Wakati wa Ujenzi wa Reli ya TAZARA zaidi ya Wafanyakazi 160 walifariki kwa ajali na magonjwa, kati yao Wachina walikuwa 64. Ujenzi ulihusisha Vibarua na Wahandisi 38,000 kutoka Tanzania na Zambia, pia timu ya Wataalam na Wahandisi 13,500 kutoka China.
Reli hiyo iliyojengwa kati ya Mwaka 1968 hadi 1975 kutoka Kapiri Mposhi (Zambia) hadi Dar es Salaam (Tanzania) ina urefu wa Kilometa 1860.
Siku ya kuwakumbuka watendaji mbalimbali walipopoteza maisha katika ujenzi wa reli hiyo huadhimishwa Aprili 1 ya kila mwaka.
Picha: Mtandao