Wakati wa uongozi Profesa Juma, Mahakama ilishindwa kusimama na wananchi dhidi ya udhalimu wa awamu ya 5

Wakati wa uongozi Profesa Juma, Mahakama ilishindwa kusimama na wananchi dhidi ya udhalimu wa awamu ya 5

Nchi hii salute yangu ni moja tu kwa wote waliowahi kuwa CJ,nayo ni kwa CJ Nyalali, huyu CJ he walk the talk, na mazingira kipindi kile yalikua magumu sana,mfumo wa Chama kimoja cha kisiasa, ila CJ Nyalali alihakikisha anasimamia haki na mahakama zili EARN RESPECT, huyu wa sasa ndio hopeless kabisa mlilia tumbo mkubwa, please go as sooner as possible
Hapo mtu wa kupewa sifa ni Nyerere kuwa alijua maana ya utawala wa sheria akamwachia CJ Nyalali uwanja wake wa kusimamia Katiba na sheria nchini. Katika utumishi Serikalini kama kuna jambo unatakiwa kufanya ambalo ni kinyume na Katiba, sheria au dhamira yako, unatafuta namna nzuri ya kujiuzulu kuliko kutumiwa kuumiza watu wengine. Hakuna wadhifa muhimu kuliko utu wako. Mtu huzaliwi ili uwe na cheo fulani lazima uchague kama hicho cheo kinakuza utu! Uamuzi huo ni wa binafsi!
 
Ni Jaji ambae ni mfano bora wa kuepukwa na jamii na aliyeacha taswira mbovu kabisa ya cheo chake!
Hafai kuitwa Mh. jaji kabisa huyu mtu! Na majaji wa namna hiyo Tz bado wapo wengi!
 
Back
Top Bottom