Wakati nikiwa siwataki tena Makocha Gomez na Hitimana, Wafuatao upesi sana Wafukuzwe na Wasimamishwe Simba SC

Wakati nikiwa siwataki tena Makocha Gomez na Hitimana, Wafuatao upesi sana Wafukuzwe na Wasimamishwe Simba SC

Wale wachezaji wanastahili lawama 100% ni wazembe sana, nikisoma ulichoandika na aina ya magoli tuliyofungwa naanza vipi kukupinga kuwa wale wajinga wamekula pesa za watu?

Seriously kuna mafaza uchwara Simba SC wanatakiwa waondoke, huyo Manula akiwa mmoja wao, hili lisiachwe lipite, sio waende shirikisho wafuzu makundi halafu tusahau, hakuna, huu uzembe unatakiwa kushughulikiwa 100%

Na hao mabeki uliowaandika nao vile vile, hawafai, wamekaa Simba muda mrefu wanajiona wamekuwa mabosi, hawana tena fighting spirit uongozi wa Simba unatakiwa kuwapunguza wale wazee ikibidi kijengwe kikosi upya.

Wameifanya Simba SC imekuwa timu ya kipuuzi isiyotabirika hata kama wakiwa na ushindi wa aggregate ya 3-0!, wale watu wazima hawaijui game management? uchunguzi ufanyike wahujumu watupwe motoni bila kujali majina yao.
Ngoja hamsa hamsa zirudi tena
 
Kuna mpuuzi ana amini Simba ikienda shirikisho itafuzu makundi, Simba hii inakwenda kutia aibu na Haina ubavu wa kwenda makundi ya shirikisho.
Imeshaingia makundu no makundi
 
1. Meneja Patrick Rweymamu

2. Mratibu Abbas

3. Kipa Aishi Manula

4. Beki Shomary Kapombe

5. Beki Pascal Wawa

6. Nahodha John Boko

7. Kocha Selemani Matola

Ninaotaka wabakie tu katika Benchi la Ufundi ni Mfia Timu Kocha wa Viungo na Kocha wa Makipa ambaye nimehakikishiwa na Mtu wa ndani kabisa kuwa ameshasema mno kuwa Golini awe anakaa Beno Kakolanya ila hana Nguvu kwakuwa Kipa Aishi Manula anapendwa na Wakubwa huku wengine akila nao 10% za Posho na Mshahara wake.

Simba SC kwa sasa Ina Nuksi nyingi tu.

Cc: Frank Wanjiru
KUFUNGWA KUSIWE NDIO MAHARIBIFU YA MFUMO WA TIMU YA SIMBA,H APO NI MAHALI PA KUJIPANGA UPYA ZAIDI.
 
1. Meneja Patrick Rweymamu

2. Mratibu Abbas

3. Kipa Aishi Manula

4. Beki Shomary Kapombe

5. Beki Pascal Wawa

6. Nahodha John Boko

7. Kocha Selemani Matola

Ninaotaka wabakie tu katika Benchi la Ufundi ni Mfia Timu Kocha wa Viungo na Kocha wa Makipa ambaye nimehakikishiwa na Mtu wa ndani kabisa kuwa ameshasema mno kuwa Golini awe anakaa Beno Kakolanya ila hana Nguvu kwakuwa Kipa Aishi Manula anapendwa na Wakubwa huku wengine akila nao 10% za Posho na Mshahara wake.

Simba SC kwa sasa Ina Nuksi nyingi tu.

Cc: Frank Wanjiru
Kuhusu Manula tushike lipi?

 
Wale wachezaji wanastahili lawama 100% ni wazembe sana, nikisoma ulichoandika na aina ya magoli tuliyofungwa naanza vipi kukupinga kuwa wale wajinga wamekula pesa za watu?

Seriously kuna mafaza uchwara Simba SC wanatakiwa waondoke, huyo Manula akiwa mmoja wao, hili lisiachwe lipite, sio waende shirikisho wafuzu makundi halafu tusahau, hakuna, huu uzembe unatakiwa kushughulikiwa 100%

Na hao mabeki uliowaandika nao vile vile, hawafai, wamekaa Simba muda mrefu wanajiona wamekuwa mabosi, hawana tena fighting spirit uongozi wa Simba unatakiwa kuwapunguza wale wazee ikibidi kijengwe kikosi upya.

Wameifanya Simba SC imekuwa timu ya kipuuzi isiyotabirika hata kama wakiwa na ushindi wa aggregate ya 3-0!, wale watu wazima hawaijui game management? uchunguzi ufanyike wahujumu watupwe motoni bila kujali majina yao.
Uko shirikisho tutapita kwa njia gani?!hatuna timu ya maana hapo.
 
Kuna mpuuzi ana amini Simba ikienda shirikisho itafuzu makundi, Simba hii inakwenda kutia aibu na Haina ubavu wa kwenda makundi ya shirikisho.
Simba ina baadhi ya wachezaji wana shepu za kishoga, siyo fighters. Bwalya, sadio
 
Tatizo la Simba Kuna wachezaji ni mafaza, makocha uwezo wao mdogo, Gomes mpaka Sasa kashindwa kujenga timu pamoja na muda wote aliokuwa. Ametumia kikosi kilekile mbinu ileile wakati mwenzake amekuja na approach tofauti.
Hiyo stahili ya kuchezesha mfungaji mmoja imetufanya kila tukikutana na yanga tunafungwa.
Viongozi badala ya kufanya maandalizi wanatuletea kina mwijaku.
Usajili wa wachezaji ni mzuri ila makocha hamna kitu.
 
Simba imekuwa timu ya hovyo kuanzia kwenye management,CEO yeye anachojua ni kubana matumizi tu,amekosa mipango ya kudhibiti kambi ya timu,amevuruga utamaduni wa timu yetu,tunafungwa mechi zote kubwa kwa sababu ya ubishi wake.
Ameshauliwa mara nyingi kwenye mechi kubwa timu ikae kambini na ulinzi wa kambi uimalishwe,wachezaji wa timu wasipewe nafasi ya kurudi nyumbani muda wote wa kambi,na kambi iwe mafichoni ili kudhibiti hujuma,wachezaji wetu ni waswahili hawa hawajielewi wanaturubuniwa na wapinzani hata kwa ahadi ya kupewa pesa na vitu vingine, lakini CEO amekuwa mbishi na kujifanya yeye ni professional zaidi na pia amekuwa hataki wazee wetu na wataalamu wetu wa asili wapewe nafasi wafanye jambo lao maana mpira wa africa bila kujizatiti kwa mbinu zote utoboi!!

Matokeo ya ubishi wake ndio ameyaona sasa,mechi kubwa kuanzia ile ya utopolo, timu imekuwa inafanyia mazoezi bunju uwanja ambao hauna hata uzio,mashabiki wanajazana kuangalia mazoezi na mipango ya timu,na wachezaji wanakuwa huru tu,hawana udhibiti wowote matokeo yake tunagongwa tu kama walevi!!nakumbuka mechi ya simba na utopolo iliyofanyika kigoma baadhi ya viongozi wa bodi wakiongozwa na Simba wa yuda Mzee kaduguda,na Asha baraka walikataa kata kata mipango ya CEO wakagoma mpaka wakakabidhiwa timu waweke udhibiti wao kuanzia kambini na kweli isingekuwa wao uto walikuwa wanatuua tena.

Mechi ya ngao ya hisani CEO alishauliwa tena kuhusu kambi na udhibiti wake, akawa mbishi kweli kweli, matokeo yake tukayaona uto wakapenyeza mambo yao tukafa kimoja cha mapema,mpira una matokeo matatu ila mechi hii ya watswana Simba haikustaili kutolewa kwa namna yeyote ile,ubishi wa CEO na Magoli pamoja na mulam ng'ambi ndio umeleta aibu hii kwa taifa,tuliwashauli mapema tuingie kambini mafichoni maana kuna harufu ya hujuma,kuna kiongozi wa utopolo bwana senzo na watu wengine maadui wa Simba Said tuli, Mwenyekiti yule aliejiuzuru, na kiongozi mmoja wa benchi la ufundi,ambao wamekuwa na mawasiliano ya karibu na watu wa galaxy ambao walikuja hapa nchini siku moja baada ya Simba kutoka Botswana, kiongozi uyo wa benchi la ufundi akishirikiana na watu wa uto hasa senzo na mwanachama maslahi wa simba said Tully,kupiga simu kwa watu wa galaxy wakitaka wapewe kiasi fulani cha pesa ili kufanya hujuma,taarifa zote magoli na CEO walipewa ila wakazipuuzia kwa kusema tumeshapita kwakua tulishinda mechi ya uko kwao,ukweli hujuma zipo Simba.

Hata baada ya MO kutia mgomo kusaini mkataba na Azam TV baadhi ya wakurugenzi wa Azam wakishirikiana na kiongozi mmoja wa bodi ya ligi,walikutana mara kadhaa kupanga kuhujumu timu ya Simba ili ionekane timu ya kawaida tofauti na MO anavyojinasibu ili kumkomoa, mambo ni mengi mno na mara zote CEO amekuwa akishauliwa na wadau wafia timu ila amekuwa akipuuzia kwa kiburi chake tu.

Nafikili sasa akili itamkaa sawa,ataelewa soka la bongo limejaa utapeli na watu wapigaji tupu,wazee wa kuchukua muhamala,MO bahati nzuri ABC zote ameshazijua ndio maana aliona ni upuuzi kuwekeza kwa timu ambayo baadhi ya wanachama wakiongozwa na Tully Said,wakishirikiana na watu wa uto na kiongozi mmoja wa bodi ya ligi,kutengeneza mtandao wa hujuma ili timu ikwame kwa maslahi yao,mfadhili wa mpango huo ni mkwepa kodi maarufu nchini mwenye asili ya Yemen mwenye ushirikiano na mstaafu mmoja aliewahi kuwa namba moja nchini.
 
Kwa upande wangu naona Simba kuna matatizo makubwa na yasipoangaliwa kwa kina basi timu itaendelea kupata matokeo mabovu kwenye ligi na hata huko shirikisho.
1. Tatizo kubwa ni mshambuliaji wa kati. Tukatae tukubali kwa sasa hivi Simba haina mshambuliaji wa kati anayeweza kuamua matokeo. Boko na Kagere umri unawatupa na wana "footwork" mbovu kabisa. Wakituliza mpira chumba na sebule na hawajui kujipanga kwenye nafasi kabisa. Na hawana uwezo wa kupiga chenga na kuwatoka mabeki hata wawili. Kufunga mpaka wawekewe mpira kwenye njia. Pia uwezo wa kuwakaba mabeki wa timu pinzani wasianzishe mashambulizi yao nyuma hawana. Na hili tatizo lilikuwepo toka msimu uliopita lakini lilikuwa linafichwa na Chama na Miquisone ambao walikuwa wanafunga na kuwapa washambilaji pasi zamwisho. Chris Mugalu ni mshambuliaji aliyekamilika kila idara. Ana "footwork" nzuri sana, mwili jumba na ana nguvu sana kiasi hakuna beki anayependa kukutana naye uwanjani. Anajua jinsi ya kujipanga kwa nafasi na mara nyingi anajitengenezea nafasi za kufunga yeye mwenyewe . Ana weza 'kuhold" mpira kwa sekunde kadhaa mpaka wenzake wafike na ni mkabaji mzuri kiasi mabeki wa kati wa timu pinzani hawawezi kuanzisha mashambulizi kirahisi. Tatizo kubwa sana kwa Mugalu ni kule kukosa kwake magoli ya wazi kiasi ni ngumu sana kumvumilia. Nini kifanyike kwenye fowadi ya Simba? Simba iachane na mshambuliaji mmoja wa kimataifa wakati wa dirisha dogo kwa gharama zozote zile na ilete mshambuliaji mwingine mwenye matumizi mazuri ya kichwa na miguu yote miwili. Kwa washambuliaji wa ndani Simba itafute mrithi wa muda mrefu wa Boko kwani Boko hana zaidi ya misimu miwili mbele. Hapa wanaweza msajili Lusajo wa Namungo au kumpandisha Andrew Michael kutoka kikosi cha pili haya yakiwa ni malengo ya muda mrefu ya kumtafuta mrithi wa Boko.
2. Tatizo la pili ni benchi la ufundi. Hapa naungana na mlete mada kuwa benchi la ufundi ni shida kabisa kwani Simba ina wachezaji wazuri lakini benchi la ufundi limekariri tu baadhi ya wachezaji ndio lazima wacheze hata kama siku hiyo hawapo fiti. Benchi la ufundi linaonekana linakosa mbinu mbadala na halijui wakati gani timu ishambulie na wakati gani timu ipaki basi. Inaonekana kabisa hata pamoja na kutazama mechi za Galaxy na kucheza nao mechi ya kwanza kwao lakini bado lilikuwa halijui kama mshambuliaji aliyewatungua goli mbili jana kama ni hatari na siku zote huwa na anatokea benchi. Kwenye mechi ya kwanza aliingia kipindi cha pili na aliwakosakosa sana Simba. Halafu timu inaongoza goli tatu badala ya timu kupaki basi na kufanya mashambulizi ya kushtukiza wao wakafanya "sub" za kuwatoa wachezaji wenye kaliba ya ukabaji wakawa wanaingiza wachezaji ambao ni "attack minded". Matokeo timu ikakosa uwiano wa kukaba na kusambulia. na kilichoharibu zaidi ni kuendelea kucheza "open game" muda wote wa mchezo.
3. Manula kwa kweli anahitajika apumzike kwa muda kwenye mbao ndefu ili arudishe umakini. Kwa kawaida kabisa mipira yote ya juu ndani ya hatua sita ni kazi ya goli kipa. Lakini yeye sijui alipigwa ganzi ya nini kweye goli la pili. Na hata goli la tatu sijui kwa nini aliamua kuufuata mpira ambao hana uhakika wa kuudaka au kugonga uende mbali.
4. Beki wa kati naona benchi la ufundi limekariri tu lazima Wawa acheze kila mechi. Lakini ni mara nyingi sana Kennnedy "amewapprove wrong" kwenye ligi na hata mechi za kimataifa. Nafikiri kwa sasa Kennedy ameshaiva vya kutosha na ni wakati sasa Simba imuamini na ijiandae kuachana na Wawa mwishoni mwa msimu ili Simba ipate nafasi nyingine moja ya kusajili mchezaji wa kimataifa.
5. Benchi la ufundi sasa liachane na pasi fupi fupi libadili mfumo na kuanza kutumia pasi ndefu na mfumo wa moja kwa moja "direct football". Kwa sasa Simba haina zile "play station" mbili Chama na Miqusone kwa hiyo kulazimisha kutumia mfumo ule ule wakati umebakiwa na Bwalya peke yake haitwezekana. Mfumo utakaowafaa sasa ni kutumia pasi ndefu na mawinga ambao wamejaa hapo Simba.
6. Wachezaji wanatakiwa wapatiwe mtaalamu wa saikolojia wakiwa kambini kwani inaonekana morali yao imeshuka sana wakiwa uwanjani. Na Simba isione aibu kuwa na mtu ambaye atawapa mzuka wachezaji wakiwa kambini na hili Jamhuri Kiwelu analiweza sana au kama kuna mwingine mwenye uwezo huo atafutwe apewe hiyo kazi.
7. Na kwa kuwa benchi la ufundi halijui matumizi sahihi ya mchezaji Abdulswamad ambaye namuona kama msaidizi sahihi wa Lwanga kwenye ukabaji wa kutumia nguvu basi ni bora wamrudishe Kagera kwa mkopo akaendelee na maisha yake ya soka.
8. Mwisho ni wakati wa mafadha wa Simba wakina Manula, Shomari, Boko, Zimbwe, Morison na wengineo wawe wanatoke benchi ili wakukumbuke wajibu wao uwanjani. Hasa huyo Morison timu inahitaji ushindi yeye anapanda mpira na kupiga chenga ambazo hazina faida kwa timu na mashabiki wanashangalia.

Ni mtizamo tu.
 
Back
Top Bottom