Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Hao viumbe sijui wana mindset ya aina gani, kusema Nyerere bado anaishi huku wameharibu kila kizuri alichofanya kama viwanda, naona wana na matatizo ya akili.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Hakuacha viwanda hivyo vikiwa functional, alivirithi vingine kutoka kwa watu binafsi vikafia serikalini, ni vilikuwa na uzalishaji usio na tija, gharama kubwa kuliko mapato... Vingine vikaja kubinafsishwa tena na Mwinyi ndio kidogo tuna viwanda kama TBL na Serengeti vinavyozalisha vinywaji kwa tija na kulipa kodi kubwa
 
Kwenye hayo machafuko kuna familia zitapoteza wapendwa wao.......
Upo tayari kuitoa familia yako ipotee kwenye hayo machafuko unayoyaomba?
Niko tayari, ili mradi yapatikane mabadiliko ya kweli. Na kwa kukusaidia tu, hata Mimi Niko radhi kufa kwa ajili ya mabadiliko hayo.
 
Basi naomba takwimu za Raisi aliyefanya vizuri kuliko wote hapa nchini kwenye suala la uchumi. Nasubiri majibu!​
Mkuu kila mmoja alijitahidi kwa namna yake. Kwanza kabisa Julius K. Nyerere aliikuta Tanganyika ina uchumi imara Afrika Mashariki. Akataifisha, akajenga viwanda kadhaa, akaleta ujumaa uchumi ukaanguka mpaka kila kitu kikakwama, akafunga nchi hakukuwepo na demokrasia, hadi Nyerere anang'atuka nchi ilikuwa nchi ya mwisho masikini duniani!

Akaja Mzee ruksa, Ali H. Mwinyi, akafungua mipaka ya nchi. Nchi ikaanza kupumua. Akapambana na uchumi, angalau maisha ya wananchi yakawa na ahueni kiasi ukilinganisha na kipindi cha Mchonga, ila hadi anaondoka serikali ilikuwa hoi bin taaban.

Mzee wa ukweli na uwazi Benjamin W. Mkapa akaingia, akaweka mifumo ya mapato, uongozi, usimamizi na udhibiti serikalini. Akapunguza mzigo wa madeni ya nje, akawezesha ubinafshishaji na kuvutia wawekezaji wa ndani na kutoka nje . Hadi anaondoka demokrasia ilishaanza kushamiri na uchumi ulikuwa umeanza kutengamaa na serikali ilikuwa na hela.

Akaingia Mzee wa mtandao; ari mpya, nguvu mpya na maisha bora kwa kila mtanzania, Jakaya M. Kikwete. Kaanza kwa kupanua wigo wa demokrasia, akajenga miundombino ya barabara nchi nzima kuunganisha mikoa na wilaya, akaongeza viwanda, akapanuwa uwekezaji kwenye viwanda, elimu, afya, benki, ujenzi, utalii, nishati, uchukuzi, mawasiliano, maji na kilimo. Akaimarisha maslahi ya watumishi wa umma, akaongeza ajira kwa vijana kuliko Rais yeyote nchini, Akaimarisha usalama kila kona ya nchi. Akagatua madaraka kwa kuongeza mikoa na wilaya kama sehemu ya kupelekea huduma na maendeleo zaidi kwa wananchi. Mahusiano na diplomasia ya nchi yetu ikafikia viwango vya juu duniani. Volume ya biashara ndani na nje ya nchi ikawa kubwa sana kiasi cha kuifanya kariakoo kuwa hub ya biashara kwa nchi za burundi, Uganda, Rwanda, Comoros, Madagascar, Malawi na Zambia. Aliwekeza kwenye usalama wa majeshi yetu ya ulinzi kiasi cha kutambulika kimataifa. Kama kuna wakati wanainchi wengi waliweza kufanya maendeleo yao binafsi ni kipindi cha awamu ya 4. Hata msingi wa kufikia uchumi wa kati ulitokana na uchumi aliouimarisha Jakaya. Hadi anaondoka wananchi walikuwa na hela na serikali ilikuwa na hela

Akaingia Mzee wa hapa kazi tu John P. Magufuli! Ikawa kazi kweli kweli! Akavuruga wafanyakazi kisa vyeti feki, wafanyabiashara, wawekezaji, wapinzani na majirani. Miaka mitano tu nchi ikawa na deni la nje tirilioni 66 kutoka tirilioni 26, kiwango cha demokrasia kikashuka, mahusiano ya nje yakaporomoka, bidhaa zikapanda bei, ajira ikawa mtihani. Akawa juu ya katiba na mizizi ya utawala wake ikajichimbia zaidi, upendeleo wa maendeleo ukazaliwa na ufisadi wa kihistoria ukatokea Ikulu! Akawaibia machinga kwa kuwa vitambulisho visivyo na maana, mauwaji yakashamiri, vyombo vya habari vikaufyata, viongozi wa dini wakatishiwa kufutiwa uraia wao! Na uporaji wa fedha za maduka ya kubadilisha kutumia jeshi mchana kweupe. Kwa mara ya kwanza fremu Kariakoo zikakosa wateja! Akaturudisha nyuma miaka 30, Mungu akaingilia kati, akaenda zake! Hadi anaenda zake vyuma vilikuwa vimekaza ajabu! Wananchi na serikali ilikuwa hoi! Hawana hela!

Ndio akaingia mama wa Kazi iendelee; mama wa 4R Samia S. Hassan. Kakuta mvurugano zaidi ya mkorogano, nchi ilikuwa imegawanyika, uchumi upo hoi, Kakuta miradi mikubwa isiyo na vyanzo vya hela, kakuta ajira hakuna kwa miaka 6, kukuta demokrasia iko taaban, mifumo ya serikali haifanya kazi na mahusiano ya nje yameparaganyika. Ndio akaanza kutanzua, kufungua na kuzibua palipoziba.

Kwa sasa nchi ameituliza, mahusiano ya nje yamerudi, biashara imeanza kuimarika na uwekezaji umeanza kurudi, demokrasia inaendelea inachipua. Ugumu unao onekana ni matokeo ya uharibifu na uchafu uliofanywa na awamu ya 5. Hata hivyo Samia anapamba sana, ni kazi ngumu kweli kweli! Hadi anamaliza muhula wake wa kwanza atakuwa amemaliza kusafisha na kusawazisha uharibifu alioukuta!
 
Mkuu Ujamaa umeanza mwaka 1967, baada ya Tanzania kuzaliwa mwaka 1964 na umoja ulikuwepo. Kusema kwamba umoja wa kitaifa umeanza baada ya mwaka 1967 ni kosa la kimantiki. Sambamba na hili, unataka kuniambia Tanzania ya Ujamaa ilikuwa na umoja wa kitaifa kuliko taifa la kibepari la Ujerumani Magharibi au Tanzania ilikuwa na umoja wa kitaifa zaidi ya mataifa ya kiarabu yanoyoishi kifalme kama Saudi Arabia na UAE ?​
Usiende huko, Muulize kama tuliwazidi Umoja USA ?
 
Basi naomba takwimu za Raisi aliyefanya vizuri kuliko wote hapa nchini kwenye suala la uchumi. Nasubiri majibu!​
Wacha usanii, wewe ulikuwa unamsifu Mkapa kwa vigezo gani?!

Umenifanya nimecheka, kumbe hukuwa na vigezo vyovyote vya kumsifu Mkapa!

Mimi sikuja na mada hapa ya kumsifu au kumponda anyone, wewe mleta mada ndie mwenye jukumu la kutuonesha ubaya wa yule unayemponda, kisha utuoneshe uzuri wa yule unayemkubali kwa vigezo, wala sio kuishia kumtaja kwa jina tu.

That's why i told you earlier, hii mada yako imekaa chongo sana, ndio maana wengi wanaokuunga mkono imewalazimu kujigeuza maroboti, kuutazama upande mmoja tu wa Nyerere, kama vile mwingine hawauoni!.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Hakuacha viwanda hivyo vikiwa functional, alivirithi vingine kutoka kwa watu binafsi vikafia serikalini, ni vilikuwa na uzalishaji usio na tija, gharama kubwa kuliko mapato... Vingine vikaja kubinafsishwa tena na Mwinyi ndio kidogo tuna viwanda kama TBL na Serengeti vinavyozalisha vinywaji kwa tija na kulipa kodi kubwa
Unaonekana una tatizo binafsi na Nyerere, unataka kutudanganya hapa viwanda vyote alivyoacha Nyerere havikuwa vikifanya kazi?!

Ile General Tyre kule Arusha haikuwa ikifanya kazi? Mwanza Textiles haikuwa ikifanya kazi? Musoma... Tanga.... Morogoro...

Wewe ni muongo, mmejaa ushabiki maandazi tu na wenzako, hamna hoja yoyote zaidi ya mihemko.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Kuna watu chuki yao dhidi ya Nyerere imejaa udini sana.

Sasa huyu anamshutumu Nyerere kiuchumi lakini anahusisha na Nyerere kuitwa mwenye heri na wakatoliki wenziwe!!
 
Kuna watu chuki yao dhidi ya Nyerere imejaa udini sana.

Sasa huyu anamshutumu Nyerere kiuchumi lakini anahusisha na Nyerere kuitwa mwenye heri na wakatoliki wenziwe!!
Hata hawa wengine wanaompinga huku, unapoona wanatumia mpaka hoja za uongo ilimradi wajibu ujue kuna motive behind, wanasukumwa na mihemko yenye vimelea vya chuki tu.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Kwenye hili Nyerere alikuwa ndiye bingwa. Alikuwa kila anayemkosoa anahama nchi. Ni vile tu ukweli hausemwi na bahati mbaya Nyerere katawala ktk kipindi ambacho media outlets zilikuwa hakuna.

Redio ya taifa ilikuwa inaandikiwa nn cha kusema kuhusu rais kwenye taarifa ya habari.

¶ Nyerere ndiye aliyefanya Kambona kuishi ukimbizini maisha yake yote.
¶ Nyerere ndiye aliyechana vyeti vya Tuntemeke Sanga.
¶ Nyerere ndiye aliyemfunga kifungo cha nyumbani (alimuweka kizuini) Kasangatumbo
¶ Nyerere ndiye alimuondoa kwenye urais Abdul Jumbe halafu akamuweka kizuizini hapo Kigamboni mpk umauti.
¶> Nyerere ndiye aliyetunga hili katiba bovu lililomfanya yeye kujipa umungu wa Tanzania.

Nyerere ni dikteta asiyesemwa.
Naunga mkono hoja
 
Wewe unatatizwa nao?
Sio issue kwangu.....
Ila ukianza kujenga hoja kupitia mlango wa imani inaanza kuleta shida kidogo, watu wajiulize lengo ni nini haswa.
Mfano, Ungeweza kuleta hii mada nzima bila kukejeli "Utakatifu" na ikaeleweka.

Utakatifu wake anapewa na wakatoliki wenzake, na si Taifa.
Hivyo huo si mjadala wa kitaifa bali ni mjadala wa kikatoliki.
Kama unatatizwa na hilo kiasi cha Kuleta mada, unaweza kwenda kupinga tu.
Lakini si ajabu wewe si mkatoliki.
 
Back
Top Bottom