisha mepesi kuliko mshika dini.
 
Kanye kanisani
Hata akinya kanisani unadhani wakristo huwa tunafanya fujo yoyoye? Sana sana tutasafisha huo uchafu na kulaani kitendo hicho. Hatutachoma misikiti kama nyinyi mnavyofanya mkiwa provoked.
 
Mkuu wewe ni muislam na mzalendo wa kweli!
 
NEW WORLD ECONOMIC ORDER ndio inayowafanya DPW wakutane na upinzani hapa Tanzania. Ukubwa wa hiyo kampuni ya Dubai huwezi kuulinganisha na hao waturuki wanaojenga SGR.

Wanamiliki meli 400 kwa ufupi ni watawala wapya wa biashara ya usafiri wa kwenye maji.

Kuondoka Djibouti ni masuala ya kuingia mikataba bila ya kuwa na utaalam mzuri, na kwenye utaalam Tanzania tupo vizuri sana kuliko Djibouti.
 

..uamuzi wa mahakama huwa haufuti mtizamo au maoni ya mhusika / wadau kuhusu shauri husika.

..Unaweza usikubaliane na hukumu lakini unawajibika kuheshimu maamuzi ya mahakama.

..hivyo basi hukumu ya mahakama haizuii wananchi kusema kuwa mkataba na Dubai haufai kabisa, unahitaji marekebisho, au unafaa.

..dhana kwamba CCM inawatumia vibaya Mashekhe na Maimamu inatokana na hoja ambazo huzijenga, na uzito wa hoja hizo.

..Kwa mfano, kuna Mashekhe na Maimamu badala ya kuujadili mkataba na vipengele vyake wanawajadili wale walioupinga mkataba huo.

..Mazingira hayo ndio yanayosababisha uwepo wa tuhuma kwamba hawa ndugu zetu wanatumiwa vibaya na CCM kushambulia wanaopinga mkataba wa Dp.

..Kwa upande mwingine kuna Mashekhe na Maimamu ambao wamejisimamia wenyewe na wametoa maoni yenye kujenga.

..Shura ya Maimamu kipindi cha nyuma walitoa maoni ambayo yako very constructive na maoni hayo yalipokelewa vizuri.
 
mkorinto kwanza ujifunze kiswahili vizuri, hakuna kitu kinaitwa "walaka" ni waraka, asili ya neno hili ni kiarabu lenye maana ya jani la mti, kwa kuwa watu wa zamani walikuwa wakiandika kwenye baadhi ya majani ya miti au vitu mfano wa majani, kwa kiswahili waraka ni karatasi iliyoandikwa taarifa maalum.
TEC ni wawakilishi wa wakristo wa kikatoliki, waraka waliyoutoa wa kupinga uwekezaji wa DPW kwenye bandari zetu kwa kusema wao wanawawakilisha watanzania wengi wenye kuukataa uwekezaji huo, swali huo wingi wa wanaowakilshwa na TEC wamepimwaje? Ikiwa TEC inawawakilisha wapinga mkataba na miongoni mwao wamefika kumshutumu raisi kwa imani yake na uasili wake kwa kusema kwa kuwa yeye ni mzanzibari na muislamu ndiyo maana anataka kuiuza nchi ya Tanganyika kwa waarabu, kwa muktadha huo ndiyo maana TEC inaingia kwenye shutuma hiyo. Ni kweli wachungaji wengi wana shahada za juu lakini kwa hili wamekosa hekima kabisa, taasisi ya kidini unaona kuna moto unawaka wewe unakwenda kumwagilia petroli! TEC wamezungumza na raisi wamezungumza na wizara, wamezungumza na vyombo mbalimbali kuhusu suala hili, ambalo serikali imelitia saini, bunge imelipitisha, mahakama imeliridhia, sasa kutoa huo waraka ni kama kudharau maamuzi ya serikali, bunge na mahakama? Huo waraka hauna afya ya usalama kwa nchi kama yetu, hayo mambo wawaachiye vyama vya siasa vya upinzani vilishughulikie haya mambo ya kuipinga serikali, wao wabaki na kondoo wao katika kuimarisha imani za wafuasi wao. Baadhi ya masheikh wamekasirika si kwa sababu ya kupinga uwekazaji wa bandari bali jinsi upingaji ulivyowasilishwa na baadhi ya wanasiasa na viongozi wa dini ya kikristo kwenye mitandano na hata mikutano ya hadhara.
Mkataba unautaalamu wake katika kuandika na hata kuusoma na kuelewa ndiyo maana wanasheria wasomi wamekwenda mahakamani kutafuta msaada wa kishreia katika mambo ambayo wao wameyaona ni mapungufu ya kuufanya mkataba uwe batili, hatima yake mahakama imetoa ushauri kama kuna maboresho yafanywe kwenye huo mkataba na kuitupilia mbali kesi na uwekezaji uendelee.
Waislamu kutokana na misingi ya sheria zao za dini, ndiyo zimewafanya kuwa na mikataba bora yenye kuwa na uaminifu, haki na uadilfu katika kutekeleza makubaliano yao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ