Wakati tunaambiwa: "Chapa kazi, chukua tahadhari" Hali halisi ni hii...

Wakati tunaambiwa: "Chapa kazi, chukua tahadhari" Hali halisi ni hii...

Mfiaukweli

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2018
Posts
5,636
Reaction score
8,777
Mkakati - kama mtu anaweza kuuita hivyo- wa serikali ya awamu ya tano kupambana na COVID-19 kuwaambia watu "waendelee kuchapa kazi huku wakichukua tahadhari". Binafsi ninachokiona ni kuwa serikali hii imeamua kufuata falsafa ya "do-nothing-and-the-problem-will-go-away". Kwa nini?

1. Naomba mtu anieleweshe kazi watakaoichapa waajiriwa kwenye makampuni yaliyofungwa (na yanaendelea kufungwa) kwa mfano mahoteli, shule, kampuni za utalii, mashamba ya maua, kampuni za ndege za kukodi, tour guides etc, etc,etc. Sioni (na sijasikia) serikali ikianzisha jitihada zozote kuwezesha biashara hizi ziendelee kuendeshwa ili watu wachape kazi.

2. "Chukua tahadhari" ina maana gani in practice? Ni kunawa mikono na kuvaa barakoa pekee? Senegal wametangaza kutengeneza kifaa cha kupima uwepo au la maambukizi ya coronavirus ambacho gharama yake ni sawa na Dola moja ya Kimarekani, kwa nini tusivitumie ili tuweze kupima watu wengi zaidi ili kuepusha maambukizi mengine mapya?

Hatuwezi kuishi kama kisiwa na tukafanikiwa. Lazima tushirikiane na mataifa mengine kukabiliana na janga hili, vinginevyo tutazidi kutengwa.
 
Mbona kelele za corona zinaanza kuvuma upya?

Kwani vp?

Mnachokishuhudia huko mliko ni nini hasa?

Hebu wekeni picha na video, kama kimewaka upya tujue. Hii mambo ya dathilamu iz thefu halafu kumbe watu wanajipiga mitama ziwekeni wazi.
 
Mkuu huu mchezo hauhitaji hasira

Kujifungia Ndani hakumalizi corona, ni swala la muda tu kila Nchi itajiachia
"Senegal wametangaza kutengeneza kifaa cha kupima uwepo au la maambukizi ya coronavirus ambacho gharama yake ni sawa na Dola moja ya Kimarekani, kwa nini tusivitumie ili tuweze kupima watu wengi zaidi ili kuepusha maambukizi mengine mapya?"

Understanding the context usijibu kwa muhemko wa kumfurahisha mtu!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona kelele za corona zinaanza kuvuma upya?

Kwani vp?

Mnachokishuhudia huko mliko ni nini hasa?

Hebu wekeni picha na video, kama kimewaka upya tujue. Hii mambo ya dathilamu iz thefu halafu kumbe watu wanajipiga mitama ziwekeni wazi.
Tuma 1.7M kwanza
 
#do-nothing-and-the-problem-will-go-away.
Mfiaukweli yaani huzioni kabisa jitihada zetu za kupiga nyungu na kujifukiza?
Huoni tulivyo busy na kupima Kama oil Ina Corona?
Jaribu kuwa na appreciation, achana na watu hao waliochanganyikiwa wanaosema eti Tanzania 🇹🇿 ni kiwanda Cha kuzalisha virusi vya korona, hao ni mabeberu 🐐 🐐 tu, na sisi ni mambuzi majike a.k.a vimada wa mabeberu 🐐 🐐 ndio maana bila fedha zao sisi tunakufa
 
Unataka Raisi afanyaje kwa mfano wape ajira basi ww, pumba tupu unajishushia heshima kuna ndugu yako kafa kwa covid au unaropoka tu ili mradi kukuza mambo
 
Kuna mambo yanasikitisha sana...

Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...



Cc: mahondaw
 
"Senegal wametangaza kutengeneza kifaa cha kupima uwepo au la maambukizi ya coronavirus ambacho gharama yake ni sawa na Dola moja ya Kimarekani, kwa nini tusivitumie ili tuweze kupima watu wengi zaidi ili kuepusha maambukizi mengine mapya?"

Understanding the context usijibu kwa muhemko wa kumfurahisha mtu!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi utafiti wa miti shamba ya Madagascar umefikia wapi? Au ile tiba was for chato republic only
 
2026 na uhakika tutagundua makaburi ya halaiki kama rwanda.

Viongozi wote waliowelwa sasa wizara ya afya ni kuficha ukweli.

Nina wasiwasi mama samia anaweza asirudi oct 2020 kwa kusema ukweli.

Pia PM sina hakika naye japo amejitahidi kuwa kimya asimwushi bosi wake.


Idd amini ilifika wakati akafuta bunge.

Maendeleo ya nini kama watu wanakufa.
 
Naomba mtu anieleweshe kazi watakaoichapa waajiriwa kwenye makampuni yaliyofungwa (na yanaendelea kufungwa) kwa mfano mahoteli, shule, kampuni za utalii, mashamba ya maua, kampuni za ndege za kukodi, tour guides etc, etc,etc. Sioni (na sijasikia) serikali ikianzisha jitihada zozote kuwezesha biashara hizi ziendelee kuendeshwa ili watu wachape kazi.
Hiyo.ni asilimia.moja tu ya ajira
Kuna wakulima,mama liahe.na.baba lishe,qanachinga,wavuvi,wachimbaji n.k
 
Huu Ugonjwa Tunaweza Kuishi Nao Kama Ukimwi
Hivyo Ndugu Zangu Tuache Kutishana Tuchape Kazi
Ni propaganda kutumia usemi huu bila kutazama kwa mapana yake.

UKIMWI tunaishi nao ni kweli, ila jitihada zilizofanyika kuzuia maambukizi yake kwa kasi na madhara yaatokanayo na ugonjwa huu kwa mida wa zaidi ya miongo 3 ni kubwa mno.

Tulipoteza nguvu kazi kubwa sana Kama taifa kabla ya

Kupekeka elimu ya UKIMWI kwa watu wengi na makundi maalumu
Kupunguza unyanyapaa
Kuandaa sera na miongozo ya tiba za wagonjwa wenye UKIMWI
Kupatikana kwa dawa za kufubadha UKIMWI
Kupatikana kwa condoms
Kuandaa kwa sheria za usimamizi wa janga hili na mambo mbalimbali mtambuka .


Kwa upande wa covid-19 bado tuko mahala pagumu. Hadi Sasa

Hatuna chanjo dhidi ya COVID-19
Hatuna tiba mahususi
Hatuna huduma nzuri kwa wagonjwa critical wa Covid-19
Hatujawa na mfumo wa kisera wa kukabiliana na kuzuia maambukizi
Elimu na ushirika wa jamii ili kupambana na janga hili bado upo chini na jamii Bado haijahamua kubadilika

Ukweli ni kwamba kujifariji kwa misemo ya kuwa tujifunze kuishi na COVID-19 Kama magonjwa mengine ni sehemu ya propaganda ili kukwepa uwajibikaji




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo.ni asilimia.moja tu ya ajira
Kuna wakulima,mama liahe.na.baba lishe,qanachinga,wavuvi,wachimbaji n.k

Akili za ajabu hizi; kwa hiyo kwa kuwa ni asilimia moja (na sijui umejuaje kuwa ni kiasi hicho) basi hakuna haja ya kuokoa ajira zao, si ndio?
 
Unataka Raisi afanyaje kwa mfano wape ajira basi ww, pumba tupu unajishushia heshima kuna ndugu yako kafa kwa covid au unaropoka tu ili mradi kukuza mambo

Akili zako zinatosha kuvukia barabara na kuimba mapambio. Sio lazima uchangie kama huelewi kitu.
 
Back
Top Bottom