Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Wee chalii akili huna sasa uongozi na masuala ya dini yana uhusiano gani ? Pumbavu
Vinahusiana inawezekana akili huna na pengine hujui kwamba sio tuu dini inaweza athiri tabia na mwenendo Bali hata Jinsia.

Sisi wachumi tuna somo linaiywa behavioral economics,Sasa wewe mbumbumbu huwezi jua hili.

Hata kama huna akili kwani huwezi chunguza miendendo ya Mwingi,JK,Samia vs Kambarage, Mwendazake na Mkapa?
 
Vinahusiana inawezekana akili huna na pengine hujui kwamba sio tuu dini inaweza athiri tabia na mwenendo Bali hata Jinsia.

Sisi wachumi tuna somo linaiywa behavioral economics,Sasa wewe mbumbumbu huwezi jua hili.

Hata kama huna akili kwani huwezi chunguza miendendo ya Mwingi,JK,Samia vs Kambarage, Mwendazake na Mkapa?
Wewe ni mchumi ?🤡 Aiseeh hivi vichekesho. sasa Samia amefanya nini ewe chawa wake ?
 
Nakuelewa lakini wewe ambaye ni Mkubwa naomba unisaidie kutoa haya majawabu.

Mosi, Mzee Nyerere na Mzee Mtei walipishani kwasababu gani. Je, mambo aliyoshauri Mtei yalikuwa mabaya hadi Nyerere kuamua kumfanyia vile? Hivi Unadhani Mzee Nyerere angekubali kufanya mabadiliko miaka ya 70's unadhani nchi ingepitia kipindi kigumu kama kile cha miaka ya 80's?

Pili, nchi ilianza kudorora uchumi tokea mwaka 1980, kwanini Mzee Nyerere hakutaka kuchukua hatua zozote zile kusaidia wananchi waliokuwa kwenye lindi kubwa la umasikini, mpaka kusubiri mwaka 1984 baada ya Mzee Dr Salim kufanya ziara kule Lindi na kumwambia Mzee Nyerere kwamba hali ilikuwa ni mbaya. Kwanini miaka yote hii alikuwa hawaonei huruma watanzania?

Tatu, kwanini Mzee Nyerere alikuja kuzikubali sera zote alizozikataa (Japo siyo vigezo vyote vya SAP vilikuwa vinatekelezeka), alizisaini mwaka 1984 na zikaanza kutekelezwa na Mzee Mwinyi. Kama sera zilikuwa ni mbaya kihivyo kwanini alizikubali baadaye ?

Nne, mbona Uchina alikioga mfumo wa Ujamaa walifanya mabadiliko mapema miaka ya 70's na hawakupata matatizo yoyote, zaidi zaidi walifanikiwa mno. Tanzania tulikuwa na uziada upi wa kuchelewesha mabadiliko kwa muda mrefu ilhali wananchi wakiwa wanapitia mateso?

Lengo lake haswa lilikuwa ni nini ?​
Uhitilafiano wa fikra ama mtazamo ni jambo la kawaida na haipaswi kuwa nongwa.

Katika maisha, na hasa hili lituhusu sisi watu tunaotafuta kujipambanua kimaendeleo, misiguano yetu ndiyo kipago cha mielekeo anuai ya maua ya ustawi.

Ndiyo, madaraka huja na 'upendeleo maalum' katika duru ama jukwa la muktadha wa ufanyaji maamuzi; na Mwalimu Nyerere hili alilifahamu vizuri kabisa na hata kaandika mawaidha na nasaha muafaka kuhusu hili katika kumbukumbu za khotuba na mitazamo kuhususiana na 'Uhuru na Maendeleo'.

Nchi-taifa changa yoyote ina mazingira yake ya kipekee yanayofanania katika kuziinua taasisi muafaka na kuasisi 'Umoja'.

Umadhubuti wa kuinuka nchi-taifa changa nalo pia ni tunda la misuguano na mivuatano ya ndani kwa ndani iliyoratibiwa, katika hili, kuna 'maarifa yake'--namna ya maarifa haya, humu umma haukidhi kuwa umejiandaa kupokea--ila kadiri inavyofaa maarifa haya yanaweza kuwasilishwa kidogo kidogo--kuweka kumbukumbu sawa.

La kuchukua katika muktadha huu yawa basi, si busara sana kuwajadili watu--ni bora kujadili fikra ama kuyatafakari maono.

Si kila jambo linatafakariwa kimaoni maoni...

Masuala ama mambo mbalimbali yanaweza kumulikwa na kubanguliwa vema ikiwa kuna uono na ufikirifu mifumo.

Kwa hivyo, unaweza kumuelewa vizuri Mwalimu Nyerere ikiwa lau una Uono na Ufikirifu Mifumo; mwaka 2023 na kusonga, tayari 'imperative', linalobidisha, umuhimu wa hili kutiliwa mkazo kwa umma wote na viongozi tayari limeshasimikwa.

Maisha ni maamuzi wakati wote, kwenye maamuzi kuna kuchagua--kuchagua na kujichagulia.

Nidhamu ya kuchagua na kujichagulia ndiyo kiini cha jamii mabadilikoni; hauwezi kula kitumbua na kubakia nacho... Kwa hivyo, ndivyo mwendelezo wa topolojia fikirifu 2.0 kwa kana vile Wabantu husema 'mshika mawili moja humponyoka'. Kuna mambo katika maisha ni kuchagua moja--kusuka ama kunyoa; watu wa mizizi si watu kusimika na kughairi... Kuona ukweli wa mambo kwa sura pana kunataka Imani, Tumaini na Pendo-Utumishi...

Kwa namna hii, kupanga ni kuchagua, na taifa la watu ni pembe tatu ya (1) Siasa za nchi-taifa, (2) Mipango na Utumishi, na (3) Uwezo na Utayari wa Jamii -- jamii mabadilikoni.

Ikiwa unataka kutathmni migongano ya fikra, uhasama ama 'demokrasia', ni vema utambue kuna matatu ya kujengea muktadha--Dira iliyopo ya Maendeleo, Elimu/Ufahamu/Utayari iliyopo miongoni mwa Jamii yote na 'Matamanio ya Wanajamii'. Kwa kuwa, matamanio ya wanajamii huakisika kwenye 'Siasa za nchi'--japo 'Elimu' inahusika sana, jamii ikiwa na Elimu haba/Kujitambua kuliko ni duni basi nyota yake husafiriwa na 'Wajanja'; Hapa ndipo linapoanzia jambo/suala mtambuka la usalama wa Jamii...

Usalama wa Jamii haukamilishwi na kikundi cha watu wachache, kuwaangalia wengi eti kama ulinzi na utetezi; usalama wa jamii ni tunda la mtu kujitambua yeye mwenyewe kwanza na vivyo hivyo kutambua mapana ya fanusi ya ustawi wake ili kulinda muktadha wa ustawi wake. Ni pale kunapokuwa na wadau wa kutosha wanarasmisha muktadha wao wa kulinda ama/kutetea mifumo ndiyo labda tunaweza kudai ipo taasisi ya usalama wa jamii--na tena hii, ikiwa imejitokeza kwa usahihi basi inakuwa ni mnyooko wa 'vijilansi', watu kuwa macho wakati wote kuanzia raia mwenyewe, ofisi za umma na mapana ya jamii kwa jumuiya zake zozote.

Mwalimu Nyerere, alikuwa ni lulu ya taifa changa la Tanzania kwa kuwa alizaliwa hasa kwa ajili ya hili -- hili la kuwa mwanataasisi anayekomaa kwa ajili ya kusudi la raia, ofisi za umma na mapana ya jamii kwa jumuiya zake zote zije kuwa na 'mwangaza halisi wa kujitambua'. Katika hili Mwalimu ana meriti kwa kila alililoazimia na kushiriki msimamo kama kiongozi-mwakilishi wa maslahi ya wote--waliojitambua, ambao hawajajitambua, waliokatashauri ama/hata bado kukata shauri juu ya 'UTU na Uhuru'--Liberiti.

Kwa watu wenye 'upeo', mdau huyu kwa kweli alitenda haki sana juu ya wito wake wa maisha... Kwa hivyo ipo namna ya kusoma matendo yake ili kukadirisha muktadha wa 'jaala yake binafsi' miongoni mwa 'jamii pana'--sasa haya ni mambo ya 'Dharma'...

Kuna namna ya kuyasoma matendo ya mtu na matendo ya mtu ili kutambua mbegu za mielekeo na stawi za jamii; hili ndilo linaweza 'kuondoa lawama' miongoni mwa wa wale wanaoweza kutaka ama kupenda kuhoji--hivi kwa nini Mwalimu aliamua hivi na si vile(?) Haya ni mambo ya Elimu 3.0... Kutumia Elimu 1.0, kila mtu atazungumza anachofikiri anajua na kumbe ni kasumba tu...

Kwa namna hii unaweza kutumia 'Trizania'--trizania ya 'Ontolojia ya Taasisi', 'Kujichagulia' na 'Usoshalisti wa Kiafrika' ili kutambua uthibiti, saburi na jitihada za kukadirisha nchi yenye misingi ya 'Haki na Usawa'. Katika hili ni vema kutambua, hata sasa hii nchi iko chini ya maono haya; figisu za walimwengu zimetufanya kuchutama tu kwa wakati--kambi ya 'Umoja' haisalitiwi, na basi usimuone kobe kainama...

Liberiti, Umoja na Amani ni adha ya waja wema katika kuiishi misingi ya taifa letu; lakini 'Umoja', kiufundi ni zao la 'Hekima'--na hapo hapo hekima ni Uhuru... Elimu 1.0, Elimu 2.0 na Elimu 3.0 ndiyo ufunguo wa 'Usalama wa Jamii'; pasi kubabaishwa na kasumba zozote za kusombwa na upepo wa Walimwengu wenye ghiriba.

Kwa namna hii, unaweza kufanya 'Mapitio Dawatini' ni namna gani kwa mfano kuyumbishwa kwa bei za mafuta miaka ya sabini na vita vya Uganda vililigharimu 'sanduku la hazina' la nchi hii... Pia unaweza kutazama kidiplomasia, kwa nini nchi za Skandinavia zilikuwa na imani kubwa na Unchi-Taifa yetu, na hata leo bado ni washirika muhimu sana... Kama kungekuwa na 'jukwaa fasaha la Elimu 3.0' basi hapa tungalizungumza hata namna gani kuna 'upacha' wa watu wa skandanavi na watu watanzania kiroho na jaala ya nchi-taifa...

Haya 'yakiotewa' ndiyo unaweza kubaini kwa nini kuifananisha 'nyota' ya Tanzania kwa mfano na China si 'jambo muafaka' hasa; China ina watu wenye asili ya tawala za 'udynasti'; hata kama wao miaka hiyo ya sitini walianza na namna ya unchi-dola unaotumia serikali yenye kufuata sera za ukomunisti, hili linanamna yake ya kukadirisha muktadha wa ontolojia ya taasisi na 'maamuzi-jamii'....

Upande ambao, humu itakuwa labda 'ajabu' kuotewa ni 'maarifa na mitazamo' ni namna gani mataifa huwa yana 'roho-kumbaizi'; ni namna gani hizi 'hupata uhai'. Hili ndilo linaweza 'kujibu' kiufundi mizungu, jamii 'zinagundishwa' na vitu gani ambavyo labda wanajamii wanatengenezwa kufungamana navyo....

Mambo ya fanusi jamii-nadharia migongano-muingiliano wa alama oanifu.
 
Jiulize na population ilikuwaje wakati huo relatively
Tanzania mpaka kufika mwaka 1964 ilikuwa na raia milioni 10. Hadi kufikwa mwaka 1985, Tanzania ndiyo nchi iliyoliwa inaongoza barani Afrika kuwa na idadi ya watu wengi wanaojua kusoma na kuandika (The Highest Literacy Rate) kwasababu watanzania wengi walipata elimu ya msingi. Hata hivyo elimu ilikuwa imekaa kama piramidi, wachache ndiyo waliweza kufika chuo kikuu. Wasomi waliokuwa wa elimu ya juu walikuwepo wachache sana nchini Tanzania hadi Mzee Nyerere akakiri hadharani na kutoa ile hotuba maarufu tuliyokuwa tunasomewa shuleni "THOSE WHO RECEIVE THIS PRIVILEGE" akikubali kwamba tulikuwa wachache na tuna kazi kubwa ya kusoma. Hence the term UNASEOMEA KIJIJI CHENYE NJAA.

Kama wasomi wangekuwa ni wengi kama unavyosema, basi sidhani kama Marehemu Mzee Israel Elinewinga angeanzisha The Quota System ambayo ilisaidia baadhi ya mikoa ilyokuwepo nyuma kusoma. Bila hivyo shule tungekuwa nazo sisi Wahaya, Wanyakyusa na Wachagga maana ndiyo tulikuwa tumeelimika kuliko makabila yote kwasababu mkoloni aliwekeza sana kwenye mikoa yetu. Miaka ya 80's hadi 90's, ilikuwa ukienda shule kama Ilboru unakutana na wanafunzi wengi wenye asili ya mikoa ya Singida na Mwanza. Hii yote ni POLICY OF QUOTA SYSTEM ili walau kila mtanzania apate elimu ya sekondari.

Kama Tanzania ingekuwa na fedha nyingi basi isingehangaika na THE QUOTA SYSTEM, ingepeleka wanafunzi wengi walau shule za ufundi. Tukifanya ulinganifu wa Literacy Rate vis-vis Demograph, mataifa kama South-Korea yalikuwa na idadi kubwa ya watu kuliko sisi Tanzania mnamo miaka ya 60's ambapo watu walikuwa wanafikia zaidi ya milioni 20, lakini ndani ya muda mfupi kuanzia mwaka 1975-1991 zaidi ya asilimia 86% ya raia wa Korea walikuwa wamesoma elimu ya juu (Higher Education). Wangeenda kwenye ile njia ya kina Kim Il Sung wa Korea Kaskazini ingekula kwao.

=========================================================================
Jambo muhimu kukumbuka: Tanzania yenye watu milioni 10 mwaka 1964, ilikuwa na mzigo mdogo kuliko Korea-Kusini yenye watu milioni 23 kwa miaka ya 1960's. Kufika mwaka 1991, asilimia 96 ya wanafunzi wa Korea waliopita elimu ya msingi walikuwa na elimu ya juu aidha chuo kikuu au mafunzo ya ufundi. Tanzania tulifanya vizuri sana kwenye UNIVERSAL PRIMARY EDUCATION, lakini kama sera za Uchumi zingefanikiwa basi watanzania wengi zaidi wangefika elimu ya juu bure kabisa. Hili hata leo hii linawezekana tukuamua kuacha kupiga siasa na porojo.
 
Uhitilafiano wa fikra ama mtazamamo ni jambo la kawaida na haipaswi kuwa nongwa.

Katika maisha, na hasa hili lituhusu sisi watu tunaotafuta kujipambanua kimaendeleo, misiguano yetu ndiyo kipago cha mielekeo anuai ya maua ya ustawi.

Ndiyo, madaraka huja na 'upendeleo maalum' katika duru ama jukwa la muktadha wa ufanyaji maamuzi; na Mwalimu Nyerere hili alilifahamu vizuri kabisa na hata kaandika mawaidha na nasaha muafaka kuhusu hili katika kumbukumbu za khotuba na mitazamo kuhususiana na 'Uhuru na Maendeleo'.

Nchi-taifa changa yoyote ina mazingira yake ya kipekee yanayofanania katika kuziinua taasisi muafaka na kuasisi 'Umoja'.

Umadhubuti wa kuinuka nchi-taifa changa nalo pia ni tunda la misuguano na mivuatano ya ndani kwa ndani iliyoratibiwa, katika hili, kuna 'maarifa yake'--namna ya maarifa haya, humu umma haukidhi kuwa umejiandaa kupokea--ila kadiri inavyofaa maarifa haya yanaweza kuwasilishwa kidogo kidogo--kuweka kumbukumbu sawa.

La kuchukua katika muktadha huu yawa basi, ni busara sana kuwajadili watu--ni bora kujadili fikra ama kuyatafakari maono.

Si kila jambo linatafakariwa kimaoni maoni...

Masuala ama mambo mbalimbali yanaweza kumulikwa na kubanguliwa vema ikiwa kuna uono na ufikirifu mifumo.

Kwa hivyo, unaweza kumuelewa vizuri Mwalimu Nyerere ikiwa lau una Uono na Ufikirifu Mifumo; mwaka 2023 na kusonga, tayari 'imperative', linalobidisha, umuhimu wa hili kutiliwa mkazo kwa umma wote na viongozi tayari limeshasimikwa.

Maisha ni maamuzi wakati wote, kwenye maamuzi kuna kuchagua--kuchagua na kujichagulia.

Nidhamu ya kuchagua na kujichagulia ndiyo kiini cha jamii mabadilikoni; hauwezi kula kitumbua na kubakia nacho... Kwa hivyo, ndivyo mwendelezo wa topolojia fikirifu 2.0 kwa kana vile Wabantu husema 'mshika mawili moja humponyoka'. Kuna mambo katika maisha ni kuchagua moja--kusuka ama kunyoa; watu wa mizizi si watu kusimika na kughairi... Kuona ukweli wa mambo kwa sura pana kunataka Imani, Tumaini na Pendo-Utumishi...

Kwa namna hii, kupanga ni kuchagua, na taifa la watu ni pembe tatu ya (1) Siasa za nchi-taifa, (2) Mipango na Utumishi, na (3) Uwezo na Utayari wa Jamii -- jamii mabadilikoni.

Ikiwa unataka kutathmni migongano ya fikra, uhasama ama 'demokrasia', ni vema utambue kuna matatu ya kujengea muktadha--Dira iliyopo ya Maendeleo, Elimu/Ufahamu/Utayari iliyopo miongoni mwa Jamii yote na 'Matamanio ya Wanajamii'. Kwa kuwa, matamanio ya wanajamii huakisika kwenye 'Siasa za nchi'--japo 'Elimu' inahusika sana, jamii ikiwa na Elimu haba/Kujitambua kuliko ni duni basi nyota yake husafiriwa na 'Wajanja'; Hapa ndipo linapoanzia jambo/suala mtambuka la usalama wa Jamii...

Usalama wa Jamii haukamilishwi na kikundi cha watu wachache, kuwaangalia wengi eti kama ulinzi na utetezi; usalama wa jamii ni tunda la mtu kujitambua yeye mwenyewe kwanza na vivyo hivyo kutambua mapana ya fanusi ya ustawi wake ili kulinda muktadha wa ustawi wake. Ni pale kunapokuwa na wadau wa kutosha wanarasmisha muktadha wao wa kulinda ama/kutetea mifumo ndiyo labda tunaweza kudai ipo taasisi ya usalama wa jamii--na tena hii, ikiwa imejitokeza kwa usahihi basi inakuwa ni mnyooko wa 'vijilansi', watu kuwa macho wakati wote kuanzia raia mwenyewe, ofisi za umma na mapana ya jamii kwa jumuiya zake zozote.

Mwalimu Nyerere, alikuwa ni lulu ya taifa changa la Tanzania kwa kuwa alizaliwa hasa kwa ajili ya hili -- hili la kuwa mwanataasisi anayekomaa kwa ajili ya kusudi la raia, ofisi za umma na mapana ya jamii kwa jumuiya zake zote zije kuwa na 'mwangaza halisi wa kujitambua'. Katika hili Mwalimu ana meriti kwa kila alililoazimia na kushiriki msimamo kama kiongozi-mwakilishi wa maslahi ya wote--waliojitambua, ambao hawajajitambua, waliokatashauri ama/hata bado kukata shauri juu ya 'UTU na Uhuru'--Liberiti.

Kwa watu wenye 'upeo', mdau huyu kwa kweli alitenda haki sana juu ya wito wake wa maisha... Kwa hivyo ipo namna ya kusoma matendo yake ili kukadirisha muktadha wa 'jaala yake binafsi' miongoni mwa 'jamii pana'--sasa haya ni mambo ya 'Dharma'...

Kuna namna ya kuyasoma matendo ya mtu na matendo ya mtu ili kutambua mbegu za mielekeo na stawi za jamii; hili ndilo linaweza 'kuondoa lawama' miongoni mwa wa wale wanaoweza kutaka ama kupenda kuhoji--hivi kwa nini Mwalimu aliamua hivi na si vile(?) Haya ni mambo ya Elimu 3.0... Kutumia Elimu 1.0, kila mtu atazungumza anachofikiri anajua na kumbe ni kasumba tu...

Kwa namna hii unaweza kutumia 'Trizania'--trizania ya 'Ontolojia ya Taasisi', 'Kujichagulia' na 'Usoshalisti wa Kiafrika' ili kutambua uthibiti, saburi na jitihada za kukadirisha nchi yenye misingi ya 'Haki na Usawa'. Katika hili ni vema kutambua, hata sasa hii nchi iko chini ya maono haya; figisu za walimwengu zimetufanya kuchutama tu kwa wakati--kambi ya 'Umoja' haisalitiwi, na basi usimuone kobe kainama...

Liberiti, Umoja na Amani ni adha ya waja wema katika kuiishi misingi ya taifa letu; lakini 'Umoja', kiufundi ni zao la 'Hekima'--na hapo hapo hekima ni Uhuru... Elimu 1.0, Elimu 2.0 na Elimu 3.0 ndiyo ufunguo wa 'Usalama wa Jamii'; pasi kubabaishwa na kasumba zozote za kusombwa na upepo wa Walimwengu wenye ghiriba.

Kwa namna hii, unaweza kufanya 'Mapitio Dawatini' ni namna gani kwa mfano kuyumbishwa kwa bei za mafuta miaka ya sabini na vita vya Uganda vililigharimu 'sanduku la hazina' la nchi hii... Pia unaweza kutazama kidiplomasia, kwa nini nchi za Skandinavia zilikuwa na imani kubwa na Unchi-Taifa yetu, na hata leo bado ni washirika muhimu sana... Kama kungekuwa na 'jukwaa fasaha la Elimu 3.0' basi hapa tungalizungumza hata namna gani kuna 'upacha' wa watu wa skandanavi na watu watanzania kiroho na jaala ya nchi-taifa...

Haya 'yakiotewa' ndiyo unaweza kubaini kwa nini kuifananisha 'nyota' ya Tanzania kwa mfano na China si 'jambo muafaka' hasa; China ina watu wenye asili ya tawala za 'udynasti'; hata kama wao miaka hiyo ya sitini walianza na namna ya unchi-dola unaotumia serikali yenye kufuata sera za ukomunisti, hili linanamna yake ya kukadirisha muktadha wa ontolojia ya taasisi na 'maamuzi-jamii'....

Upande ambao, humu itakuwa labda 'ajabu' kuotewa ni 'maarifa na mitazamo' ni namna gani mataifa huwa yana 'roho-kumbaizi'; ni namna gani hizi 'hupata uhai'. Hili ndilo linaweza 'kujibu' kiufundi mizungu, jamii 'zinagundishwa' na vitu gani ambavyo labda wanajamii wanatengenezwa kufungamana navyo....

Mambo ya fanusi jamii-nadharia migongano-muingiliano wa alama oanifu.
Maneno mengi lakini bila chochote cha maana. Bure kabisa.
 
Putting states in a monolith and then judging them will not spare the fallacy of generalization.

Hii tabia ya kupenda kulinganisha nchi za Afrika kwa kuziweka kwenye kundi moja kama mayai ni kichaka cha watawala wengi na wasomi wavivu kukwepa kuwajibika. Mazingira ya Tanzania ukilinganisha na nchi nyingine za Afrika yalikuwa na utofauti mkubwa sana hata kama mtalazimisha kufanana. Tanzania ilikuwa na nafasi ya kufanya vizuri pengine kuliko nchi nyingine zote za Afrika. Ukifiatilia vizuri utafahamu kwamba Tanzania ilikuwa na kila kitu kuweza kuwa tajiri zaidi ya nchi zingine zote hapa Afrika. Nyerere squandered the opportunity.​
Nyerere alikataa kuingia mikataba na makampuni ya kuchimba madini kwa sababu walikuwa wanatoa asilimia ndogo sana kwa Serikali !
Hapo ni kweli Nyerere squandered the opportunity !
Then wakaja wanaojua how to use apportunities wakaingia mikataba ya madini kwa spidi ya 5G kwa kusaidiwa kupewa 3% kama mgao wa faida kwa Serikali !!
Kweli Nyerere squandered apportunities !
Na Gesi nayo wenye kujua how to do with apportunities wakaingia mikataba chapchap !
Mwamba akaja akatuambia TUMEPIGWA 😱😱 !!

Kweli Nyerere alituchelewesha sana !!
 
Swala ni kwamba hakukuwa na haja ya kuingia ndani ya Uganda kupigana vita ili kumuondoa dikteta Idi Amin kwa lengo la kumrejesha rafiki wa Nyerere madarakani hali ambayo imepelekea nchi kufa kabisa kiuchumi hadi leo.
Hii point ina mashiko sana. !!
Maana sisi tuliokuwepo kipindi hicho na tulishiriki vita kwa namna moja au nyingine,
Tunakumbuka baada ya vita tuliambiwa hali ya uchumi ni mbaya na kwamba tujifunge mikanda kwa miezi 18,
Lakini baada ya muda mfupi kupita Waziri Mkuu Hayati Sokoine akatuambia huenda Mwalimu alikosea hesabu na kwamba tunatakiwa tufunge mikanda kwa miaka 18. !!
Na hivyo ndivyo ilivyokuwa mambo hayakwenda vizuri na Wakubwa wa Dunia wakatoa masharti kama tunataka tukopeshwe Dolari zao ni lazima tukubali kushusha thamani ya shilingi yetu !
Mwalimu alikataa kushusha thamani ya shilingi ya Tanzania !
Akaamua kung’atuka !!
Habari ndio hiyo kwa mukhtasari !!
 
Tanzania mpaka kufika mwaka 1964 ilikuwa na raia milioni 10. Hadi kufikwa mwaka 1985, Tanzania ndiyo nchi iliyoliwa inaongoza barani Afrika kuwa na idadi ya watu wengi wanaojua kusoma na kuandika (The Highest Literacy Rate) kwasababu watanzania wengi walipata elimu ya msingi. Hata hivyo elimu ilikuwa imekaa kama piramidi, wachache ndiyo waliweza kufika chuo kikuu. Wasomi waliokuwa wa elimu ya juu walikuwepo wachache sana nchini Tanzania hadi Mzee Nyerere akakiri hadharani na kutoa ile hotuba maarufu tuliyokuwa tunasomewa shuleni "THOSE WHO RECEIVE THIS PRIVILEGE" akikubali kwamba tulikuwa wachache na tuna kazi kubwa ya kusoma. Hence the term UNASEOMEA KIJIJI CHENYE NJAA.

Kama wasomi wangekuwa ni wengi kama unavyosema, basi sidhani kama Marehemu Mzee Israel Elinewinga angeanzisha The Quota System ambayo ilisaidia baadhi ya mikoa ilyokuwepo nyuma kusoma. Bila hivyo shule tungekuwa nazo sisi Wahaya, Wanyakyusa na Wachagga maana ndiyo tulikuwa tumeelimika kuliko makabila yote kwasababu mkoloni aliwekeza sana kwenye mikoa yetu. Miaka ya 80's hadi 90's, ilikuwa ukienda shule kama Ilboru unakutana na wanafunzi wengi wenye asili ya mikoa ya Singida na Mwanza. Hii yote ni POLICY OF QUOTA SYSTEM ili walau kila mtanzania apate elimu ya sekondari.

Kama Tanzania ingekuwa na fedha nyingi basi isingehangaika na THE QUOTA SYSTEM, ingepeleka wanafunzi wengi walau shule za ufundi. Tukifanya ulinganifu wa Literacy Rate vis-vis Demograph, mataifa kama South-Korea yalikuwa na idadi kubwa ya watu kuliko sisi Tanzania mnamo miaka ya 60's ambapo watu walikuwa wanafikia zaidi ya milioni 20, lakini ndani ya muda mfupi kuanzia mwaka 1975-1991 zaidi ya asilimia 86% ya raia wa Korea walikuwa wamesoma elimu ya juu (Higher Education). Wangeenda kwenye ile njia ya kina Kim Il Sung wa Korea Kaskazini ingekula kwao.

=========================================================================
Jambo muhimu kukumbuka: Tanzania yenye watu milioni 10 mwaka 1964, ilikuwa na mzigo mdogo kuliko Korea-Kusini yenye watu milioni 23 kwa miaka ya 1960's. Kufika mwaka 1991, asilimia 96 ya wanafunzi wa Korea waliopita elimu ya msingi walikuwa na elimu ya juu aidha chuo kikuu au mafunzo ya ufundi. Tanzania tulifanya vizuri sana kwenye UNIVERSAL PRIMARY EDUCATION, lakini kama sera za Uchumi zingefanikiwa basi watanzania wengi zaidi wangefika elimu ya juu bure kabisa. Hili hata leo hii linawezekana tukuamua kuacha kupiga siasa na porojo.
Nyerere alijitahidi sana kulingana na enzi zake. Kama binadamu alifanya makosa lakini kwa nia njema. Alikuwa kiongozi mwenye maono japo yaweza yasiwe sahihi ila yanajulikana. Tatizo letu sasa hatuna viongozi wanaofikIria nchi kwanza kabla kujifikria wao na familia zao. Matokeo yake tuna tabaka la wanasiasa matajiri sana kutoka chama tawala na wanafikiria zaidi kubaki madarakani kwa gharama yoyote ile kuliko kuimarisha uchumi wa nchi
 
Swala ni kwamba hakukuwa na haja ya kuingia ndani ya Uganda kupigana vita ili kumuondoa dikteta Idi Amin kwa lengo la kumrejesha rafiki wa Nyerere madarakani hali ambayo imepelekea nchi kufa kabisa kiuchumi hadi leo.
Hakukuwa na haja au kulikuwa na haja hilo sio swali. Swali ni kwa nini hali ya uchumi ilikuwa mbaya baada ya 1980, unanielewa hapo?😎
 
Nyerere alijitahidi sana kulingana na enzi zake. Kama binadamu alifanya makosa lakini kwa nia njema. Alikuwa kiongozi mwenye maono japo yaweza yasiwe sahihi ila yanajulikana. Tatizo letu sasa hatuna viongozi wanaofikIria nchi kwanza kabla kujifikria wao na familia zao. Matokeo yake tuna tabaka la wanasiasa matajiri sana kutoka chama tawala na wanafikiria zaidi kubaki madarakani kwa gharama yoyote ile kuliko kuimarisha uchumi wa nchi
Uungwana ni kukubali mambo ambayo wengine wanayaonea aibu. Hakuna mtu mwenye akili timamu hapa Tanzania atapuuza na kudharau mchango wa Mzee Nyerere kwenye maisha ya kila mtanzania. Tatizo ni kwamba jambo ambalo alikosea, UCHUMI lilikuwa na madhara makubwa kuliko sera zake nyingine alizowahi kuzikosea. Muhimu ni kufahamu:

1. Wapi alijikwaa ?
2. Kwanini alijikwaa ?
3. Mazingira yapi yalipelekea ajikwae ?
4. Wanaomzunguka walichangia kwa kiwango gani ajikwae ?
5. Madhara ya kujikwaa kwake yalileta shida gani kwa taifa lote ?
5. Waliomfuta walijifunza somo gani katika kujikwaa kwake yeye kama Raisi wa kwanza ?​
 
Hakukuwa na haja au kulikuwa na haja hilo sio swali. Swali ni kwa nini hali ya uchumi ilikuwa mbaya baada ya 1980, unanielewa hapo?😎
Sasa hujui nini hapo wakati pesa zote zilitumika kwenye hivyo vita na nchi ikafirisika na kukopa Nyerere akakataa masharti ya IMF/WB.
 
Yaani mimi baba yako unaniita kijana, haya ndio mapungufu ya hii mitandao ebu jaribu kucheki profile yangu.
Mimi ni BABA yako. Nimezaliwa kabla ya uhuru wa Tanganyika kwa hiyo funga mdomo wako tafadhali; au unataka nikujibu kwa ile ID yangu ya zamani?
 
Back
Top Bottom