"Wakati watu wanalia kuhusu kikokotoo nilikuwa naona kawaida, sasa nimeona ukali wake" Mtumishi aliyeambulia 10M baada ya kustaafu miaka 33 Magereza

"Wakati watu wanalia kuhusu kikokotoo nilikuwa naona kawaida, sasa nimeona ukali wake" Mtumishi aliyeambulia 10M baada ya kustaafu miaka 33 Magereza

Mkombozi ni shamba tu! Maana yake shamba la bei poa, kinyumba cha gharama nafuu sana wenyewe wanaita SLOPE , weka solar .

Fuga kuku wa kienyeji, kipindi cha kilimo Lima kwa utaalam, mambo mengine muombe Mungu.
 
Acha hao mapolisi waijue CCM LIVE. tukiandamana bandari isiuzwe wako mstari wa mbele kuitetea CCM. Tukidai katiba mpya wanasema tunaleta vurugu.
Wacha wazisome namba.
Mapolisi wakumbuke kwamba mbunge akustaafu baada ya miaka mitano ya bila kusema chochote bungeni analipwa milioni Mia mbili sabini. (Kwa miaka mitano) polisi miaka 33 milioni ishirini.
Kudumu chama Cha mapunduzi.
 
Mm najuta sana, mkataba umeisha toka mwaka jana May, nafutalia pesa zangu lakin bilabila unaambiwa mpk miaka 55-60 wakati hata 40 sijafika mamaeeeeh
Ila mbunge anapata stahiki zake siku ya kuvunja bunge.

Tena haambiwi akalete cheti cha ushindi wake wala kitambulisho cha ubunge.

Ajabu mtumishi mnyonge baada ya kutumika miaka 30+ siku ya kufuatilia mafao uchwara anaambiwa apeleke barua ya ajira, barua ya kuidhinishwa kazini, kitambulisho cha NIDA na makaratasi lukuki kisha anasugua benchi kusubiria mafao kiduchu ya kikokotoo cha CCM.
 
Mkombozi ni shamba tu! Maana yake shamba la bei poa, kinyumba cha gharama nafuu sana wenyewe wanaita SLOPE , weka solar .

Fuga kuku wa kienyeji, kipindi cha kilimo Lima kwa utaalam, mambo mengine muombe Mungu.
Tatizo letu watanzania wengi tunadhani KILIMO ni rahisi, eti mtu umezeeka umestaafu ndio unatafuta shamba, kimsingi unatafuta kifo, hapa jf ukiigia jukwaa la kilimo ndio utaona baadhi changamoto za kilimo, ukitaka kulima anza kabla hujastaafu
 
Tatizo letu watanzania wengi tunadhani KILIMO ni rahisi, eti mtu umezeeka umestaafu ndio unatafuta shamba, kimsingi unatafuta kifo, hapa jf ukiigia jukwaa la kilimo ndio utaona baadhi changamoto za kilimo, ukitaka kulima anza kabla hujastaafu
Unajua, kikokotoo ni PIGO la ghafla toka serikalini, kutoka kutegemea 55,000,000/= halafu unakuja pata 10,000,000/= . Usipotuliza akili, usipopata faraja toka watu wako wa karibu haswa familia !! UTACHIZIKA/ STROKE itakunyemelea.

Ushauri wangu huo, eneo dogo nimefanya na naendelea kufanya!. Kilimo ninachokizungumzia hapo ni kile cha kukufanya uwe na chakula.

Mfano - mm mwaka jana nimelima eneo dogo sana hapa ninapoishi kama robo heka au pungufu ya hapo nimepata kama gunia 1, mwaka huu nategemea kulima kama heka 5 maana tayari nimepata uzoefu mkubwa. Maana nililima kwa kufuata ushauri mtandaoni nilipanda kwa mbolea tatizo nilisafiri hivyo mbolea ya kukuzia sikuweka yaani nilitakiwa DAP /UREA/CAN .

Hivi sasa nafuga kuku na ninao kuku wa kienyeji , pamoja na kanga, ifikapo mwezi wa Dec 2024 Kwa uwezo wa Mungu ntakuwa nimepiga hatua kubwa na kusahau kabisa mambo ya KIKOKOTOO maana kimeniumiza sana.

Pension yangu imebidi nimpe kadi binti yangu aliyeko CHUO KIKUU maana kanyimwa mkopo, ukizingatia nikiwa kazini nilimsomesha shule za kulipia.
 
Mara nyingi tunajiona tuko salama, tunafikiri mabadiliko, kanuni, sheria za kigandamizi zinazofanywa na watawala hazituhusu sisi hasa hawa watumishi wa uma; watu wa magereza, wanajeshi, maaskari police, watumishi wa almashauri, walimu, mahakimu n.k.

Hutashangaa kusikia kada hizi zikikemea wanaopinga kikokotoo kipya, hutashangaa kusikia wakiwapinga na kuwabeza wanaotaka katiba mpya, hutashangaa wakiwabeza wanaowauliza watawala dhalimu maswali magumu na ya msingi kuhusu kubinafsishwa kwa bandari zetu zote na baadhi ya misitu na hifadhi za wanyama. Kinyume utawasikia wakisema hao wana wivu, hawa ni wapinga serikali, hawa hawana akili, wametumwa na mabeberu, hakika watatuhalibia amani na upendo wa nchi yetu

Sasa leo yamemkuta aliyekuwa mtumishi wa Magereza ndugu Shamte (56) staff Surgent alipojikuta akiambulia kiinua mgongo (malipo ya pension ya kustaafu) cha shilingi 21 millioni badala ya shilingi 55 millioni aliyotarajia baada ya kuitumikia serikali kwa miaka zaidi ya 33.Mstaafu huyo aliyasema hayo baada ya kutembelea ofisi za Magazeti ya mwananchi juzi.

"Najiona mfungwa mtarajiwa baada ya kubakia na shillingi 10 millioni kwani shillingi 10 millioni nyingine zimekatwa baada ya kuwa nilikopa chama cha ushirika wa Akiba na Mikopo cha watumishi wa Jeshi la Magereza" alitoa masikitiko yake bwana Shamte akitumia mfano wa mateso ya watu aliokuwa akiwachunga kila siku wakati akifanya kazi gerezani, kwani anajua machungu ya kuwa mfungwa. "Nilitegemea nikanunue shamba la kulima mazao niweze kujisitili baada ya kustaafu sasa haiwezekani, sioni mbele maisha yatakuwaje" bwana Shamte akitoa sentensi kuashiria kukata tamaa ya maisha

"Wewe ndugu, utaratibu wa malipo ya pensheni halipi CGP, waziri husika au katibu mkuu, utalipwa kulingana na michango yako" hayo ndiyo majibu ya kifupi na kukatisha tamaa aliyopewa mtumishi mstaafu ndugu Shamte kutoka kwa wakuu wake baada ya kupata ujumbe wa kiasi atakacholipwa.

Swali la kujiuliza ni, je ? tuko akina Shamte wangapi? akina shamte ambao tunakubali kila kitu watawala wanachopitisha kwa manufaa yao, akina shamte tunaokuwa wa kwanza kuwanyooshea vidole wale wachache wenye akili timamu na uthubutu wa kuhoji haya mabadiliko dhalimu kwa niaba na manufaa yetu, utasikia hawana akili hao, utasikia wamechanganyikiwa hao, nakwambia utasikia wametumwa na wazungu , mabeberu. Wengi wetu tunafikili madhara ya sheria dhalimu , mabadiliko kandamizi haya hayatuhusu sisi, yanawahusu wale tu wanaolalamika.

Hakika bwana shamte amekumbuka shuka wakati kunakucha , amekumbuka jinsi alivyokuwa akiwadharau waliokuwa wakipinga kikokotoo kipya na pengine alishiriki kuwahadhibu walipopelekwa gerezani alikokuwa akifanya kazi, hakika alimalizia kwa kutubu na kusema "Wakati watu wanalia kuhusu kikokotoo nilikuwa naona kawaida,sasa nimeona ukali wake.

Swali la msingi ni, Je...? wewe na mimi tumejifunza nini katika kisa mkasa hiki cha mstaafu Shamte?
hali ni tete wacha watumishi wakomeshwe wanaikumbatia sana ccm,juzi mwalimu wa secondary mwandamizi kastaafu kaambulia milion 33 alitegemea 80,huku wakimuahidi kalaki 4 kila mwezi
 
Tatizo letu watanzania wengi tunadhani KILIMO ni rahisi, eti mtu umezeeka umestaafu ndio unatafuta shamba, kimsingi unatafuta kifo, hapa jf ukiigia jukwaa la kilimo ndio utaona baadhi changamoto za kilimo, ukitaka kulima anza kabla hujastaafu
Anza immediately ndani ya miaka miwili baada ya kuajiriwa
Baada ya miaka 5 huwazi hata mshahara
 
Hivi bro.. ukiona mtu mzima anatoa machozi usifikiri masihala, je unajua huyu jamaa alikuwa akipokea mshahara wa shilingi ngapi? je unajua ana watoto na wategemezi wangapi? umemsikia akisema alitegemea hela hii ya mkupuo anunue ka-shamba na kuanza kulima, kwa hiyo inawezekana hana nyumba hata kasehemu ka kujihifadhi.....je hako kaposho ka asilimia ngapi sijui ya average ya mishahara yake ya nyuma kila mwezi katatosha. kumbuka hata hako ka 10 millioni anasema kuna msururu wa wadai wanakasubilia na kenyewe.
Maisha ya askari walio chini ya wizara ya mambo ya ndani ni magumu haswa. Huyu Ssgt amewawakilisha wengi ambao wengi wao hawawezi kuongea kutokana na utumishi wao.
 
Pension ya kila mwezi ndio kitu gani mkuu?
Baada ya kustaafu kuna ile hela mkupuo, siju niite ya kikokotoo inayolalamikiwa, lakini kuna pesa unapata kila mwezi, wanadai ni robo ya mshahara wako wa mwisho, nimewahi kusikia kuwa Askari Wana utaratibu tofauti, sasa ndio maana nikauliza, kuna wadau wakanishambulia, ndo nikawa mpole!!!
 
Baada ya kustaafu kuna ile hela mkupuo, siju niite ya kikokotoo inayolalamikiwa, lakini kuna pesa unapata kila mwezi, wanadai ni robo ya mshahara wako wa mwisho, nimewahi kusikia kuwa Askari Wana utaratibu tofauti, sasa ndio maana nikauliza, kuna wadau wakanishambulia, ndo nikawa mpole!!!
Ni vyema kuuliza kwanza kabla ya kutoa maelezo kama vile Jambo unalifahamu vizuri. Hapa ukumbuni wapo watu wenye uwelewa na kada mbalimbali mkuu. Usijari lakini utaelezewa na kuelewa hapahapa
 
Mara nyingi tunajiona tuko salama, tunafikiri mabadiliko, kanuni, sheria za kigandamizi zinazofanywa na watawala hazituhusu sisi hasa hawa watumishi wa uma; watu wa magereza, wanajeshi, maaskari police, watumishi wa almashauri, walimu, mahakimu n.k.

Hutashangaa kusikia kada hizi zikikemea wanaopinga kikokotoo kipya, hutashangaa kusikia wakiwapinga na kuwabeza wanaotaka katiba mpya, hutashangaa wakiwabeza wanaowauliza watawala dhalimu maswali magumu na ya msingi kuhusu kubinafsishwa kwa bandari zetu zote na baadhi ya misitu na hifadhi za wanyama. Kinyume utawasikia wakisema hao wana wivu, hawa ni wapinga serikali, hawa hawana akili, wametumwa na mabeberu, hakika watatuhalibia amani na upendo wa nchi yetu

Sasa leo yamemkuta aliyekuwa mtumishi wa Magereza ndugu Shamte (56) staff Surgent alipojikuta akiambulia kiinua mgongo (malipo ya pension ya kustaafu) cha shilingi 21 millioni badala ya shilingi 55 millioni aliyotarajia baada ya kuitumikia serikali kwa miaka zaidi ya 33.Mstaafu huyo aliyasema hayo baada ya kutembelea ofisi za Magazeti ya mwananchi juzi.

"Najiona mfungwa mtarajiwa baada ya kubakia na shillingi 10 millioni kwani shillingi 10 millioni nyingine zimekatwa baada ya kuwa nilikopa chama cha ushirika wa Akiba na Mikopo cha watumishi wa Jeshi la Magereza" alitoa masikitiko yake bwana Shamte akitumia mfano wa mateso ya watu aliokuwa akiwachunga kila siku wakati akifanya kazi gerezani, kwani anajua machungu ya kuwa mfungwa. "Nilitegemea nikanunue shamba la kulima mazao niweze kujisitili baada ya kustaafu sasa haiwezekani, sioni mbele maisha yatakuwaje" bwana Shamte akitoa sentensi kuashiria kukata tamaa ya maisha

"Wewe ndugu, utaratibu wa malipo ya pensheni halipi CGP, waziri husika au katibu mkuu, utalipwa kulingana na michango yako" hayo ndiyo majibu ya kifupi na kukatisha tamaa aliyopewa mtumishi mstaafu ndugu Shamte kutoka kwa wakuu wake baada ya kupata ujumbe wa kiasi atakacholipwa.

Swali la kujiuliza ni, je ? tuko akina Shamte wangapi? akina shamte ambao tunakubali kila kitu watawala wanachopitisha kwa manufaa yao, akina shamte tunaokuwa wa kwanza kuwanyooshea vidole wale wachache wenye akili timamu na uthubutu wa kuhoji haya mabadiliko dhalimu kwa niaba na manufaa yetu, utasikia hawana akili hao, utasikia wamechanganyikiwa hao, nakwambia utasikia wametumwa na wazungu , mabeberu. Wengi wetu tunafikili madhara ya sheria dhalimu , mabadiliko kandamizi haya hayatuhusu sisi, yanawahusu wale tu wanaolalamika.

Hakika bwana shamte amekumbuka shuka wakati kunakucha , amekumbuka jinsi alivyokuwa akiwadharau waliokuwa wakipinga kikokotoo kipya na pengine alishiriki kuwahadhibu walipopelekwa gerezani alikokuwa akifanya kazi, hakika alimalizia kwa kutubu na kusema "Wakati watu wanalia kuhusu kikokotoo nilikuwa naona kawaida,sasa nimeona ukali wake.

Swali la msingi ni, Je...? wewe na mimi tumejifunza nini katika kisa mkasa hiki cha mstaafu Shamte?
Hao wa majeshi ni wapuuzi sana....hata watumishi wa kawaida sisi wanatudharau.....hata mkilalamika katika vikao tu vya gambe ndio wanaenda kutuchoma hovyo sana hao.....
 
Hiyo milioni 10 anunue pikipiki 2 ambazo ni almost 6m awe analetewa hesabu hiyo nne ndiyo akahangaike kutafuta shamba ambalo halitazidi 1m aanze kilimo mdogomdogo ataweza kuwa na uzee mwema kidogo
Boda hawahawa!?? Au Kuna wengine wa kutengeneza kama roboti Eunice!?? ....
 
Naskia Kuna pension ya Kila mwezi je pia nayo hapati?
Kwa KUMBUKUMBU zangu ..... Pensheni ya kila mwezi ni 67% ya mshahara aliostaafia AMBAPO pia Kwa awali alikuwa apokee 75% ya mshahara aliostaafia ..Sasa unajua mshahara wa sajent wa Magereza !??
 
Back
Top Bottom