Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Namba 9 ina maajabu !
Upande moja inonekana ni 6 lakini upande mwingine ni 9.
Maisha yenye furaha ni mindset ya kila mtu alivyojitengenezea !!
Wapo watu wanayafurahia maisha huko Korea na wapo watu wanayachukia maisha huko USA !
Watu wanahama kutoka Korea Kaskazini, Cuba kwenda Marekani ila sio kinyume chake
Hata Wahamiaji kutoka Afrika wanata kwenda nchi za kibepari na sio za kijamaa
 
Ninachokiona hapa ni chuki dhidi ya Nyerere na ujamaa wake...

Malcom ningekushangaa kama ungemsifia Nyerere na ujamaa wake ili hali wewe ni bepari

Haiwezi tokea ...

Ninachokijua ni kuwa Nyerere hakua malaika, alikua binadamu mwenye mazuri na mabaya...

Kwa msingi huo sidhani kama ni sawa kumweleza Nyerere kwa mabaya huku mazuri tukiyafumbia macho...

Kwa kutumia itikadi ya ujamaa Nyerere aliweza kutufanya watanzania tujione ni ndugu licha ya tofauti za makabila...

Ujamaa uliwafanya watanzania kusoma bure na kutibiwa bure kama nakosea naruhusu kukosolewa...

Ujamaa kama tusingeruhusu vita ya kagera nchi yetu ingekua mbele ya nchi zote za Afrika mashariki na kenya ikiwemo....

Huo ubepari unaoupigia kampeni sijawahi ona faida zake kwa nchi za Afrika, kama zipo zitaje.
Mkuu Ujamaa umeanza mwaka 1967, baada ya Tanzania kuzaliwa mwaka 1964 na umoja ulikuwepo. Kusema kwamba umoja wa kitaifa umeanza baada ya mwaka 1967 ni kosa la kimantiki. Sambamba na hili, unataka kuniambia Tanzania ya Ujamaa ilikuwa na umoja wa kitaifa kuliko taifa la kibepari la Ujerumani Magharibi au Tanzania ilikuwa na umoja wa kitaifa zaidi ya mataifa ya kiarabu yanoyoishi kifalme kama Saudi Arabia na UAE ?​
 
Nyerere alishaondoka duniani na madarakani, Leo tuna rais mwingine ambaye tatizo la umeme ameshindwa kutatua, wakati wa Nyerere hakukuwa na mgao wa umeme Tena tulikuwa na viwanda vikubwa.
Badala ya kupambana na Nyerere pambana na Ras wako anayekuletea mgao Hadi kipindi Cha mvua.
Mgao ulikueko wa umeme,wa chakula,wa mavazi,wa dawa za hospital,shule zilikuwa chache za mgao pia.Hakuna TV,wakati Znz na Kenya zipo.Barabara mbovu,magari hakuna.Petrol,diesel,mqfuta ya taa ya mgao.Sabuni za kufulia na kuogea hakuna.Dawa za meno hakuna,sanda za kuzikia kwa waislamu ilikuwa hakuna,nguo za kuvyaa hakuna.Sare za shule hakuna.Chaki,kalamu,madaftari,ni ya mgao.Kila kitu ni mgao .
 
Huwa najiuliza sana lakini sipati majawabu, lakini naomba wasomi wa humu ndani mnisaidie.

Hivi Mzee Nyerere alikuwa ana roho ya namna gani kuona mambo kama haya yakitokea kwa wananchi lakini bado hataki kubadilika na akaendelea kutumia mkono wa chuma kuhakikisha anasigina kabisa uwezo binafsi wa mtanzania kuweza kujikwamua kiuchumi. Ujamaa wa Tanzania hakuleta matokeo yoyote makubwa na ya kuchangaza ukilinganisha na kule Asia na Ulaya ambako walau walifanya mapinduzi ya sayansi na teknolojia.

Uchina walifanikiwa sana baada ya Raisi Deng Xiaping kuanza kuwaonea huruma raia wake akifahamu kabisa kwamba njia waliyokuwa wanaenda ilikuwa siyo sahihi. Aliruhusu watu waanze kumiliki mali zao binafsi na kufanya biashara. Najiuliza sana, miaka yote 18 ya Ujamaa, yalifanyika na kutokea mambo mengi mno kwa watanzania, kiasi kwamba kiongozi yoyote mwenye huruma na wananchi ni lazima angekaa chini na kujifanyia tathmini, lakini Raisi Nyerere hakufanya hivyo, aliendelea kuwa na moyo mgumu kama Farao. Hebu tuzingatie haya:

1. Sera ya utaifishaji wa mali, ilileta umasikini mkubwa sana kwa watu.
2. Kufuta vikundi ya ushirika (Cooperatives) na kuweka vile vya TANU kulididimiza mno sekta ya kilimo.
3. Kupiga marufuku watu binafsi kuagiza bidhaa nje ya Tanzania kulipelekea uhaba wa bidhaa na huduma muhimu.
4. Kuweka ugumu katika kusafiri (Travelling Restrictions) kulisababisha ukosefu wa ujuzi kwa watanzania.
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.

Mpaka kufika miaka ya 80's Ujamaa ulikuwa umefeli vibaya mno. Tanzania tulikuwa hatuna hata unga wa kupikia, mafuta, wala sukari. Mtaa mzima mlikuwa mnaenda kwa mwenyekiti kuomba sukari au sabuni kutoka maduka ya ushirika. Ukikamatwa na mafuta, sabuni au dawa za binadamu zilizolanguliwa kutoka Kenya lazima ushughulikiwe na dola. Kama ulisoma miaka ya 80's unaweza kukumbuka kwamba hata sare za shule zilikosa rangi, watu tukawa tunavaa vitu vya ajabu vilivyochakaa kama vile vichaa. Ukibahatika kukutana na wamishionari au taasisi za kidini ndiyo ulikuwa unaweza kupewa hata nguo, mahitaji na wazungu.

Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.

Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?​
Hovyo kabisa
 
Huwa najiuliza sana lakini sipati majawabu, lakini naomba wasomi wa humu ndani mnisaidie.

Hivi Mzee Nyerere alikuwa ana roho ya namna gani kuona mambo kama haya yakitokea kwa wananchi lakini bado hataki kubadilika na akaendelea kutumia mkono wa chuma kuhakikisha anasigina kabisa uwezo binafsi wa mtanzania kuweza kujikwamua kiuchumi. Ujamaa wa Tanzania hakuleta matokeo yoyote makubwa na ya kuchangaza ukilinganisha na kule Asia na Ulaya ambako walau walifanya mapinduzi ya sayansi na teknolojia.

Uchina walifanikiwa sana baada ya Raisi Deng Xiaping kuanza kuwaonea huruma raia wake akifahamu kabisa kwamba njia waliyokuwa wanaenda ilikuwa siyo sahihi. Aliruhusu watu waanze kumiliki mali zao binafsi na kufanya biashara. Najiuliza sana, miaka yote 18 ya Ujamaa, yalifanyika na kutokea mambo mengi mno kwa watanzania, kiasi kwamba kiongozi yoyote mwenye huruma na wananchi ni lazima angekaa chini na kujifanyia tathmini, lakini Raisi Nyerere hakufanya hivyo, aliendelea kuwa na moyo mgumu kama Farao. Hebu tuzingatie haya:

1. Sera ya utaifishaji wa mali, ilileta umasikini mkubwa sana kwa watu.
2. Kufuta vikundi ya ushirika (Cooperatives) na kuweka vile vya TANU kulididimiza mno sekta ya kilimo.
3. Kupiga marufuku watu binafsi kuagiza bidhaa nje ya Tanzania kulipelekea uhaba wa bidhaa na huduma muhimu.
4. Kuweka ugumu katika kusafiri (Travelling Restrictions) kulisababisha ukosefu wa ujuzi kwa watanzania.
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.

Mpaka kufika miaka ya 80's Ujamaa ulikuwa umefeli vibaya mno. Tanzania tulikuwa hatuna hata unga wa kupikia, mafuta, wala sukari. Mtaa mzima mlikuwa mnaenda kwa mwenyekiti kuomba sukari au sabuni kutoka maduka ya ushirika. Ukikamatwa na mafuta, sabuni au dawa za binadamu zilizolanguliwa kutoka Kenya lazima ushughulikiwe na dola. Kama ulisoma miaka ya 80's unaweza kukumbuka kwamba hata sare za shule zilikosa rangi, watu tukawa tunavaa vitu vya ajabu vilivyochakaa kama vile vichaa. Ukibahatika kukutana na wamishionari au taasisi za kidini ndiyo ulikuwa unaweza kupewa hata nguo, mahitaji na wazungu.

Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.

Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?​
Nchi yetu Ina baba wa taifa mmoja tu ambaye ni JK Nyerere. Dunia nzima inatambua kazi yake. Muache apumzike na kwasasa leta mada za kuhusu bomu la sasa na matapeli ya chama cha maigizo (CCM)
 
Sikuwepo duniani kipindi cha Nyerere,lakini kupitia maandiko mbalimbali unaweza kuona utawala ule ulikua na ahueni kwa wananchi licha ya changamoto mbalimbali zilizojitokeza.waliokuwepo enzi hizo wanasema hakukua na mgao wa umeme,elimu ilikua bora zaidi,huduma mbalimbali za kijamii pamoja na kwamba zilikua chache lakini zilitolewa kwa wakati na bila upendeleo wowote na tena kwa kiwango cha juu, utu wa Mtanzania ulikua ni kipaumbele cha serikali, serikali iliwajibika kisawasawa.je tujiulize miaka 38 sasa tangu Nyerere atoke madarakani zaidi ya kuongezeka majengo marefu kwenye miji mikubwa kama Dar nini cha maana serikali zilizopita zimefanya ambacho hakikufanywa na serikali ile ya Nyerere?
Kiongozi lazima awe na principles zake, kusimamia kile anachokiamini mpaka mwisho, kiongozi asiye na msimamo ndie chanzo cha kuyumba kwa taifa lolote hapa duniani, leo atashika hiki atakiacha, kesho atashika kile nacho atakiacha...

Kulalamika miaka yote ya Nyerere kuwepo madarakani halafu bado hali ya maisha ya mtanzania ikaendelea kuwa mbaya, kwangu sioni kama kuna mantiki yoyote, kwasababu siku zote mabadiliko hayaji kwa usiku mmoja, ni mchakato.

Sasa ndani ya kipindi hicho cha mchakato ndicho kinamfanya kiongozi aendelee kusimamia kile anachokiamini, akiamini atafikia malengo, kama kikija kuwa na matokeo tofauti hayo ni mambo ya kibinadamu, kwamba alikosea, na ndio maana akawapisha wengine.

- Lakini unaposema Nyerere hakuwa na huruma na watu wake unakosea, alikuwa na huruma kupitiliza.

1. Hakujilimbikizia mali yoyote, licha ya madini na kila aina ya rasilimali tulizonazo.

2. Aliwahi kukaririwa akisema; "kiongozi unapita barabarani, unaona hali ya mtanzania ilivyo mbaya, unajua hili ni jukumu langu kumuondoa hapo alipo".

3. Hakuna hata mtoto wake mmoja tunayesikia amewahi kuhusishwa na wizi/ufisadi wa aina yoyote.

Mpaka hapo naamini utapata picha Nyerere alikuwa kiongozi wa aina gani, kwamba licha ya sera yake ya ujamaa kufeli, lakini dhamira ya dhati ya kumkomboa mtanzania toka kwenye lindi la umasikini alikuwa nayo tofauti na ulivyoandika.

Above all, hivi umewahi kujiuliza baada ya Nyerere kuondoka madarakani nini kilifuatia?

Kilichofuatia ndicho kile ambacho Nyerere alikipiga vita na wewe unaonekana kukifurahia, binafsi nchi hii naamini hakuna mabadiliko yoyote ya maana kiuchumi zaidi ya kuwepo pengo kubwa kati ya walio nacho na wasio nacho, hili Nyerere na Sokoine ndio walikuwa wakilipinga.

- Hii kwangu ni sawa na kusema, licha ya kumuona Nyerere alifeli, lakini hata hao waliofuatia baada yake nao wamefeli pia, hatuna cha maana cha kujivunia, mgao wa umeme, ukosefu wa maji safi na salama, wanafunzi kukosa matundu ya vyoo shuleni na madawati, mambo ni mengi...

Labda uniambie tu kwa sasa unafurahia uwepo wa unga, sabuni, mchele na mahitaji mengineyo mitaani, lakini ukweli wa mambo ni kwamba, licha ya uwepo wa vitu hivyo, bado hali ya mtanzania kiuchumi ni mbaya na ndio maana mpaka leo bado wapo ndugu zetu vijijini wakisubiri kampeni zianze, ili wagaiwe t-shirts na kofia za CCM ziwastiri.

Hivyo kwangu, kumlaumu Nyerere kwa kufeli bila ya kunionesha yule aliyefaulu hapa ndani kwetu sikuelewi, na kutumia mifano ya nje kumhukumu Nyerere bila kunionesha nani aliyefuatia wa hapa ndani akafaulu, umemuonea, that's unfair comparison.

Unless uniambie mahitaji yetu siku zote yangebaki yale yale ya unga, mchele na sabuni kupatikana madukani, jambo ambalo kwangu halina mantiki, naamini mahitaji hubadilika kulingana na wakati, na pale unaposhindwa kuwapa watu wako kile wanachohitaji kwa wakati husika, basi umefeli, there is no way out.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Mgao wa umeme ulikuwepo.Maishs yalikuwa magumu.Barabara mbovu,magari ya abiria ilikuwa hamna.Chakula cha mgao,petrol,dipel,mafuta ya taa ya mgao.Mafuta,sabuni,nguo,Shida tupu.
 
Mkuu Eyce, Merry Christmas to you Brother,

Mzee Nyerere is a controversial, enigmatic, mysterious and polarizing figures. Wengi wanamkubali na wengine hawamkubali, hasahasa kizazi ambacho kiliyaishi makosa ambayo aliyafanya Mzee Nyerere. Huu ndiyo ukweli mchungu. Kukosea kila mtu anakosea hapa duniani, jambo ambalo linanitatiza ni kwamba hata baada ya kuiingiza Tanzania vitani dhidi ya Uganda na kuifilisi Tanzania, Raisi Nyerere hakukubali makosa na akaendelea kutumia mkono wa chuma kudhibiti watanzania ambao walionekana kutoridhika na ile hali. Kwanini hakutaka kubadilika hata baada ya kuona watanzania wako kwenye lindi kubwa la umasikini ambao ulisababishwa na sera zake?

Miaka mitano ya mwisho ya Mzee Nyerere ilijaa taharuki mambo ya kuogopesha kuwahi kutokea Tanzania. Wengi hawafundishwi lakini Tanzania ilipitia changamoto nyingi za kiusalama, na ziliondoka punde tu baada Mzee Nyerere kung'atuka madarakani. Hebu tupitishane kwa harakaharaka.

1. Utekaji wa ndege uliofanya na vijana waliotaka Raisi Nyerere ajiuzulu.
2. Mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa na maafisa wa jeshi waliotaka Raisi Nyerere auawawe.
3. Uasi kanda ya ziwa, maafisa wa kijeshi huko mkoa wa Mara walianzisha nchi yao iitwayo Jamhuri ya Chui.
4.Mzee Nyerere anamrudisha Waziri Mkuu Sokoine madarakani huku akilalamika kwa Samora kwamba wanapishana.
5. Kuna minong'ono kwamba kuna chama cha kisiasa kinataka kuanzishwa na kina mahusiano na taifa la Ujerumani Mashariki.
6. Harakati za kusaka wahujumu uchumi zinaanza ambapo chama kiligawanyika na Sokoine katishia hadi maaskofu.
7. Waziri Mkuu anauwawa kwa ajali, jambo ambalo siyo kawaida kwenye msafara wake. Postmertem haikufanywa.
8. Nyerere anazungukwa na wajanja kina Thabiti Kombo ambao wanamwambia Mwinyi akubali kuwa Raisi.

Watanzania ni watu wenye utulivu mno, ukiona hadi wamefikia hatua ya kutumia jeshi, vurugu na kukuzunguka kisiasa, suala zima la kukubalika kwa Mzee Nyerere linatutia wengi ukakasi. Mwishoni Mzee alishindwa kuidhibiti dola na chama, watu wakawa wanamfanyia hujuma waziwazi. Nini kilipelekea hili kutokea ?​
Merry Christmas brother

Ukitaka kupata jibu lako bhasi inabidi uutumie uongozi wa Hayati Magufuli ambaye alitaka kuleta aina ya uongozi ule ule wenye mlengo wa kumsiliza kiongozi mmoja na kama haitoshi kilichotokea katika uchaguzi wa 2020 ambao ulionesha dhamira ya wazi kurejesha mfumo wa chama kimoja bungeni.

Ni wazi Nyerere aliongoza taifa la watu wachache lakini wengi wao wakiwa hawana elimu, pia vyombo vya babari vilikuwa vichache, vinavyofika sehemu chache lakini pia vilivyoweza kudhibitiwa kirahisi. Hivyo, taarifa yoyote inayoleta uchochezi au alternative thoughts iliweza kudhibitiwa kiurahisi

Mfano mengi uliyoyaongea mimi nimesimuliwa na mzee wangu ambaye aliyaona first hand, si kwa vita ya Idd Amini, vuguguvu la mapinduzi ya kijeshi na hata hiyo jamhuri ya chui.

Hivyo, tu vinaweza kukuonesha ni kwa jinsi gani usambazi wa taarifa ulikuwa controlled na hivyo kuwafanya watu wachache waliofunguka kukosa power ya "ukweli na umoja" Ambao Magufuli alipata nao tabu kutokana na uwepo wa mitandao ya kijamii lakini pia watu wengi walioelimika.


Kingine Tanzania aliyoikuza Nyerere ni ile iliyorithishwa kutoka kwa ukoloni ambao kiongozi alikuwa ni Mungu mtu lakini pia kwa uhalisia mwingine, Tanzania ni religious and traditional society kwa kiasi kikubwa hivyo viongozi kama mapadre, masheikh na hata baba katika ngazi ya familia huwa right muda wote na hata wakikosea hawawezi kuwa questioned kwa sababu hiyo ni dalili ya kukosa adabu. Hii tu imetufanya tuwe ni taifa la watu waliokosa mitazamo huru je, vipi kwa enzi hizo ?.....

Kwa hiyo kabla ya kumuangalia Nyerere kama controversial figure ni vyema tukawaangalia watanzania pia maana humo ndipo jibu lako lilipo 🙏🏽
 
Huyu mzee ni wa motoni tu, jinsi alivyo tesa watu na akili zake za kimaskinini sidhani hata utukufu utampunguzia zambi. Magufuli alitaka kuja na system hiyo hiyo lakini mwenyezi mungu aliwapenda zaidi watanzania na akampumzisha milele.
 
Tanzania dependency ratio bado ni kubwa brother na hata ukiangalia kiwango kikubwa cha ajira na biashara kinategemea sekta isiyo rasmi ambayo ni hand to mouth. Kiufupi Tanzania tuna unproductive population na hata graduates bado wengi hawawezi kupambana katika mfumo wa dunia

Hiyo FDI ni sawal lakini impact yake kwa common mwananchi ni nini zaidi ya Capital inflow and profit outflows ya kutosha

Huko kwenye international market tunyamaze tu maana ukifikiria balance of trade unaweza kulia japo haishangazi maana hata toothpick tunaagiza

Kiufupi vya kujivunia vichache
Nakubali kwamba Tanzania kuna changamoto nyingi tu, niseme haya yafuatayo:

Mosi, Tanzania inaweza kutengeneza Healthiest Dependency Ratio kwasababu, watu wenye uwezo wa kufanya kazi (Working Age Population) ni wengi kuliko wale wasioweza kufanya kazi (Dependents). Hili ni tatizo la kisera ambalo serikali ikiwa makini inaweza kulimaliza kama Uchina walivyofanya. Injecting the youths into the Market, either through employment and self-employment. Tanzania imejaa vijana waliomaliza chuo kikuu wenye utaalamu mwingi ambao wanaweza kufanya kazi endapo watawezeshwa na kusaidiwa.

Pili, FDI ni muhimu na Tanzania ni nchi ambayo ni kivutio kikubwa. Hili mbona halina ubishi. Tatizo ni lilelile la kisera, kwamba tunafanyaje kuhakikisha kwamba watanzania wa kawaida wananufaika na uwekezaji kutoka nje, aidha kwa kupitia kodi, ajira, ujuzi na ushirikishwaji katika uwekezaji. Mpaka sasa faida haionekani kwasababu kuna sehemu panavuja na hatujasimama kidete kuhakikisha tunarekebisha. Mashirika mengi yanapewa Tax Holidays na mikataba ya uwekezaji ina changamoto kama ule wa bandari. Ila binafsi naamini leo hii tukiamua kukusanya kodi kwa mashirika yanayowekeza hapa nchini, hela ipo nyingi mno.

Tatu, kwenye biashara ya kimataifa sisi ni Commodity Based Economy bado hatujawa Industrial Based Economy au Financial Based Economy nadhani tuendelee kujikita huko ambako tuna Comparative Advantage. Soko la dunia ya leo linahitaji sana rasilimali za uzalishaji ambazo Tanzania inazo kwa wingi na zinaiuzwa kwa Benchmark Price. Tunaweza kufanya mambo mengi mno kupitia Bilateral Trade na tukafanikiwa vizuri sana, tatizo ni kwamba watu wanafanya maksudi kwasababu wanataka kupata mafungu ya kumi (Ten Percent).

Nne, viwanda vidogo-vidogo vya kutengeneza Toothpick vinaweza kuanzishwa nchini Tanzania hata kesho endapo tutaamua. Kipindi hiki inawezekana kwasababu watu wengi wana mitaji na ujuzi, na uwepo wa soko la ajira la bei nzuri (Cheap Labour). Tatizo tunarudi palepale, kwamba watu wananufaika wenyewe na hii hali.

Niseme tu, hakuna pesa ambayo inatengenezwa Tanzania isionekane. Pesa zipo lakini zinaingia mifukoni kwa watu ndiyo maana uchumi kweli unakua lakini wewe mtu wa kawaida huuoni kwasababu, watu wachache wanazitafuna na kujimilikisha nchi. Hili ndiyo changamoto yetu Tanzania.​
 
Nami nimepata mshangao wa kulitumia neno MTAKATIFU sijui anafanya dhihaka au nini. Kwa namna alivyo humu ndani jf na hiyo lugha anayotumia ndo hayo tunayosema madhaifu ya kibinadamu.
Mzee Nyerere atatangazwa MTAKATIFU, ni suala la muda tu. Kama mwaka 2015 Papa alimtangaza MTAKATIFU mkoloni, Junipero Serra aliyesaidia kusambaza ukoloni kule Marekani mnamo karne ya 18, sembuse Mzee wetu Julius Nyerere ambaye alisaidia mimilioni ya waafrika kupata uhuru? Ndiyo maana binafsi nishaanza kumuita MTAKATIFU mapema kabisa nikifahamu fika kwamba hakuna kitakachozuia kanisa Katoliki kufanya hivyo. Askofu Thomas Becket alikuwa hapendwi nchini Uingereza kwa mambo aliyoyafanya katika kukandamiza uhuru wa watu wa kisiwa kile, lakini hili halikuzuia Vatican kumpa UTAKATIFU.

Wanasema Roma locuta, Causa finita au nakosea ?​
 
Huwa najiuliza sana lakini sipati majawabu, lakini naomba wasomi wa humu ndani mnisaidie.

Hivi Mzee Nyerere alikuwa ana roho ya namna gani kuona mambo kama haya yakitokea kwa wananchi lakini bado hataki kubadilika na akaendelea kutumia mkono wa chuma kuhakikisha anasigina kabisa uwezo binafsi wa mtanzania kuweza kujikwamua kiuchumi. Ujamaa wa Tanzania hakuleta matokeo yoyote makubwa na ya kuchangaza ukilinganisha na kule Asia na Ulaya ambako walau walifanya mapinduzi ya sayansi na teknolojia.

Uchina walifanikiwa sana baada ya Raisi Deng Xiaping kuanza kuwaonea huruma raia wake akifahamu kabisa kwamba njia waliyokuwa wanaenda ilikuwa siyo sahihi. Aliruhusu watu waanze kumiliki mali zao binafsi na kufanya biashara. Najiuliza sana, miaka yote 18 ya Ujamaa, yalifanyika na kutokea mambo mengi mno kwa watanzania, kiasi kwamba kiongozi yoyote mwenye huruma na wananchi ni lazima angekaa chini na kujifanyia tathmini, lakini Raisi Nyerere hakufanya hivyo, aliendelea kuwa na moyo mgumu kama Farao. Hebu tuzingatie haya:

1. Sera ya utaifishaji wa mali, ilileta umasikini mkubwa sana kwa watu.
2. Kufuta vikundi ya ushirika (Cooperatives) na kuweka vile vya TANU kulididimiza mno sekta ya kilimo.
3. Kupiga marufuku watu binafsi kuagiza bidhaa nje ya Tanzania kulipelekea uhaba wa bidhaa na huduma muhimu.
4. Kuweka ugumu katika kusafiri (Travelling Restrictions) kulisababisha ukosefu wa ujuzi kwa watanzania.
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.

Mpaka kufika miaka ya 80's Ujamaa ulikuwa umefeli vibaya mno. Tanzania tulikuwa hatuna hata unga wa kupikia, mafuta, wala sukari. Mtaa mzima mlikuwa mnaenda kwa mwenyekiti kuomba sukari au sabuni kutoka maduka ya ushirika. Ukikamatwa na mafuta, sabuni au dawa za binadamu zilizolanguliwa kutoka Kenya lazima ushughulikiwe na dola. Kama ulisoma miaka ya 80's unaweza kukumbuka kwamba hata sare za shule zilikosa rangi, watu tukawa tunavaa vitu vya ajabu vilivyochakaa kama vile vichaa. Ukibahatika kukutana na wamishionari au taasisi za kidini ndiyo ulikuwa unaweza kupewa hata nguo, mahitaji na wazungu.

Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.

Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?​

Kumlaumu Mzee Nyerere kwa yale yaliyo tokea, ni kujificha nyuma ya kivuli cha uzembe na ujinga wetu. Aling'atuka mwaka 1985 alikufa mwaka 1999. Mpaka sasa ni miaka 38 tangu ang'atuke na miaka 24 tangu afe. Kwa kipindi chote hiki, kilichopita tukiona kuwa Nyerere ni sehemu ya matatizo yetu. Basi itakuwa kuna shida sehemu. Kwa sasa hatuwezi kusingizia ukoloni, vita vya Uganda, Nyerere nk. nk. kwa kutopiga hatua za kimaendeleo. Mchawi wetu tunamjua fika. Hatuwezi kuwa watumwa wa hisstoria, wakati mambo yanayotukwamisha kimaendeleo yako wazi kabisa.
 
Huwa najiuliza sana lakini sipati majawabu, lakini naomba wasomi wa humu ndani mnisaidie.

Hivi Mzee Nyerere alikuwa ana roho ya namna gani kuona mambo kama haya yakitokea kwa wananchi lakini bado hataki kubadilika na akaendelea kutumia mkono wa chuma kuhakikisha anasigina kabisa uwezo binafsi wa mtanzania kuweza kujikwamua kiuchumi. Ujamaa wa Tanzania hakuleta matokeo yoyote makubwa na ya kuchangaza ukilinganisha na kule Asia na Ulaya ambako walau walifanya mapinduzi ya sayansi na teknolojia.

Uchina walifanikiwa sana baada ya Raisi Deng Xiaping kuanza kuwaonea huruma raia wake akifahamu kabisa kwamba njia waliyokuwa wanaenda ilikuwa siyo sahihi. Aliruhusu watu waanze kumiliki mali zao binafsi na kufanya biashara. Najiuliza sana, miaka yote 18 ya Ujamaa, yalifanyika na kutokea mambo mengi mno kwa watanzania, kiasi kwamba kiongozi yoyote mwenye huruma na wananchi ni lazima angekaa chini na kujifanyia tathmini, lakini Raisi Nyerere hakufanya hivyo, aliendelea kuwa na moyo mgumu kama Farao. Hebu tuzingatie haya:

1. Sera ya utaifishaji wa mali, ilileta umasikini mkubwa sana kwa watu.
2. Kufuta vikundi ya ushirika (Cooperatives) na kuweka vile vya TANU kulididimiza mno sekta ya kilimo.
3. Kupiga marufuku watu binafsi kuagiza bidhaa nje ya Tanzania kulipelekea uhaba wa bidhaa na huduma muhimu.
4. Kuweka ugumu katika kusafiri (Travelling Restrictions) kulisababisha ukosefu wa ujuzi kwa watanzania.
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.

Mpaka kufika miaka ya 80's Ujamaa ulikuwa umefeli vibaya mno. Tanzania tulikuwa hatuna hata unga wa kupikia, mafuta, wala sukari. Mtaa mzima mlikuwa mnaenda kwa mwenyekiti kuomba sukari au sabuni kutoka maduka ya ushirika. Ukikamatwa na mafuta, sabuni au dawa za binadamu zilizolanguliwa kutoka Kenya lazima ushughulikiwe na dola. Kama ulisoma miaka ya 80's unaweza kukumbuka kwamba hata sare za shule zilikosa rangi, watu tukawa tunavaa vitu vya ajabu vilivyochakaa kama vile vichaa. Ukibahatika kukutana na wamishionari au taasisi za kidini ndiyo ulikuwa unaweza kupewa hata nguo, mahitaji na wazungu.

Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.

Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?​
Ahsante sana mleta mada. Kiujumla nami pia nachangia mada hii kwa kuangazia hali halisi iliyokuwako kwa wakati huo wa miaka ya 1980 na katika uchangiaji wangu nitaangazia maeneo matatu. Maeneo hayo ni elimu, idadi ya watu na uchumi wa nchi kwa wakati huo.

Naanza na elimu; Kwangu Mimi neno elimu ninalifahamu kuwa ni uwezo wa kimaono ambao mtu anao na uwezo huo ni lazima uwe na tija kwa mtu mmoja mmoja na jamii kiujumla. Sasa wakati wa Mwalimu watu wenye uwezo wa kuchambua mambo kwa undani walikuwa wachache sana ukilinganisha na nchi ya Uchina.
Pili ni ukosefu wa elimu ya kiukombozi kwa watanzania ndio ilikuwa sababu kubwa ya kushindwa kuufahamu uwezo wa kiongozi wao. Kiongozi wao alikuwa anauwezo mkubwa kimaono ila kwa baadhi ya raia wake uwezo ulikuwa ni wa kiwango cha chini. Jambo hili la uwezo mdogo lilipelekea kufeli baadhi ya sera na mikakati ya kiuchumi iliyokuwa ifanyike. Kwa mfano; kuna baadhi ya mambo nchi inapaswa kufanya yenyewe na yaliyojuu ya uwezo wake inahitaji isaidiwa kutoka kwa nchi au mataifa mengine. Sasa kwa Tanzania kwa wakati ule ilikuwa inakwenda kufanya yale yaliyokuwa yakiwezekana kwa nchi ili iweze kupiga kasi ya kimaendeleo. Lakini ikiwa safarini kuna baadhi ya wasafiri walianza kuujumu jitihada za nchi kwa kuanza kupenda bidhaa za nje ya nchi zaidi ya zile zinozalishwa ndani. Jambo ambalo lilikuwa ni kama kuuza ajira za watanzania na kuajili wenzetu.

Kiuchumi pia kwa wakati huo wa sera za kiujamaa nchi yetu haikuwa imara sana na hii ilikuwa inajidhilisha wazi kwa kuangalia miundombinu yetu haikuwa bora kiwango cha kuchangia maendeleo kwa kasi. Kwa mfano; nchi ilikuwa ikitegemea vifaa na baadhi ya mashine kutoka n'gambo. Na kwa kuwa nchi ambazo zilikuwa zikiiuzia mitambo na mashine Tanzania, nazo pia zilikuwa zinaingalia Tanzania kama soko. Sasa zilipoona Tanzania inakwenda kujikwamua zilianza kuweka vikwazo kwa Tanzania na vikwazo vililenga sekita ya viwanda jambo ambalo lilipelekea nchi kushindwa kupata baadhi ya vipuli kwa ajili ya matengenezo ya mitambo na kwa sababu hiyo sekita ya viwanda iliyumba.

Idadi ya watu; Tanzania kwa wakati huo ilikuwa na rasilimali watu kidogo ukilinganisha na Uchina. Jambo hili lilipelekea uchumi wa nchi kukua kwa kasi ndogo.

Mwisho napenda kuishauri serikali kuwa tayari kubadilika kuendana na nyakati. Kwa mfano nchi ya Uchina sasa iko katika uchumi jumuishi na awali ilikuwa socialist country.
 
We jamaa ni mtu wa ajabu sana.
Hapo uko hai na matatizo yote mnayaona Live.
We unakurupuka kumlaumu Nyerere.
We hiyo hali hapo nchini huioni saa hii.?
Nyerere tena anahusikaje?
Aisee kuna watu wa ajabu sana humu duniani.
This thread is for research purposes only, but you are welcome to digress it with a spectacle of personal interpretation.​
 
Kumlaumu Mzee Nyerere kwa yale yaliyo tokea, ni kujificha nyuma ya kivuli cha uzembe na ujinga wetu. Aling'atuka mwaka 1985 alikufa mwaka 1999. Mpaka sasa ni miaka 38 tangu ang'atuke na miaka 24 tangu afe. Kwa kipindi chote hiki, kilichopita tukiona kuwa Nyerere ni sehemu ya matatizo yetu. Basi itakuwa kuna shida sehemu. Kwa sasa hatuwezi kusingizia ukoloni, vita vya Uganda, Nyerere nk. nk. kwa kutopiga hatua za kimaendeleo. Mchawi wetu tunamjua fika. Hatuwezi kuwa watumwa wa hisstoria, wakati mambo yanayotukwamisha kimaendeleo yako wazi kabisa.
Binafsi sijamlaumu Mzee Nyerere because a dead man tells no tales. Ninachofanya hapa ni kuuliza kwanini Mzee Nyerere na wajamaa hawakuwa na huwakuonesha kustushwa na hali ambayo watanzania tulikuwa tunapitia kipindi kile. Lengo lao haswa lilikuwa ni nini? Kuuliza haya maswali ni tofauti na kusema kwamba umasikini wa Tanzania chanzo chake ni Mzee Nyerere (There's life into this argument, thou I never brought this).

Mimi nachotaka hapa ni kufahamu historia na kueleweshwa The State of Mind of Nyerere and his acolytes wakati ule. Alikuwa anawaza nini yule mzee hadi kufanya vile alivyotufanya?​
 
Nafikiri pengine ni uchanga wa kuendesha nchi ambapo kwa namna moja ama nyengine kiongozi atakuwa tu too idealistic. Kwa mfano uliyotoa kwa nchi tuliyochukua sera zao za kiujamaa wenzetu civilisation yao ni kubwa kwa maana imejengeka kwa miaka mingi. Hivyo kutakuwa na namna kwa wao kuwa rahisi kubadilika.

Nimejaribu tu kuwaza.
Tangu mjadala wote uanze, hii ndiyo hoja ambayo inabidi itazamwe kwa undani zaidi. Aidha ni uchanga wa Nyerere, kwasababu alikuwa anafanya majaribio baada ya nchi kupata uhuru akiamini kwamba yuko sahihi. Hapa naona kuna hoja inakuja, japo linazaliwa swali jengine. Mbona kuna wengine ambao walikuwa ndiyo viongozi wa kwanza lakini walifanikiwa sana? Mzee Nyerere alikosea wapi? Hili ni tatizo lake binafsi au Afrika yote?

Mwishowe narudi palepale, kwanini hakustuka hata pale alipoona nchi yote imetumbukia kwenye lindi la umasikini?​
 
Mgao ulikueko wa umeme,wa chakula,wa mavazi,wa dawa za hospital,shule zilikuwa chache za mgao pia.Hakuna TV,wakati Znz na Kenya zipo.Barabara mbovu,magari hakuna.Petrol,diesel,mqfuta ya taa ya mgao.Sabuni za kufulia na kuogea hakuna.Dawa za meno hakuna,sanda za kuzikia kwa waislamu ilikuwa hakuna,nguo za kuvyaa hakuna.Sare za shule hakuna.Chaki,kalamu,madaftari,ni ya mgao.Kila kitu ni mgao .
Hivi unajua kwanini mradi wa uzalishaji wa umeme wa bwawa la Nyerere haukufanyika kipindi like? Kuna mwislamu aliyekufa akakosa sanda? Hiyo rais wenu nchi imemshindwa anabaki kuwagawia vitu waarabu.
 
Binafsi sijamlaumu Mzee Nyerere because a dead man tells no tales. Ninachofanya hapa ni kuuliza kwanini Mzee Nyerere na wajamaa hawakuwa na huwakuonesha kustushwa na hali ambayo watanzania tulikuwa tunapitia kipindi kile. Lengo lao haswa lilikuwa ni nini? Kuuliza haya maswali ni tofauti na kusema kwamba umasikini wa Tanzania chanzo chake ni Mzee Nyerere (There's life into this argument, thou I never brought this).

Mimi nachotaka hapa ni kufahamu historia na kueleweshwa The State of Mind of Nyerere and his acolytes wakati ule. Alikuwa anawaza nini yule mzee hadi kufanya vile alivyotufanya?​

Kwa kipindi kile lile alilofanya lilisaidia kwa nyakati zilezile. Kimsingi alikuwa sahihi. Umoja na amani yetu miongoni mwetu, ndicho kikubwa alichotaka kukifikia. Hayo matatizo yaliyojitokeza zilikuwa ni changamoto tu za kufikia malengo hayo.
 
Nchi yetu Ina baba wa taifa mmoja tu ambaye ni JK Nyerere. Dunia nzima inatambua kazi yake. Muache apumzike na kwasasa leta mada za kuhusu bomu la sasa na matapeli ya chama cha maigizo (CCM)
Usijali kabisa, mafisadi lazima lazima yaguswe. Hakuna jiwe ambalo litasalia juu ya jiwe. Ukweli ndiyo utatuweka huru, kwamba mbali na sifa zote ambazo marehemu Baba wa Taifa kama unavyomuita anapewa, ni lazima ukweli kwamba kuna sehemu alikosea sana usemwe. Hili ni muhimu ili vizazi vijavyo vijifunze na kutorudia makosa yaleyale.

Waungwana husema hivi, those who do not learn from history are doomed to repeat it's mistakes.​
 
Nyerere alishaondoka duniani na madarakani, Leo tuna rais mwingine ambaye tatizo la umeme ameshindwa kutatua, wakati wa Nyerere hakukuwa na mgao wa umeme Tena tulikuwa na viwanda vikubwa.
Badala ya kupambana na Nyerere pambana na Ras wako anayekuletea mgao Hadi kipindi Cha mvua.

Hili la viwanda wengi, hususan vijana hawalijui. Kuna kipindi Tanzania iliwahi kuwa nchi ya viwanda.
 
Back
Top Bottom