Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Ukijaribu kitazama vizuri, hayo mambo ya utawala wa enzi za Nyerere yana tofauti ndogo sana na sasa. Hata Sasa hakuna uhakika wa kupata haki huko mahakamani iwapo viongozi watatoa maelekezo toka juu. Unaweza kuporwa mali yako na viongozi na usifanye Lolote. Rejea alichofanya Magufuli na fedha za Plea bargaining, na fedha za bureau De change. Mabadiliko yaliyoko sasa ni maigizo tu, lakini tabia zile zipo Hadi Leo.
Angalau hakuna ushahidi kwamba Nyerere alinyang'anya watu mali kwa maslahi yake binafsi au ya wale waliomzunguka. Nyerere alikuwa na makosa na kasoro zake nyingi ila ni vigumu kuziona katika mrengo wa maslahi yake binafsi, familia au waliomzunguka.
 
Huwa najiuliza sana lakini sipati majawabu, lakini naomba wasomi wa humu ndani mnisaidie.

Hivi Mzee Nyerere alikuwa ana roho ya namna gani kuona mambo kama haya yakitokea kwa wananchi lakini bado hataki kubadilika na akaendelea kutumia mkono wa chuma kuhakikisha anasigina kabisa uwezo binafsi wa mtanzania kuweza kujikwamua kiuchumi. Ujamaa wa Tanzania hakuleta matokeo yoyote makubwa na ya kuchangaza ukilinganisha na kule Asia na Ulaya ambako walau walifanya mapinduzi ya sayansi na teknolojia.

Uchina walifanikiwa sana baada ya Raisi Deng Xiaping kuanza kuwaonea huruma raia wake akifahamu kabisa kwamba njia waliyokuwa wanaenda ilikuwa siyo sahihi. Aliruhusu watu waanze kumiliki mali zao binafsi na kufanya biashara. Najiuliza sana, miaka yote 18 ya Ujamaa, yalifanyika na kutokea mambo mengi mno kwa watanzania, kiasi kwamba kiongozi yoyote mwenye huruma na wananchi ni lazima angekaa chini na kujifanyia tathmini, lakini Raisi Nyerere hakufanya hivyo, aliendelea kuwa na moyo mgumu kama Farao. Hebu tuzingatie haya:

1. Sera ya utaifishaji wa mali, ilileta umasikini mkubwa sana kwa watu.
2. Kufuta vikundi ya ushirika (Cooperatives) na kuweka vile vya TANU kulididimiza mno sekta ya kilimo.
3. Kupiga marufuku watu binafsi kuagiza bidhaa nje ya Tanzania kulipelekea uhaba wa bidhaa na huduma muhimu.
4. Kuweka ugumu katika kusafiri (Travelling Restrictions) kulisababisha ukosefu wa ujuzi kwa watanzania.
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.

Mpaka kufika miaka ya 80's Ujamaa ulikuwa umefeli vibaya mno. Tanzania tulikuwa hatuna hata unga wa kupikia, mafuta, wala sukari. Mtaa mzima mlikuwa mnaenda kwa mwenyekiti kuomba sukari au sabuni kutoka maduka ya ushirika. Ukikamatwa na mafuta, sabuni au dawa za binadamu zilizolanguliwa kutoka Kenya lazima ushughulikiwe na dola. Kama ulisoma miaka ya 80's unaweza kukumbuka kwamba hata sare za shule zilikosa rangi, watu tukawa tunavaa vitu vya ajabu vilivyochakaa kama vile vichaa. Ukibahatika kukutana na wamishionari au taasisi za kidini ndiyo ulikuwa unaweza kupewa hata nguo, mahitaji na wazungu.

Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.

Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?​
Ule ni mfumo wa utaahira ambao ulilenga kuwafukarisha watu Ili uwatawale.

The likes of Magufuli system ilikuwa Ukiwa na tu mil.10 wewe ni mhujumu uchumi utaletewa Kila Figisu ili tuu uendelee kuwa mnyonge na kumpogia makofo Jiwe.

Jiwe anajua fika ukitaka kumtawala mtu mfanye maskini.

Tofauti na Samia anajaribu Kuwavutia wenye pesa upande wake Ili asipate shida kwenye kutawala.
 
Tukumbuke pia wakati wa Nyerere kulikuwa na vita kali baridi ya Magharibi na Mashariki, Nyerere hakuwa anapenda ubepari wa Magharibi lakini pia hakuwa tayari kufuata ule ujamaa halisi na ukatili wake kama wa USSR na China hapo ni kama alipatwa na dilemma ya kujua muelekeo ni upi na akalitatanisha taifa pia, japo kwa nia njema kwamba Tanzania inatakiwa kuwa sovereign na sio kibaraka wa yoyote.
Nyerere aliupenda sana udikteta wa China kipindi cha mwenyekiti Mao kitu kingine Nyerere huyo huyo alienda China kwa mara ya Kwanza katika miaka ya 60 kipindi ambacho China kulikuwa na ubabe wa kutisha wa genge la Mao kwa wale wasio wafuasi wake.

Hiyo miaka ya 50 na 60 ndio kipindi China ilikuwa inafanya blunder nyingi kubwa za kiuchumi zilizo wagharimu na Nyerere alicopy na zikamuangukia pua.

Utofauti wake na Mao ni baada kutokuelewana kati ya Usovieti na China Mao kuamua kuamisha upepo na kufungua milango ya magharibi miaka ya 70.
 
Changamoto ya Tanzania siyo umasikini. Katika ngazi ya kitaasisi Tanzania imekuwa sana kiuchumi na inaendelea kukua kwa kasi. Nchi ina uwekezaji kutoka nje (FDI), inafanya biashara za kimataifa (International Trade) na ina nguvu kazi iliyoelimika (Skilled Manpower). Changamoto kubwa ya Tanzania ni mgawanyo wa keki ya taifa (Redistribution of National Wealth), kwasababu sehemu kubwa ya uchumi wa nchi inamilikiwa na matajiri wachache ambao mifumo inawalinda. Hili ni tatizo ambalo linaikumba dunia yote kwasasa, kwamba watu wanafanya kazi lakini utajiri wao unanyonywa kupitia mifumo ya kiutawala.

Hata Marekani kuna hii shida, Uingereza kuna hii shida, Nigeria ambako ndiyo wakubwa hapa barani kuna hii shida. Ndiyo maana unakuta taifa linatangazwa kweli linakua kiuchumi, lakini huo uchumi wewe raia wa kawaida hauoni, ni kwasababu mifumo inakupa wewe kitu kidogo ila inakunyonya sana. Hili ndiyo mwanauchumi nguli kabisa duniani aliyewahi kushinda tuzo ya Nobel, Prof Joseph Stiglitz anaelezea kwenye kitabu chake kiitwacho THE PRICE OF INEQUALITY. Hivyo Tanzania, chakula kipo, ardhi ipo, huduma zipo lakini kuzipata huduma hizo bila kuwa na pesa ndiyo changamoto.

Hivyo wananchi wengi na watumishi wa ummah, wanafanya kazi sana huku nguvu zao zikinyonywa na wanaoshikilia mfumo. Wanakata kodi kubwa (Levying Heavy Taxes), hawadhibiti mfumuko wa bei (They can't curb inflation) jambo ambalo linaharibu akiba za watu, hawayatozi mashirika makubwa kodi inayotakiwa(Tax Holidays to the Rich), matumizi yasiyo na msingi (Excessive Government Spending) na rushwa (Corruption). Hizi ndizo changamoto zetu kipindi hiki, Raisi Mzee Mkapa alijitahidi kupambana nazo japo hilo la rushwa lilimshinda kabisa.​
Tanzania bado ni masikini sana hata cha kugawana bado ni kidogo, huwa nashangaa watu wanaoshangilia ukuaji uchumi usiozidi 7%. Uchumi wa China wakatia unawaondoa raia wake wengi katika umaskini ulikuwa unakuwa hadi kwa 14%. Sisi angalau hatukapaswa kushuka chini ya 10% hata kwa miaka 10 mfululizo.
 
Ule ni mfumo wa utaahira ambao ulilenga kuwafukarisha watu Ili uwatawale.

The likes of Magufuli system ilikuwa Ukiwa na tu mil.10 wewe ni mhujumu uchumi utaletewa Kila Figisu ili tuu uendelee kuwa mnyonge na kumpogia makofo Jiwe.

Jiwe anajua fika ukitaka kumtawala mtu mfanye maskini.

Tofauti na Samia anajaribu Kuwavutia wenye pesa upande wake Ili asipate shida kwenye kutawala.
Magufuli na Samia wote sawa.

CCM imejaza watu wa ajabu ajabu na machawa kama wewe
 
Tanzania dependency ratio bado ni kubwa brother na hata ukiangalia kiwango kikubwa cha ajira na biashara kinategemea sekta isiyo rasmi ambayo ni hand to mouth. Kiufupi Tanzania tuna unproductive population na hata graduates bado wengi hawawezi kupambana katika mfumo wa dunia

Hiyo FDI ni sawal lakini impact yake kwa common mwananchi ni nini zaidi ya Capital inflow and profit outflows ya kutosha

Huko kwenye international market tunyamaze tu maana ukifikiria balance of trade unaweza kulia japo haishangazi maana hata toothpick tunaagiza

Kiufupi vya kujivunia vichache
Hakika, Tanzania bado tunajitafuta kwenye suala la uchumi na maendeleo, bado tuko mbali sana.
 
Tukumbuke pia wakati wa Nyerere kulikuwa na vita kali baridi ya Magharibi na Mashariki, Nyerere hakuwa anapenda ubepari wa Magharibi lakini pia hakuwa tayari kufuata ule ujamaa halisi na ukatili wake kama wa USSR na China hapo ni kama alipatwa na dilemma ya kujua muelekeo ni upi na akalitatanisha taifa pia, japo kwa nia njema kwamba Tanzania inatakiwa kuwa sovereign na sio kibaraka wa yoyote.
Utofauti ni kwamba Nyerere yeye hakuwa tayari kuacha ukatoliki na kuwa mkana Mungu kama idol wake Mwenyekiti Mao na wakomunisti wa China.
 
Hii katiba inayomfanya Rais awe juu ya Sheria ni yeye aliiweka. Unatarajia Nini kama cheo Cha rais ndio kinapanga nani awe kiongozi? Au unadhani misingi mibovu ya hivyo inaondoka kirahisi huku afrika bila machafuko na mapinduzi ya kijeshi?
Katiba inaweza kuwa tatizo lakini kuna matatizo ya Waafrika ni common na ni vigumu mno kuyaelezea wakati mwingine.
Mfano Kenya wana Katiba nzuri ila ufisadi umetamalaki na pia viongozi wanapatikana zaidi kwa demokrasia ya ukabila, huu ni mtanziko wa aina yake.
 
Angalau hakuna ushahidi kwamba Nyerere alinyang'anya watu mali kwa maslahi yake binafsi au ya wale waliomzunguka. Nyerere alikuwa na makosa na kasoro zake nyingi ila ni vigumu kuziona katika mrengo wa maslahi yake binafsi, familia au waliomzunguka.
Ndio hapo niliposema Kuna tofauti ndogo sana ya mambo ya utawala wa Nyerere na wa sasa. Ni kweli hakufanya maamuzi mengi kwa maslahi yake binafsi, lakini Bado hakuruhusu maamuzi yaliyokuwa hayamfurahishi. Na Hawa wengine wameiga huko huko japo Kuna tofauti Fulani ya approach.
 
Hizi ndizo akili za wana CCM. Foolish

Buku ngapi dogo wanakupa kama kifuta jasho
Buku Moja tuu sawa we boya
20230215_120116.jpg
 
Katiba inaweza kuwa tatizo lakini kuna matatizo ya Waafrika ni common na ni vigumu mno kuyaelezea wakati mwingine.
Mfano Kenya wana Katiba nzuri ila ufisadi umetamalaki na pia viongozi wanapatikana zaidi kwa demokrasia ya ukabila, huu ni mtanziko wa aina yake.
Lakini kwa upande wa demokrasia hasa unaolindwa na katiba ya Kenya, wako maili nyingi kulinganisha na sisi. Sisi hatuna ukabila hilo ni kweli, lakini wenye ukabila wana demokrasia nzuri kuliko sisi.
 
Nakubali kwamba Tanzania kuna changamoto nyingi tu, niseme haya yafuatayo:

Mosi, Tanzania inaweza kutengeneza Healthiest Dependency Ratio kwasababu, watu wenye uwezo wa kufanya kazi (Working Age Population) ni wengi kuliko wale wasioweza kufanya kazi (Dependents). Hili ni tatizo la kisera ambalo serikali ikiwa makini inaweza kulimaliza kama Uchina walivyofanya. Injecting the youths into the Market, either through employment and self-employment. Tanzania imejaa vijana waliomaliza chuo kikuu wenye utaalamu mwingi ambao wanaweza kufanya kazi endapo watawezeshwa na kusaidiwa.

Pili, FDI ni muhimu na Tanzania ni nchi ambayo ni kivutio kikubwa. Hili mbona halina ubishi. Tatizo ni lilelile la kisera, kwamba tunafanyaje kuhakikisha kwamba watanzania wa kawaida wananufaika na uwekezaji kutoka nje, aidha kwa kupitia kodi, ajira, ujuzi na ushirikishwaji katika uwekezaji. Mpaka sasa faida haionekani kwasababu kuna sehemu panavuja na hatujasimama kidete kuhakikisha tunarekebisha. Mashirika mengi yanapewa Tax Holidays na mikataba ya uwekezaji ina changamoto kama ule wa bandari. Ila binafsi naamini leo hii tukiamua kukusanya kodi kwa mashirika yanayowekeza hapa nchini, hela ipo nyingi mno.

Tatu, kwenye biashara ya kimataifa sisi ni Commodity Based Economy bado hatujawa Industrial Based Economy au Financial Based Economy nadhani tuendelee kujikita huko ambako tuna Comparative Advantage. Soko la dunia ya leo linahitaji sana rasilimali za uzalishaji ambazo Tanzania inazo kwa wingi na zinaiuzwa kwa Benchmark Price. Tunaweza kufanya mambo mengi mno kupitia Bilateral Trade na tukafanikiwa vizuri sana, tatizo ni kwamba watu wanafanya maksudi kwasababu wanataka kupata mafungu ya kumi (Ten Percent).

Nne, viwanda vidogo-vidogo vya kutengeneza Toothpick vinaweza kuanzishwa nchini Tanzania hata kesho endapo tutaamua. Kipindi hiki inawezekana kwasababu watu wengi wana mitaji na ujuzi, na uwepo wa soko la ajira la bei nzuri (Cheap Labour). Tatizo tunarudi palepale, kwamba watu wananufaika wenyewe na hii hali.

Niseme tu, hakuna pesa ambayo inatengenezwa Tanzania isionekane. Pesa zipo lakini zinaingia mifukoni kwa watu ndiyo maana uchumi kweli unakua lakini wewe mtu wa kawaida huuoni kwasababu, watu wachache wanazitafuna na kujimilikisha nchi. Hili ndiyo changamoto yetu Tanzania.​
Mimi ni moja ya waamini kuwa Tanzania inahitaji black enterprises nyingi zaidi kuliko wawekezaji. Hapa tulipo tu uchumi umeshikiliwa na watu ambao hawana asili ya Tanzania lakini private sector imeshikiliwa na multinationals hivyo, kuhimiza uwekezaji wa foreigners ilhali Tu watanzania bado hawajafikia kiwango cha kutengeneza biashara kubwa kiasi cha kutumia rasilimali zilizopo ipasavyo,

Tutangeneza taifa lenye uchumi unaomilikiwa na wageni huku wenyeji wakibaki kama vibarua

Kwenye uchumi kwa sasa naona diversity imekuwapo haswa baada ya service and creative industry kuja juu japo, tourism inachangia pakubwa lakini nilitamani tuwekeze nguvu kwenye utalii wa mijini ili hata miji yetu ifikie global standards za kuhost watalii kama Rwanda inavyojitahidi kuifanya kigali kuwa mji wa kitalii wa kiteknolojia, burudani na mikutano.

Gaps zipo nyingi sana za kushauri na sidhani kama zitafanyiwa maana kama ulivyosema. Mfumo uliopo unanufaisha baadhi ya watu
 
Mataifa karibia yote yaliyokuwa na mchanganyiko mkubwa kama sisi yalianza kuliwa na ukanda, udini na ukabila baada ya wakoloni kuondoka. Penda usipinde Nyerere aliweza kudhibiti hilo na kuunda taifa, wengi waliochanganyikana kama sisi waliishia kuwa na nchi na kuhasimiana tu.
Ukabila usingeweza kutokea Tanganyika.

Moja ya blunder kubwa ya Nyerere ni totally failure ya kushindwa kutengeneza nchi moja Tanzania.

Huyu mtu unamsifu kwa sababu gani nchi ya Tanganyika? Kama tu kuunda taifa moja la Tanzania alifeli ni kipi unacho msifu ?
 
Back
Top Bottom