Wakati Ulaya wakikusanya kodi ya miaka 20 iliyopita, Tanzania Samia anauliza miaka iliyopita mlikuwa wapi, msikusanye

Wakati Ulaya wakikusanya kodi ya miaka 20 iliyopita, Tanzania Samia anauliza miaka iliyopita mlikuwa wapi, msikusanye

Mukulu wa Bakulu

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2014
Posts
4,051
Reaction score
12,954
Wakati mwingine unajiuliza kama kiongozi wetu anaelewa anachokifanya ama haelewi chochote kabisa.

Juzi rais akiwa Kagera akasema kodi inayopaswa kukusanywa ni ya mwaka mmoja nyuma tu, miaka ya nyuma mamlaka zilikua wapi. Hapo ndio palinifanya kujiuliza kama rais wetu ana ufahamu hata wa sawa na punje ya haradani kuhusu masuala ya kodi ama hana kabisa.

Leo kampuni kubwa ya Mcdonald, imelipishwa zaidi Tsh Trilioni 2.5 za Kitanzania huko Ufaransa baada ya kugundulika imekua ikikwepa kulipa kodi kwa miaka 14 iliyopita. Mcdonald walikua wanachakachua hesabu na kuonyesha faida kidogo ili kukwepa kodi kwa miaka yote hiyo.



Sasa unajiuliza, iwapo Ufaransa wenye mifumo iliyoendelea bado makampuni yanatumia ujanja kukwepa kulipa kodi ila yakigundulika yanapelekwa mahakamani ana yanakubali kulipa bila kupelekwa mahakamani, kwa Tanzania watu wanakwepa kulipa kodi kisha wanaenda kuomba kwa rais wasilipe na rais anasema wasilipe.

Taifa ambalo haliko thabiti kwenye kukusanya kodi na mfumo wa kodi inaingiliwa na wanasiasa haliwezi kwenda popote.

Hii ndio matokeo yake tunayoyaona sasa, Rais wetu kwa kua hataki watu walipe kodi basi mbadala wake ni mikopo tu, kukopa tu. Tumeona kwenye bajeti yeye anawaza kukopa tuu.

Ndugai alisema ipo siku hii nchi itapigwa mnada na huo ndio ukweli.
 
Mama asali anataka kumfurahisha kila mtu bila kuacha sheria zichukue mkondo wake. Hajui kuwa mkataba mkubwa sana baina ya serikali na waja wake ni kodi, yaani hilo siyo jambo la kufanyiwa mzaha.

Nchi nyingi ukigundulika kuwa ulificha taarifa za mapato yako ukalipa kodi chini miaka ya nyuma, utapigwa faini hadi 75% huku ukitakiwa kulipa kodi uliyokwepa pamoja na interest kwa muda wote huo.
 
Hajui (wala hajisumbui kutaka kujua) matakwa ya Tax Administration Act, Cap 438, ambayo Serikali yake kupitia TRA inao wajibu wa kuisimamia.

Kwa mujibu wa Sheria hii, statute of limitations ni miaka mitano. There is a five-year time limit for the TRA to adjust an income tax return filed by a taxpayer. The five years runs from the due date of filing the final tax return.

Sasa huyu anaropoka tu kadri akili yake inavyomtuma, kana kwamba TRA wanakusanya kodi kwa kutumia mchakato wowote wanaoupenda wao au anaoutamka yeye majukwaani.

Ni aibu kwamba nchi ya watu takribani million 60 inaongozwa na kiongozi kama huyu!
 
Shida ni kwamba mkuu huku kwetu haya yalifanyika kwa ushahidi wenye mashaka sana

Lengo halikuwa kukusanya kodi bali kuwakomoa baadhi ya watu

Hakuna nchi ambayo haina sheria za kodi zinazozipa mamlaka za kodi authority ya kukagua tax returns za miaka ya nyuma.
 
Wakati mwingine unajiuliza kama kiongozi wetu anaelewa anachokifanya ama haelewi chochote kabisa.

Juzi rais akiwa Kagera akasema kodi inayopaswa kukusanywa ni ya mwaka mmoja nyuma tu, miaka ya nyuma mamlaka zilikua wapi. Hapo ndio palinifanya kujiuliza kama rais wetu ana ufahamu hata wa sawa na punje ya haradani kuhusu masuala ya kodi ama hana kabisa.

Leo kampuni kubwa ya Mcdonald, imelipishwa zaidi ta Trilioni 2.5 za Kitanzania huko Ufaransa baada ya kugundulika imekua ikikwepa kulipa kodi kwa miaka 14 iliyopita. Mcdonald walikua wanachakachua hesabu na kuonyesha faida kidogo ili kukwepa kodi kwa miaka yote hiyo.



Sasa unajiuliza, iwapo Ufaransa wenye mifumo iliyoendelea bado makampuni yanatumia ujanja kukwepa kulipa kodi ila yakigundulika yanapelekwa mahakamani ana yanakubali kulipa bila kupelekwa mahakamani, kwa Tanzania watu wanakwepa kulipa kodi kisha wanaenda kuomba kwa rais wasilipe na rais anasema wasilipe.

Taifa ambalo haliko thabiti kwenye kukudanga kodi na mfumo wa kodi inaingiliwa na wanasiasa haliwezi kwenda popote.

Hii ndio matokeo yake tunayoyaona sasa, Rais wetu kwa kua hataki watu walipe kodi basi mbadala wake ni mikopo tu, kukopa tu. Tumeona kwenye bajeti yeye anawaza kukopa tuu.

Ndugai alisema ipo siku hii nchi itapigwa mnada na huo ndio ukweli.

Hujui unaongea nini na pia hujui rais anaongea kitu gani ni bora uombe kuelewesha kuliko kuamka na uzi wa kukosoa bila ya kuwa n maarifa ya hicho ulichotaka kukiongea.

TRA walikuwa na mchezo wa kubambikia watu kodi za miaka ya nyuma. Kaka yangu mfanyabiashara ya utalii alichomekewa malimbikizo ya kodi za miaka ya nyuma ya shilingi milioni 250 wakati ushahidi wa risiti aliwaonyesha watu wa kodi ya mapato.

Akalazimika kulipa mara mbili, ule ulikuwa ni uporaji wa kimfumo, ambao marehemu JPM alikubaliana nao pengine kwa kutaka pesa za kumalizia miradi aliyoanzisha.

SSH amesema makusanyo ya kodi yasiwe ni yale ya miaka mitatu au minne nyuma, hao TRA walikuwa wanafanya nini wakati wote huo.?. SSH hataki kukusanya kodi ya dhuluma, hayo madeni feki ya miaka ya nyuma ndio dhuluma zenyewe hizo.
 
Statute of Limitations ni miaka mitano!
Hata ushahidi wa malipo ukiwekwa mezani bado statute of limitations inakuwa na nguvu?. Dhuluma ni mbaya sana.

Zakayo mkusanya ushuru alitubu mbele ya Yesu, ufike wakati na nyinyi mjiulize kuhusu wizi na dhuluma mnazowafanyia raia wasio na mtetezi.
 
Wakati mwingine unajiuliza kama kiongozi wetu anaelewa anachokifanya ama haelewi chochote kabisa.

Juzi rais akiwa Kagera akasema kodi inayopaswa kukusanywa ni ya mwaka mmoja nyuma tu, miaka ya nyuma mamlaka zilikua wapi. Hapo ndio palinifanya kujiuliza kama rais wetu ana ufahamu hata wa sawa na punje ya haradani kuhusu masuala ya kodi ama hana kabisa.

Leo kampuni kubwa ya Mcdonald, imelipishwa zaidi ta Trilioni 2.5 za Kitanzania huko Ufaransa baada ya kugundulika imekua ikikwepa kulipa kodi kwa miaka 14 iliyopita. Mcdonald walikua wanachakachua hesabu na kuonyesha faida kidogo ili kukwepa kodi kwa miaka yote hiyo.



Sasa unajiuliza, iwapo Ufaransa wenye mifumo iliyoendelea bado makampuni yanatumia ujanja kukwepa kulipa kodi ila yakigundulika yanapelekwa mahakamani ana yanakubali kulipa bila kupelekwa mahakamani, kwa Tanzania watu wanakwepa kulipa kodi kisha wanaenda kuomba kwa rais wasilipe na rais anasema wasilipe.

Taifa ambalo haliko thabiti kwenye kukudanga kodi na mfumo wa kodi inaingiliwa na wanasiasa haliwezi kwenda popote.

Hii ndio matokeo yake tunayoyaona sasa, Rais wetu kwa kua hataki watu walipe kodi basi mbadala wake ni mikopo tu, kukopa tu. Tumeona kwenye bajeti yeye anawaza kukopa tuu.

Ndugai alisema ipo siku hii nchi itapigwa mnada na huo ndio ukweli.

Ukiona Taifa kiti cha uraisi mnashindana alafu anaibuka mtu hukuwahi muona popote basi juwa sikubza Taifa hilo mbeleni nisiku ngumu kuliko zile linapita sasa. Kiti cha Rais sio sio issue ya gender Kiti cha Rais nikiti kinahitaji mtu kweli mwenye uwezo na akili namsomi wa vitabu. Angalia Marais wote wanao tikisa dunia na mataifa yanayo tikisa dunia Rais kweli anakuwa Rais anajuwa vitu ndani na nje. Angalia Taifa nalioenda as role mode Israel hawa jamaa wanaisumbuwa dunia lakina hawaweki watu wakawaida pale juu. Muangalie huyu waziri mkuu wa sasa Nathan Benet hiyo brain ni hatari kwenye maswala ya ulinzi wa kimtandao na udukuzi yani hiyo brain kaa mbali nayo...
Angalia mifumo ya idara za hili taifa utakaa chini yani ni majitu yenye akili... Bakini kuwekena mtoto washangazi, mke na mashemeji kwenye mifumo ipo siku maji mtaita mma... Maana tuna leader ambao sio visionaries bali wana waza uchaguzi. Such leader they will kill silence this nation. Nakama watu hawajuwi kuwa hakuna kitu kibaya kama kuliuwa taifa kimfumo wakisiasa yani mtajikuta siku hata vita hamuwez pigana maana huna watu unawajomba mashemeji na wakwe kwenye system mataifa imara Rais hateuwi watu wakumpendezesha anateuwa watu wenye uzalendo hawajuwi kutaja muheshimiwa Rais mtukufu what what wanajuwa muheshimiwa Taifa langu yani wapo kwa ajili ya Taifa naukiwazinguwa wanakushusha. Sisi tuna idara yenyenguvu kuliko zote Rais. Haya. End
 
Hujui unaongea nini na pia hujui rais anaongea kitu gani ni bora uombe kuelewesha kuliko kuamka na uzi wa kukosoa bila ya kuwa n maarifa ya hicho ulichotaka kukiongea.

TRA walikuwa na mchezo wa kubambikia watu kodi za miaka ya nyuma. Kaka yangu mfanyabiashara ya utalii alichomekewa malimbikizo ya kodi za miaka ya nyuma ya shilingi milioni 250 wakati ushahidi wa risiti aliwaonyesha watu wa kodi ya mapato.

Akalazimika kulipa mara mbili, ule ulikuwa ni uporaji wa kimfumo, ambao marehemu JPM alikubaliana nao pengine kwa kutaka pesa za kumalizia miradi aliyoanzisha.

SSH amesema makusanyo ya kodi yasiwe ni yale ya miaka mitatu au minne nyuma, hao TRA walikuwa wanafanya nini wakati wote huo.?. SSH hataki kukusanya kodi ya dhuluma, hayo madeni feki ya miaka ya nyuma ndio dhuluma zenyewe hizo.
Do not fool people.
 
East Africa kuna hata kampuni 1 inayoifikia McDonald ?
Kampuni inayojivunia kuwa na Real Estates zenye thamani kubwa kuliko thamani ya Real Estates za Roman Catholic Church all over the world
Ukiwa na kampuni kama hiyo ktk nchi yako unaiachaje isilipe kodi ?

Anachofanya SSH ni kutengeneza tax base ili aweze kukusanya Tax kubwa. Na hicho utakigundua ktk muda wake mfupi amekusanya kodi kubwa bila ya makelel makubwa ==> UFANISI

Anachofanya SSH ni kujenga Confidence kwa Wafanyabiashara, wote humu ni mashahidi kwamba ilifikia wakati Wafanyabiaahara waliiahi kama digidigi nchi hii wali freeze Capital zao wakawa wanaishi kwa style ya "Wait and See Strategy"

Mfanyabiashara mwenye maghorofa 3 Kariakoo ukimlazimisha aishi ktk style hiyo yeye hana shida, maana ghorofa 1 litalipa ada, chakula na petrol la 2 litalipia School Fees, Outings na social obligations nyingine, na la 3 ataishi mwenyewe na familia zake

Shida kubwa itakuwa kwa nchi
1. Lazima atapunguza wafanyakazi

2. Lazima mzunguko wa fedha utapungua

3. Lazima uzalishaji utapungua hatimae GDP Itashuka

4. New Foreign & Local investors watakuwa discouraged.


All in all SSH ameamua vyema kuwa kiongozi ambaye sasa ni Matron wa Business Community

Ni msiba mkubwa ktk nchi kama yetu kuona bado kuna viongozi wanawaona Wafanyabiashara kama Wanyonyaji/Wezi/Wanaojipatia ulwa kwa njia za mkato badala ya kuwaona Wafanyabiashara kama Wadau wakubwa wa Maendeleo. Let's ignore Business Community at our own risks


Wakatabahu
 
Unaletewa hesabu 2015 unakaa nazo mpaka 2020 halafu unafanya examination ukikuta kuna upungufu wa kodi au kuna kakodi hakakulipwa unacharge riba kila mwezi kwa miaka mitano? HUU UJAMBAZI MAMA NASHUKURU ANAUKEMEA.

2020 Kuna mtu alipewa riba karibu M15 sababu ya kakosa ka auditor ka kuongeza Tsh 300,000 kwenye mishahara. Hilo kosa angeambiwa ndani ya mwaka mmoja asingeingia hiyo hasara mpaka kufunga biashara. Mtaji wenyewe unakuta M30 unampa mtu riba M15. Nusu ya mtaji.
 
Back
Top Bottom